Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyo haaminiki, aliahidi laptop kila mwalimu, milioni 50 kila kijiji, na Ilani yao ya mwaka 2015 waliahidi katiba mpya, baada ya kupata wakaruka kimanga.
We mfanyabiashara wa nchi gani au Ubelgiji? Unajambo gani hali yakuwa mimi mfanyabiashara wa hapa bongo mi5 kwa JPM kazi iendelee.Yani huyuu mnafki kashawaona wafanya kazi Ni wa wajinga.
Wafanya biashara taree 28 tunajambo Letu.
Wafanyakazi wa Tanzania jamani tusidanganyike na kauli za Magufuli eti ataongeza mishahara na marupurupu awamu hii akirudi tena madarakani. Huu ni uongo wa mchana kweupe. Magufuli ni mjeuri na kiburi sana. Magufuli anachosema sicho anachomaaanisha na anachomaaanisha sicho anachosema. Huyu jamaa ni kigeugeu sana. Nawaaambia mimi safari hii akirudi tena madarakani mujue atakuwa mtu mbaya zaidi kuliko hata alivyokuwa miaka mitano iliyopita. Chondechonde Watanzania wenzangu tushikamane sote kwa pamoja tumpunzishe Magufuli madarakani awamu hii. Tutakuja kujuta na kusaga meno awamu hii iwapo Magufuli akirudi tena madarakani.Nilimsikia Rais Magufuli, katika mkutano wake wa kampeni hapo Jana, huko Bagamoyo mkoani Pwani, akiwaahidi wafanyakazi kuwa atawaongeza mishahara yao wafanyakazi hao, iwapo watamchagua tena katika uchaguzi mkuu ujao!
Hivi si ndiyo huyu huyu Rais Magufuli amekuwa akigoma katakata kuongeza mishahara ya wafanyakazi, kila amapoonbwa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi kutokana na kupanda kwa hali ya maisha kwa wafanyakazi hao, katika kila sherehe za Mei Mosi, kila mwaka tokea aiingie madarakani mwaka 2015, akidai kuwa hawezi kuongeza mishahara wafanyakazi, kwa kuwa katika kipindi hiki anajenga miundo mbinu mikubwa ya reli ya SGR na bwawa la umeme la Stieglers Gorge?
Wakati Rais Magufuli amekuwa akigoma katakata kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa sababu hizo zisizokuwa na mashiko hata kidogo, marais wenzake wote waliomtangulia walikuwa wakiwaongeza mishahara yao wafanyakazi, pamoja na marais hao pia walikuwa wakiendelea kujenga miundo mbalimbali hapa nchini
Hivi Rais Magufuli kutoa ahadi hiyo wakati huu wa kampeni, anatugeuza sisi wafanyakazi wa nchi hii ni wajinga mno na tunaoweza kudanganyika kirahisi hivyo?
Sisi wafanyakazi wa nchi hii, hatudanganyiki tena na Rais Magufuli na tuna jambo letu ambalo tutalitimiza ifikapo Oktoba 28 mwaka huu kwenye sanduku la kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Ninakubaliana na wewe kabisa 100%Magufuli ni muongo huyu jamaa. Hataongeza mishahara hata kidogo. Watumishi wa umma musidanganyike. Safari hii Magufuli akirudi tena madarakani mujue atakuwa mtu mbaya zaidi kuliko hata alivyokuwa miaka mitano iliyopita. Chondechonde Watanzania wenzangu tushikamane sote kwa pamoja tumpunzishe Magufuli madarakani.View attachment 1605624
Tumpumzishe mtu huyu wiki ijayo.Nilimsikia Rais Magufuli, katika mkutano wake wa kampeni hapo Jana, huko Bagamoyo mkoani Pwani, akiwaahidi wafanyakazi kuwa atawaongeza mishahara yao wafanyakazi hao, iwapo watamchagua tena katika uchaguzi mkuu ujao!
Hivi si ndiyo huyu huyu Rais Magufuli amekuwa akigoma katakata kuongeza mishahara ya wafanyakazi, kila amapoonbwa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi kutokana na kupanda kwa hali ya maisha kwa wafanyakazi hao, katika kila sherehe za Mei Mosi, kila mwaka tokea aiingie madarakani mwaka 2015, akidai kuwa hawezi kuongeza mishahara wafanyakazi, kwa kuwa katika kipindi hiki anajenga miundo mbinu mikubwa ya reli ya SGR na bwawa la umeme la Stieglers Gorge?
Wakati Rais Magufuli amekuwa akigoma katakata kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa sababu hizo zisizokuwa na mashiko hata kidogo, marais wenzake wote waliomtangulia walikuwa wakiwaongeza mishahara yao wafanyakazi, pamoja na marais hao pia walikuwa wakiendelea kujenga miundo mbalimbali hapa nchini
Hivi Rais Magufuli kutoa ahadi hiyo wakati huu wa kampeni, anatugeuza sisi wafanyakazi wa nchi hii ni wajinga mno na tunaoweza kudanganyika kirahisi hivyo?
Sisi wafanyakazi wa nchi hii, hatudanganyiki tena na Rais Magufuli na tuna jambo letu ambalo tutalitimiza ifikapo Oktoba 28 mwaka huu kwenye sanduku la kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Huyu mzee hana hata aibu! Yaani anadhani Wafanyakazi wote nchini wana akili finyu kama wale wa Lumumba. HATUDANGANYIKI. Awaongezee wafanyakazi wake wa CCM!Mei mosi zote alikuwa anawaajibu watu utumbo
Acha ramri hizo, atakuwa mbaya zaidi kwani wewe ni mama yake mzazi unajifanya unamjua sana. Watanzania tumechagua ukweli na maendeleleo, tunajua Magufuli akiahidi anatekeleza. Aliposema aongezi mishahara alitoa sababu tukamwelewa, sasa ameahidi kupandisha tunamwamini. Mfano alisema atajenga barabara akajenga, alesema atanunua ndege ilikufufua shirika la ndege amefanya, alisema atanunua korosho kwa bei ya elfu3 kwa wakulina kanunua, acha uzushi wako sisi tuko na mzalendo wa kweli anayetuheshim kwakutuambia ukweli kuliko huyo kibaraka wenu cha domo mropokaji jeuri. #MAGUFULI MI 5 TENA KAZI IENDELEEWafanyakazi wa Tanzania jamani tusidanganyike na kauli za Magufuli eti ataongeza mishahara na marupurupu awamu hii akirudi tena madarakani. Huu ni uongo wa mchana kweupe. Magufuli ni mjeuri na kiburi sana. Magufuli anachosema sicho anachomaaanisha na anachomaaanisha sicho anachosema. Huyu jamaa ni kigeugeu sana. Nawaaambia mimi safari hii akirudi tena madarakani mujue atakuwa mtu mbaya zaidi kuliko hata alivyokuwa miaka mitano iliyopita. Chondechonde Watanzania wenzangu tushikamane sote kwa pamoja tumpunzishe Magufuli madarakani awamu hii. Tutakuja kujuta na kusaga meno awamu hii iwapo Magufuli akirudi tena madarakani.
Wewe si unajulikana kuwa akili yako ina hitilafu.Haha mimi kura yangu ni JPM tu.