Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Alichoongea Rais ni sawa kabisa... huu ni ukweli unaouma..
Mtoto wa shule ya msingi mpaka sekondari anapata mimba maana yake nin?, maana yake kashakua mkubwa huyo aende akalee mtoto.. mwisho tuwe na watoto watakaokua wanaanza michezo ya ajabu mapema ambayo hata vitabu vya dini vimekataza kuzaa kabla ya kuoa au kuolewa....

tuachen kupinga kila kitu
 
Uko NGO gani...!??

Msituharibie maadili...
 
Hivi vi-NGO uchwara vikatafute shimo la kuingia sasa.Vinapewa hela na wezi wa rasilimali zetu,halafu vinakuja kupotosha jamii zetu.Uharibifu double,hatukubali. Hata mjinga anajua kwamba ukiruhusu watoto wanaopata mimba waendelee na masomo, you are encouraging others to do the same.Hawa sijui akili za kijinga hizi wanazitoa wapi na sijui nani kawapandikizia.Nadhani ni roho za kipepo hizi, sio bure. Ku-encourage umalaya kwenye jamii!

Hongera Rais wangu kwa uamuzi huu wa busara mno.Jambo hili lilikuwa linanikera mno.
 
Bado naendelea kufanya utafiti , lakini mpaka dakika hii dalili zinaonyesha kwamba DR JOHN MAGUFULI anaweza kuwa ndiye raia wa Tanzania mwenye ROHO MBAYA ZAIDI KUWAHI KUWEPO TANGU KUUMBWA KWA MBINGU NA ARDHI .

He is too aggressive !
 
hajasema aliempa Mimba aendelee na shule... kasema aliempa Mimba awe mwanafunzi au mtu wa mtaani nae aende jela miaka 30
 
Duh..
Kwa hekima za Raisi Ni wazo zuri..

Mimi Ni mwalimu,lakini kwa hili simuungi mkono hata kidogo..

Watoto wakike wanachangamoto nyingi sana,ikiwemo kutokukomaa kiakili, kubakwa,n.k

Hivyo tukiwaadhibu kwa kuwataka wafikiri kama watu wazima wakati wao Ni watoto tutakuwa hatuwatendei haki.

Ushauri wangu raisi atilie mkazo katika kudhibiti vyanzo vya mimba kwa wanafunzi.
 
Hao wa ulaya unaosema kuwa wamelichukulia busara wana maendeleo kuliko sisi.....sasa makosa ni yapi?
 
Hapo Rais bado hajafanya solution.....mimba kwani hazitoki?
 
Comment za page ya kwanza na kuendelea zinampiga juhudi za rais za kukemea ushoga, Raia wa Tanzania walisha data.... Kama upinzani ndiyo huu wa kutetea mashoga ni bora msajili wa vyama akavifutia usajili vyama vya upinzani vyote....
Sawa Mwanaccm washakusikia
 
Magufuli yuko sahihi. Tunapokea tu kila kitu kama makinda ya ndege, shwaiiin!
 
Mngekuwa walimu, wala msingemlaumu Mh Rais. Kwa kauli hiyo mm sijaona kosa lake hapo. Ni ukweli usiopingika kuwa lazima watoto wetu wazingatie maadili mema hasa wanapokuwa wanafunzi/shuleni. Mtoto akipata mimba in haki asirudi shuleni. Adha inayopatikana huko shule za serikali ni kubwa sana, kufundisha wazazi wenzio ni shida kubwa sana. Hongera mh Rais.
 
Hivi vi-NGO uchwara ndivyo vilivyo wapandikizia mawazo hayo potofu.Mkuu hata ukiwa mwalimu unaweza kupotoshwa.Mwalimu, wanafunzi waamue moja, kusoma au umalaya, hakuna jinsi.Ukiruhusu ujinga huo, utakuwa unahamasisha umalaya mashuleni,hatukubali.Mimi kama mzazi nasema uamuzi wa Rais ni wa busara mno.Hongera zake.Jamii yetu imepotoshwa vya kutosha,enough is enough.
 

kazi gani kubwa kusomesha wazazi wenzio?labda mkileta changamoto zenu tutawaelewa
 

Sioni Rais alipokosea na sio kwamba namtetea..he is very right.Ndiyo maana kaweka exceptional waende private.Kupata mimba kwa mwanafunzi wa kike ni kosa.Kwanza kujihusisha katika mapenzi kwa wanafunzi ni kosa.Tusitake kufanya watu wazidi kukiuka maadili eti wakishusha engine warudishwe darasani..haitakuwa na maana na haimfundishi chochote yule mwingine ambaye hakupata mimba aachane na uzinzi.Kwa hali hii watasoma tuu na hawatawaza uzinzi.
 
Hata aliposema hatatoa chakula cha bure watu hamkumuelewa Rais,matokeo yake watu msimu huu wameingia shambani kwa wingi na hawatachezea tena chakula
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…