Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Wewe sio mzazi. Kama una watoto labda sio wa kike. Kama unao basi sio baba muwajibikaji. Tunaotatizwa na kauli hizo ni sisi wazazi sio hao watia mimba. Wao watatia mimba na watakimbia. Kazi itabaki sisi wazazi tunaotegemea shule hizi za kata!
 
Kama kweli kasema hivyo basi kapotoka sana na sikubaliani naye kabisa.

Mwanafunzi wa kike kupata ujauzito siyo kosa kubwa hivyo hadi anyimwe fursa ya kujiendeleza kielimu.

Hapo adhabu haiendani kabisa na kosa!
Akipata mimba usisahau kuwa atahitaji kunyonyesha na kumtunza mtoto miezi sita. Hawezi akazaa leo akarudi shule kesho utakuwa umezalisha baby mzuka. Amechagua kuzaa, azae na kulea. Kama anataka kusoma aache kuzaa; simple.
 
Kusema ukweli mimi nimechoka na hizi kauli za kuudhi kila siku, sijui hata nifanyeje!
 
Kama kweli kasema hivyo basi kapotoka sana na sikubaliani naye kabisa.

Mwanafunzi wa kike kupata ujauzito siyo kosa kubwa hivyo hadi anyimwe fursa ya kujiendeleza kielimu.

Hapo adhabu haiendani kabisa na kosa!
Wewe unataka mwanao akasome na ujauzito!! Huoni ni aibu mwanao anakwenda shule na mtoto hiyo itakuwa ni vema tuwafundishe maadili ya ukweli wanetu sio kuponda kauli ya rais kuruhusu jambo hilo ni kuruhusu umalaya hadi shule maana hata kinga hawatatumia wakijua shule watasoma tu hata baada ya kujifungua
 
Watanzania bwana kwa ujinga na kujifanya wajuaji ni namba moja...

Kwahiyo mlitaka Raisi aseme "mwanafunzi akipata mimba ni sawa tu, ataendelea na shule..." Big NO, haiwezekani...

Angeruhusu hilo uku mtaani ingekuwa machafuko, mazingira ya watoto wengi wa kitanzania tunayajua. Watoto wangeanza kupigana mimba uku mtaani. Yani mtoto anazaa mtoto. woga saa nyingine unasaidia...

Msilete mambo ya ajabu.... Msitetee mambo ya ajabu...
 
mmmh kinachofwata kutakuwa na ongezeko kubwa la watoaji mimba.
Bora kuliko kusoma na mtoto ni aibu inaonesha mwanafunzi hakufuata maadili ni aibu kwa mzazi kwanza
 
Rais anapokuwa wakwanza kuwanyima watu wake haki yao yakupata elimu basi tupo pabaya sana kama taifa.
Na akiruhusu atakaepata mimba aendelee na masomo tu hakuna msichana atakaepona darasani,wote watapata mimba,chezea wabongo wewe ????!!!
 
Mheshimiwa nimekuunga mkono,Mwenyenzi Mungu aendelee kukuongoza,,
 
Dah, inasikitisha sana kuwaona watu kama nyie mnashangalia suala la mtoto wa kike kunyimwa haki yake ya msingi "Elimu". Kuna msemo usemao "mtoto akiunyea mkono haukati", sasa kwanini mtoto wa kike akibeba mimba anyimwe haki yake. Mm nina mdogo wangu alibeba mimba akiwa shule ila alifanikiwa kuendelea na masomo yake na baada ya kujifungua alilea mtoto miezi mitatu akarudi shule kama kawaida. Mimba sio ulemavu na kupata mtoto sio mwisho wa maisha.


Akipata mimba usisahau kuwa atahitaji kunyonyesha na kumtunza mtoto miezi sita. Hawezi akazaa leo akarudi shule kesho utakuwa umezalisha baby mzuka. Amechagua kuzaa, azae na kulea. Kama anataka kusoma aache kuzaa; simple.
 
Mama samia anasemaje kuhusu hili? Maana kuna cku ktk kuptapta mitandaon nkakuta chanzo flan hv et kmeandka mama anampango wa kuwafany watoto wa kike waliopata ujauzto warud shulen,sasa hii imekuaje jaman? Wacha m nbak neutral sina tim
 
Hii italeta adabu kwa mtoto wa kike
 
hata msipowarudisha shuleni,hamjakata mzizi,

wasichana na wavulana at that age,wanajifunza kuexperiment mambo mengi yanayotokea/kubadilika na baiolojia zao,

hio ni nature,

hata nchi zilizoendelea kabisa,tatizo la mimba shuleni ni la kawaida.
Sawa! Wewe unashauri nini? Hizo nchi zingine zinafanyaje kuhusu hili?
 
Bora kuliko kusoma na mtoto ni aibu inaonesha mwanafunzi hakufuata maadili ni aibu kwa mzazi kwanza
mmmh yani bora kutoa mimba???? kuliko kuwa na mtoto???alitakiwa kuboresha mazingira mazuri ya elimu ili kuzuia haya yote.
 
Ili usiwape ajira kama sasa, angekuwa mtoto wako ungesema hivyo. Shida mnazungumza theory na sio practical.
 

Mtu kuwa na mtoto ni jambo la aibu?

Bure kabisa wewe!!!!
 
Well said mkuu
 
Huyu anataka bei ya kutoa mimba ipande sasa! Ghafla ukimimbisha mchepuko itakugharimu parefu maana demand kubwa kitoka kwa students!
 
Kama kweli kasema hivyo basi kapotoka sana na sikubaliani naye kabisa.

Mwanafunzi wa kike kupata ujauzito siyo kosa kubwa hivyo hadi anyimwe fursa ya kujiendeleza kielimu.

Hapo adhabu haiendani kabisa na kosa!
Huwezi kusomesha wajawazito,, dunia nzima hakuna, hata ULAYA hawafanyi hivyo, Ukizaa unasoma kama mtu mzima, ukichanganywa na watoto wataiga mwenzao,,kale kamchezo lazma kawekewe sheria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…