Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Hivi MAGUFURI HAYO MANENO UWA UNASEMA KAMA MANENO BINAFSI(PRIVATE ) KAMA MSOMI AU VIPI

Shida moja ya nchi yetu naimani ni kutokuwa na sheria na kifuatacho ndio maana rais au mtu mwenye mamlaka akisema kitu tunadhani ndio mwisho wa usemi na mwisho wa mjadala. Sasa rais kuamka kusema mambo hivi inamaana haipo sheria inayoongelea wanafunzi wanaopata mimba. Au yeye ndio mtungaji sheria wa nchi. Kama yeye ni mtungaji sheria wa nchi tuelewe.

Sababu mara kibao nimesikia mara hivi mara hivi. Hivi weww rais magufuri uwe wakati unaongea unasema hivi naongea kama binafsi au naongea kadiri ya sheria. Ili asiwepo mtu hata kama ni rais azungumze juu ya sheria na kwa mabavu. Hivyo hatuendi na utatufikisha pabaya.Hata viongozi wengine unakuta anaropoka tu sasa I amaana haipo sheria hadi tufikie kusema katika uongozi wangu. Au katika sheria tulizo jiwekea.

Tuache ushabiki wa maneno maneno au kutaka kujikuza katika madaraka ya mtu aliyonayo. Hii sio sahihi. Tufuate sheria ndio haki na mwelekeo. Sio "mimi katika uongozi wangu", hii sentensi ni ya ajabu. Ni ya ajabu maana;
1.Kwa hiyo kiongozi atakae kuja nae aje na amri yake. Je itakuwa nchi au jalala la kujiamlia na kuumiza wa chini.
2. Ni sheria sasa iandikwe kwenye mkutano wako au tunatunga sheria kwa chombo gani.

Nieleweke siko upande wowote ila baadhi ya kauli zinazotolewa na viongozi wetu sio nzuri. Bali ukiwa mkutanoni tueleze mambo ya maendeleo lakini suala la kuamua sheria ya watoto kusoma au kutosoma ipitishwe na chombo cha kutunga sheria sio kusimama au kuamka kwenye kitanda chako na kwenda mkutanoni unaropoka ropoka ili kwa mawazo yako ya siku hiyo ichafue Tanzania yetu yenye sheria zake.

Tunakuheshimu ila sio maana ukikosea sheria zilizopo usiambiwe itakuwa upofu wa ajabu sana.

Kwa hili ukubali umeamka kitandani bila kufikiria maneno ya kusema. Na ni hatari sana ukiendelea hivi.
 
Lakini kumbuka zila adha azipatazo mwanafunzi mja mzito, kumbuka aina ya mtazamo anaoweza kuuambukiza darasani kwa wale wenzake ambao hawajawahi kupata uja uzito.
Ni bora kukemea mitazamo inayowakuza wanafunzi kwenye mambo ya ngono na kuweka mkazo kwenye fikra za utafutaji wa elimu.
Starehe za kimaisha mtoto wa kike atazikuta tu huko mbeleni, tena atazichoka, kwanza akili itulizwe darasani.
Basi suluhisho ni kwa serikali kujenga shule maalum kwa ajili ya waliojifungua ili 'wasiwaambukize' wenzao tabia 'mbaya' na sio kuwanyima fursa ya elimu.

By the way, nimefurahi kuona kuwa unaamini ujauzito ni upele au kipindupindu kwamba unaambukiza😛😛.
 
KWA KAULI YA MH.RAIS NATAMANI HATA NIMPE ZAWADI YA KUKU TU ILA SIJUI ITAMFIKIAJE. AMENIFURAHISHA SAAANA! WOTE TUNAJUA MAPENZI NA ELIMU NI SUMU NA MSHIKA MAWILI MOJA HUMPONYOKA! WAAMUE AMA SHULE AU MIMBA!
Kwa kusema hivyo yeye ndo mtunga sheria au yuko juu ya sheria. Nini kinachotuongoza sheria au maneno ya mkutanoni.
 
akiongea akiwa bagamoyo kwenye uzinduzi wa barabara ya bagamoyo msata chalinze rais amekemea vikali sana wote wanaopigia debe eti wanafunzi wazalishwe halafu waendelee na masomo, rais amesema hili haliwezekani na ole wake awaye....ole wake anatakayezaa halafu arudishwe shuleni. ole wake atakayempa mimba mwanafunzi halafu sheria imuache akirandaranda mitaani.
Kwani Ja.neet katoa ngapi kabl ya kuwa pale alipo?
 
Mbona kauli kuhusu suala la mimba zinachanganya?? Waziri wa afya, makamu wa rais na rais kauli zao zinatofautiana.
Hii awamu hawajawahi kuwa na safu inayoonana. Kila mtu na lwake. Mwisho rais anatoa uamuzi unaoacha tahayari au anatumbua alieenda tofauti.

Kuna wakati humu ilisemwa mtu na makamu wake hawaelewani. Hili la mimba ni ushahidi tosha. Laiti kama inafaa kutumbua makamu!!
 
Habari wanaJF,

Leo akiwahutubia wakazi wa Bagamoyo, Mkoani Pwani. Rais Magufuli amesema hakuna Mwanafunzi aliyebeba ujauzito atakayerudi shule katika utawala wake. Akaongeza kuwa hawezi kufanya kazi ya kusomesha wazazi.



" Inaweza kufika kipindi darasa zima linawatoto, Mwalimu akifundisha wao wanatoka nje kwenda kunyonyesha".

Hata kama ni watoto wangu, yani nikupeleke shule alafu upate mimba nikurudishe? Aende akapate mimba aone kama nitamrudisha.

Mimi nimetoa fedha ili mwanafunzi asome bure, halafu leo mtu apate mimba arudi shule? Ndani ya utawala wangu, haitotokea.

Wakati mwingine ukizikiliza hizo NGOs zitakuwa zinalipeleka taifa pabaya. Ndani ya utawala wangu haitotokea. NEVER.

Hizi NGOs kama zinawapenda sana hao watoto zikafungue shule zao za kusomesha wazazi. Serikali haiwezi kuwasomesha.

Hawa wanaotuletea haya mambo hawatupendi ndugu zangu. Wametuletea dawa za kulevya, wameleta ushoga ambao hata ng'ombe hawana.

Huku kuiga iga tutakuja kuiga mambo ambayo hata hayafai. Wanakuja na misaada ambayo ni mali zetu wametuibia.

Nyie wafugaji mmefuga lakini hamjawahi kuona hata mbuzi au nguruwe amekosea huu mchezo. Lakini wao wanataka Watanzania wakosee.

Wakati huo huo, Rais amesema kuwa anawaomba msichukue maeneo ya Magereza, hata mimi nikifungwa siku moja nipate sehemu ya kulima.

Rais Magufuli ametoa eneo la ekari 65 kwa wananchi lililokuwa na mgogoro kati yao na Jeshi la Magereza.

Pig up sana mr presedent
 
Habari wanaJF,

Leo akiwahutubia wakazi wa Bagamoyo, Mkoani Pwani. Rais Magufuli amesema hakuna Mwanafunzi aliyebeba ujauzito atakayerudi shule katika utawala wake. Akaongeza kuwa hawezi kufanya kazi ya kusomesha wazazi.



" Inaweza kufika kipindi darasa zima linawatoto, Mwalimu akifundisha wao wanatoka nje kwenda kunyonyesha".

Hata kama ni watoto wangu, yani nikupeleke shule alafu upate mimba nikurudishe? Aende akapate mimba aone kama nitamrudisha.

Mimi nimetoa fedha ili mwanafunzi asome bure, halafu leo mtu apate mimba arudi shule? Ndani ya utawala wangu, haitotokea.

Wakati mwingine ukizikiliza hizo NGOs zitakuwa zinalipeleka taifa pabaya. Ndani ya utawala wangu haitotokea. NEVER.

Hizi NGOs kama zinawapenda sana hao watoto zikafungue shule zao za kusomesha wazazi. Serikali haiwezi kuwasomesha.

Hawa wanaotuletea haya mambo hawatupendi ndugu zangu. Wametuletea dawa za kulevya, wameleta ushoga ambao hata ng'ombe hawana.

Huku kuiga iga tutakuja kuiga mambo ambayo hata hayafai. Wanakuja na misaada ambayo ni mali zetu wametuibia.

Nyie wafugaji mmefuga lakini hamjawahi kuona hata mbuzi au nguruwe amekosea huu mchezo. Lakini wao wanataka Watanzania wakosee.

Wakati huo huo, Rais amesema kuwa anawaomba msichukue maeneo ya Magereza, hata mimi nikifungwa siku moja nipate sehemu ya kulima.

Rais Magufuli ametoa eneo la ekari 65 kwa wananchi lililokuwa na mgogoro kati yao na Jeshi la Magereza.



Tanzania ina inashika mkia kwa elimu, kwasababu kila Rais wetu aliyeingia madarakani elimu waliiweka kitu cha mwisho huku wakisomesha watoto wao. Umasikini kwenye jamii ambao ndiyo wengi ni kukosa elimu. Wakati Rais wetu anasema bila ya aibu na mawazo yake ya kizamani hasoneshi wazazi, wazazi anaowaita ni watoto waliopata mimba kwa shida mbali mbali, hana Wakati wa kuwasikiliza, ni kuwazika wazima kwa kuwapa adhabu bila ya haya. Rais Magufuli hapa anavunja haki za binaadamu, na hii itamvunjia heshima yake ulimwenguni Kate na yote anayoyafanya yataonekana hovyo. Wakati anasema hivyo nchi jirani wamepitisha kwenye katiba yao mtoto wa kike asikataliwe masomo kwajiri ya ujauzito. Tatizo la mamba Tanzania ni kubwa zaidi kati ya nchi za East Afrika, hii kwasababu ya kukosa elimu na ugumu wa maisha ya watoto wengi wao wanatoka kwenye familia masikini, kwa hiyo Tanzania kwa semi wa Rais Magufuli, ukizaliwa masikini hakuna chance ya maisha ni kufa masikini. Leo Tanzania Pamoja na Mali zote tunakuwa masikini, jibu, miaka NENDA miaka rudi Viongozi wetu wametunyima elimu ya maana. Nyerere alikosea, lakini hawa wote waliokuja nyuma yake walikuwa na nafasi ya kuribadilisha hili taifa, lakini wamelididimiza kwa kudharau kudumisha elimu. Ukimuelimisha mama unaelimisha familia nzima.

 
Kabisa hizi NGOs zinamambo ya ajabu kweli ilifika wakati wakawa wanagawa hadi vilainishi eti kuzuia michubuko.!
Hazifanyi kazi kiwiziwizi lakini, tusiangalie tulipoanguka pia tuangalie pale tulipojikwaa.
 
japo simkubali sizonje ila hili aliloliongea kuhusu ushoga ni ukweli mtupu hata wanyama hawaingiliani kinyume na maumbile
 
Kwa kusema hivyo yeye ndo mtunga sheria au yuko juu ya sheria. Nini kinachotuongoza sheria au maneno ya mkutanoni.
kasisitiza tu hajatubga sheria kama sheria ipo miaja mingi tu kaamua kukukumbusheni
"SERIKALI HAITOSOMESHA WAZAZI!" WANATUHARIBIA WENZAO WADOGO WAONE NI JAMBO LA KAWAIDA KUZAA UKIWA MWANAFUNZI
 
Kwani lini wanafunzi walikuwa wanaruhusiwa kuzaa na kurudi shule? Maana yake utoaji mimba upo hadi sasa. Kuna taasisi ambazo wazazi wanarhusiwa kusoma ila rais kasema serikali yake haiwezi kusomesha wazazi. Hivyo waendelee na masomo sehemu ambazo serikali haigharimii. Hajakataza wasome.
kuna watu tunawajua wamezaa na kurudi shule na mmoja alikuwa anasoma jangwani, na hili linafahamika. ??

utoaji mimba upo lakini hauwezi kulinganisha na haya makatazo ambayo yanawekwa yataongeza zaidi

huyo rais hawezi kusomesha wazazi mbona makazini anasomesha wazazi???
 
Basi suluhisho ni kwa serikali kujenga shule maalum kwa ajili ya waliojifungua ili 'wasiwaambukize' wenzao tabia 'mbaya' na sio kuwanyima fursa ya elimu.

By the way, nimefurahi kuona kuwa unaamini ujauzito ni upele au kipindupindu kwamba unaambukiza😛😛.
Umenielewa vibaya kwa bahati mbaya. Ndio maana mkuu kaziambia hizo NGOs ziwajenge shule hao mabinti wanaopata uja uzito.

Sooth, kumbuka kuwa kimtazamo dada mwenye uja uzito au aliye tayari na mtoto anakuwa ameshapevuka kiakili kulinganisha na wenzake mle darasani. Hao wenzake hawatakawia kuona kwamba uja uzito masomoni ni jambo jepesi tu.

Na ni dhana mbaya sana kwa mfano kwa darasa zima kuwa na wasichana ambao akili zipo nusu darasani na nusu kwenye fikra za kwenda gesti jioni.

Madhara mengine ya mchanganyiko wa mwanafunzi aliyejifungua na wale ambao bado, unaweza hata kuonekana kwenye vyombo vya usafiri, unakuta kundi la wasichana wanaongea mambo ya kiutu uzima mbele ya mzee anayeweza kuwa babu yao au bibi yao.

Sababu ni kule kuwahi kujihusisha na ngono wakiwa bado wapo shuleni. Utotoni mwetu miaka ya 80 ilikuwa ni vigumu kwa kundi la wasichana kujiachia kimaongezi mbele ya watu wanaoweza kuwa wazazi wao.
 
Back
Top Bottom