Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Rais Magufuli: Sitasomesha Wanafunzi waliopata ujauzito, siwezi kusomesha Wazazi

Serikali inapaswa kurudi kwenye wajibu wake wa kusimamia sheria halali zilizotungwa na bunge dhidi ya kunajisi na kubaka watoto wa shule badala ya kupanga kuwaadhibu wahanga wa jinai hizo kwa kuwakatishia elimu.
Malengo ya elimu ya msingi na sekondari ni maendeleo binafsi ya mwanafunzi, kuwafanya watoto kuwa raia wema na kuwaandaa kujitafutia vipato vyao maishani na hivyo kuliingizia taifa mapato.
Kuwazuia wasichana wasiendelee na masomo kwa sababu tu wamepata uja uzito ni kulikomoa taifa lote na si wanafunzi husika tu.
 
Mtoto mdogo aadhibiwe kwaajili gani? Na ukute aliyempa mimba ni mwanaume mtu mzima. Hapa ni kuhalalisha ubakaji kwa watoto wetu. Watu wanayafurahia hayo maamuzi ili waendelee kunyanyasa watoto wadogo wa kike. Shame on you!
 
Katika Mh. Rais anatukumbusha kuboresha malezi ndani ya familia zetu na si vingine wazazi na walezi tulijisahau sana ktk usimamizi mzima wa malezi kwa watoto wetu
 
Mtoto anakosa haki ya kupata elimu tena kwa familia ambazo hazina uwezo wa kumpeleka private school
 
Halafu Mzee Rungwe bado unabisha kuwa nchi haijapinda?!!😀😀😀😀
Ile video clip ya mzee rungwe nilishindwa kuifuta Ni ushahidi tosha kuwa tz hamna haina viongozi
 
  • Thanks
Reactions: Mj1
Sio kwa kusomesha wajawazito kwa ghalama ya serikali, tuwe na uelewa, kwa hilo maana hakuzuhia masomo ya QT wala masomo ya kujilipia. hapo ana tukumbusha tuongee na watoto wetu mara kwa mara ilikuweza tambua mwenendo na si mradi mtoto yupo shule ni mtoto wa shule na si wa mtu fulani aliye mleta shuleni kwa malengo ya kusoma.
 
Mtoto anakosa haki ya kupata elimu tena kwa familia ambazo hazina uwezo wa kumpeleka private school
Wapo watoto wachache wamepata mimba kwa kubakwa kwa nguvu lakini wengi hubakwa kwa hiyari(makubaliano na under 18).Kuna msemo mmoja aliutumia JK kuhusu hawa watoto ni kweli kabisa kama huamini kaa karibu na wanafunzi, wakati wewe unamchukulia kama mtoto mwenzio anajiona mtu mzima mwenzio na hakuogopi kimahusiano. Sasa hivi mwanafunzi asiye na mpenzi huonekana mjinga na mwenye mpenzi huonekana mjanja. Ata kama serikali itawaruhusu kusoma haitakiwi Rais atangaze maana watu hawatawajibika watazitafuta mimba kwa kudhani hakuna kitakachoharibika.
 
Wakati mnapongezana ujinga lazima muelewe,kuna watoto wanabakwa wakiwa wanatembea kwenda mashuleni hasa vijijini ambako shule ziko mbali, njia ni mapori. Na asilimia kubwa ya mimba za utotoni ni Vijijini.
 
Wakati mnapongezana ujinga lazima muelewe,kuna watoto wanabakwa wakiwa wanatembea kwenda mashuleni hasa vijijini ambako shule ziko mbali, njia ni mapori. Na asilimia kubwa ya mimba za utotoni ni Vijijini.
Nadhani paragraph ya tano kwa maoni yang nimeligusia kidogo hili suala la kubakwa, hata na mie pia nilikua mtoto wa kike ndio mana nikaileta makala hii
 
Wakati mnapongezana ujinga lazima muelewe,kuna watoto wanabakwa wakiwa wanatembea kwenda mashuleni hasa vijijini ambako shule ziko mbali, njia ni mapori. Na asilimia kubwa ya mimba za utotoni ni Vijijini.
Tunaishi kwenye jamii na tunaona jinsi visichana vya shule hasa sekondari vinavyokimbizana na vijana na Wababa waliowazidi umri.Huo Upuuzi wa kusingizia kubaka futa, ndio nyie Mnasemaga bikra ilitoka kwa kuendesha baiskeli Kumbe umeanza ngono na miaka 10.
HATUSOMESHI WAZAZI
 
Typically unaandika rubbish
Mkuu tens acha kabisa kuongea ivyo nano kalazimishwa kama sio ushenzi wao wenyewe, wamekuwa seduced na mafataki
Hakuna mtoto anaetoka nyumbani na nia ya kwenda kufanya mapenzi, wengi wanalazimishwa na watu wazima, walimu n.k. sasa mtoto innocent kama huyo unamnyimaje fursa ya kusoma.
 
Hongera kwa uchambuzi huu!
Na afterall Tanzania haijawahi kuruhusu wasichana wenye mimba au waliozaa masomoni kurudi shule tokea zamani, labda kwa private schools.
 
Raisi wetu anataka kuongea juu ya kila kitu hii inamfanya kuonekana hajui kitu.

Suluhisho ni hili;
Elimu ya uzazi itiliwe mkazo siyo miaka yetu tunaangalia kitabu cha la sita kina picha ya ub00 darasa zima tunacheka.
Na mwalimu anaona aibu mada anaigusia gusia tu matokeo mwanafunzi anapata hedhi hata hajui na hakumbuki kama alishawahi kusoma hiko kitu.

Tunafuata uzazi wa mpango, achana na kauli yake ya kusema tufyatue tu watoto, uzazi wa mpango kinagaubaga unaruhusu abortion.

Iwekwe kisheria kua abortion imeruhusiwa, watoto wafundishwe juu ya after morning pills na vidonge vya kucounter mimba zisizotarajiwa.

Watakaobakwa wawahishwe hospitali watakingwa hata na ukimwi.
 
Binti Kapewa Mimba Kafukuzwa Shule, Aliempa Mimba Kafungwa Miaka 30 Jela, Mtoto Atakaezaliwa Atatunzwa Na Mama Alipigwa Mimba Akiwa Shuleni, Kazi Yake Kwa Sasa Ni Baa Med, Huyo Mtoto Wa Bar Maid Na Baba Alifungwa Segerea Unategemea Yeye Pia Kama Ni Wa Kike Ataachaje Kudungwa Mimba Kama Mama Yake,....huu Utakuwa Mzunguko Hadi Hapo Tutakapo Jua Hawa Tunaowahukumu Ni Watoto, Nakubaliana Na Raisi Kuwa Wasirejee Shule Na Wapatiwe Skill Za Maisha, Kama Cherehani Na Ufundi Mwingine, Serikali Iwawekee Programu Maalumu Ili Wasibaki Kuwa Walezi Hali Ya Kuwa Nao Wanalelewa
 
Kwa hiyo Veta Ni Taasisi ya Elimu isiyo na Heshima? Je Na Wavulana Watakaowapa Watoto wa Kike Magufuli Atawafukuza Pia? Au ni selective justice!
Mkuu tafuta clip ya rais akiongea Bagamoyo, halafu isikilize vizuri kabla hujafikia hatua ya kutoa maoni. Nenda youtube utaiona.
 
Tunaishi kwenye jamii na tunaona jinsi visichana vya shule hasa sekondari vinavyokimbizana na vijana na Wababa waliowazidi umri.Huo Upuuzi wa kusingizia kubaka futa, ndio nyie Mnasemaga bikra ilitoka kwa kuendesha baiskeli Kumbe umeanza ngono na miaka 10.
HATUSOMESHI WAZAZI
Samahani kwa hili swali mkuu. Umemuuliza mama yako alikuzaa akiwa na umri gani. Siwatetei wanaopata mimba shuleni, ila hao unaowasema ni asilimia ndogo wanaopata mimba ,kwani wanajua hadi kumeza vidonge vya kuzuia mimba au kutoa.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
A

..nakuelewa.

..sijui umri wako, lakini enzi zangu shule za sekondari zilikuwa tofauti kwa wavulana na wasichana.

..naamini mazingira hayo yalitusaidia kutuepusha na vishawishi vya ngono.

..lingine lilikuwa ni marafiki niliokua nao. Wengi walikuwa makini sana ktk masomo na hawakuendekeza starehe.

..mazingira sasa hivi yamebadilika. Shule ni za mchanganyiko.
Ni kweli shule za mchanganyiko. Pia mavazi na simu za mikononi ni mtego mwingine wa kuwanasia wanafunzi wa kike.

Umbali wa kutoka nyumbani kwenda shuleni ukichanganya na pato dogo la wazazi, pia huchangia mimba za shuleni.

Unakuta mwanafunzi anaishi Bunju B na anasoma Benjamini Mkapa pale Ilala...kila siku aamke saa kumi na moja na kuanza shughuli ya usafiri kwenda shuleni, ni mtihani kwao.

Kuna dada mmoja miaka ya 2000 mwanzoni alikuwa akitembea na dereva wa daladala, kwa sababu tu binti alikuwa haiwezi ile shughuli ya kugombea kuingia ndani kupitia mlangoni, hivyo dereva akawa anamruhusu aingie kupitia mlango wake.

Yapo mengi ambayo kwa kweli ni chanzo cha hawa mabinti kujikuta wameingia kwenye mtego wa mahusiano wakiwa shuleni.
 
Ni kweli shule za mchanganyiko. Pia mavazi na simu za mikononi ni mtego mwingine wa kuwanasia wanafunzi wa kike.

Umbali wa kutoka nyumbani kwenda shuleni ukichanganya na pato dogo la wazazi, pia huchangia mimba za shuleni.

Unakuta mwanafunzi anaishi Bunju B na anasoma Benjamini Mkapa pale Ilala...kila siku aamke saa kumi na moja na kuanza shughuli ya usafiri kwenda shuleni, ni mtihani kwao.

Kuna dada mmoja miaka ya 2000 mwanzoni alikuwa akitembea na dereva wa daladala, kwa sababu tu binti alikuwa haiwezi ile shughuli ya kugombea kuingia ndani kupitia mlangoni, hivyo dereva akawa anamruhusu aingie kupitia mlango wake.

Yapo mengi ambayo kwa kweli ni chanzo cha hawa mabinti kujikuta wameingia kwenye mtego wa mahusiano wakiwa shuleni.

Na mzazi kama hauna uwezo kwanini umpeleke mwanao shule ya mbali wakati shule za karibu zipo? Pili wewe mtoto tamaa ni zanini kwanini wewe upate mimba mbona wengine hawapati? Ni kiherehere hicho na tamaaa
 
Back
Top Bottom