Hili swala la corona kiukweli Tanzania imefanya vizuri, wengi wetu humu ni watanzania ,tukiangalia hata kwenye makazi yetu hakuna vifo vya marafiki, ndugu wala jamaa kwa gonjwa hili, sijui kimefanyika nini Tanzania lakini ni hali ambayo ipo, mimi sioni umuhimi wowote kwa baadhi ya watanzania kuendelea kulazimisha lockdown, au sijui tufanye kama nchi zinge ,scenarios ni tofauti.
Binafsi ni miongoni mwa watu walioogopa sana gonjwa hili hata kuomba serikali tuingie lockdown lakini serikali haukufanya vile na madhara hakuna, kwa hiyo sio kila kitu kinachofanyika nchi zingine kifanyike Tanzania, labda la muhimu ni kwamba tuendelee kuchukua hatua basi.