Rais Magufuli: Sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani (Covid19), tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya. Akemea Chanjo

Rais Magufuli: Sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani (Covid19), tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya. Akemea Chanjo

Hamasa ya upandaji wa miti huko Chato na Dodoma ihimizwe kufanyika nchi nzima hasa Shinyanga, Simiyu, Mwanza, Singida, Pwani, Lindi, Mtwara, Kigoma, Morogoro, Rukwa, Katavi, Mara, Manyara, Arusha, Tanga, Ruvuma, Tabora, Njombe, Iringa, Mbeya, Kilimanjaro na Dar Es Salaam.

Msitu wa kupandwa wa Mafinga Iringa, Morogoro, Tanga na Arusha zilianzishwa na Mwalimu Nyerere. Enzi za Mwalimu Nyerere mwaka 1977-1979 wananchi vijijini walikuwa wanaenda kupanda na kupalilia miti ya serikali na kupata ujira wa unga wa njano au ngano aina ya buruka. Miti lishamiri sana na hali ya hewa ilitamalaki mvua za kutosha lakini baada ya soko huru kufunguliwa na sera za serikali kutokuwa na mwelekeo unaotabirika wajanja wachache kutoka serikalini walihujumu rasilimali hizo kwa kukata miti kwa ajili ya mbao, kuni na mkaa; mfani kule Kibaha kulikuwa na mapori ya miti ya mikorosho kuanzia Kongowe ingia ndani kupita Chuo kikuu cha Open yalitelekezwa na watu binafsi wakahodhi kisha kuanza kuuzia mtu mmoja mmoja.

Miti ya vivuli, matunda na mbao inatija kama hamasa itazingatiwa kwa nchi nzima ambapo itasaidia sana kurekebisha uchafuzi wa mazingira, kulinda vyanzo vya maji, kulinda viumbe hai adimu kama vipepeo, vyura (Kihansi Morogoro, Ruhuji Njombe, Ziwa Ngozi kule Rungwe Tukuyu, Amboni Tanga, Mlima Mbeya, Milima Livingstone and Kipengele kule Njombe na Ruvuma, Kondoa Irangi, Uvinza Kigoma kwenye mto Malagarasi, Ilolangulu na Sikonge Tabora, Bonde la mto Simiyu kule Magu na Gamboshi, Ziwa Kindai an Singida kule mjini Singida nk
 
Kwa sasa kinachoendelea ni utambulisho wa viongozi ikiwemo wizara na idara za serikali. Waliokuwepo kwa uchache ni Dkt. Damass Ndumbaro, Medadi Kalemani ambae ni mbunge mwenyeji na waziri wa nishati, Dotto Biteko ambae ni waziri wa madini, Elias Kwandikwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Waziri wa maji, Jumaa Aweso na Marry Masanja Naibu waziri wa Utalii. Pia yupo Mwita Waitara naibu wa Mazingira.

Pia upo uongozi wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii, wapo wakurugenzi, wakuu wa taasisi ikiwemo Tawa, Tafori na DTI. Upo pia ungozi wa mkoa wa Geita ukiongozwa na mkuu wa mkoa, makatibu tawala na manaibu wao, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, kamati ya usalama wilaya ya Chato, viongozi wa chama cha Mapinduzi Geita, viongozi wa dini mkoa na wilaya pia wabunge wa mkoa wa Geita.

=========

Medard Kalemani: Mheshimiwa Rais wetu, sisi wananzengo na wananchi wa Chato kwa siku ya Leo ni siku ya furaha kubwa na kwetu sisi ni siku ya kihistoria, nichukue nafasi hii kwa niaba ya wananzengo na wananchi wa Jimbo letu na wilaya yetu ya Chato, kwanza kabisa kuwakaribisheni Chato.

Chato ndugu zangu ni nchi yetu sote, naomba wananchi wa Chato tuwapigie makofi wageni wote waliofika hapa.

Nimesikia huu ni msitu wa pili kwa ukubwa nchini kwetu, hongereni sana. Pia msitu ni wa kwanza kwa aina ya misitu mchanganyiko, misitu ya kupanda na misitu asili. Eneo hili limetoa ajira na watumishi na wafanyakazi ni wanaozunguka maeneo haya.

Mheshimiwa Rais na ndugu wananchi, kwa heshma ya pekee napenda nitoe shukrani ya moyoni, hawa wananchi walioko hapa kama kawaida ya misitu mmetupatia chakula, nawaomba wananchi tushangilie sana. Kitendo cha kutupatia ng'ombe wanne wakubwa madume yaliyonona kwa ajili ya wananchi hawa kula walau leo mchana na kilo 1,500 kwa ajili ya chakula cha mchana tunawashukuruni sana, wananchi tupige makofi na vigerere kwa ushirikiano huu mzuri. Mheshimiwa Rais na Waziri baada ya kusema hayo, niwashukuruni sana kwa kunisikiliza.

10:20 Asubuhi: Rais John Magufuli amewasili eneo la tukio na kupokewa na viongozi kadhaa kisha kuimbwa wimbo wa Taifa na wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Baada yahapo zimefata Dua na Sala kutoka kwa viongozi wa dini.
Mwambieni mkuu huku kwetu TANGA - Lushoto, kuna mashamba ya miti makubwa zaidi ya hayo, waje wazindue kama vya kuzindua vimeisha .........
 
Magu ni denialist, kama hataki chanjo sisi tunaitaka. Sisi wengine hatutaki kufa.

Magu anakiri kua corona ipo kuna watu wameileta ila hataki hata kuhamasisha watu wachukue tahadhari, anapongeza watu wasiovaa barakoa.

Yeye anaamini corona imeletwa na wazungu ili waje kuichukua Afrika.

Kama chanjo mbaya tukatae chanjo zote, sio ya corona tu, tukatae za malaria, kifua kikuu, typhod, kichocho, kansa. Ikiwezekana tufute wizara ya afya na serikali isinunue madawa, tupambane na tiba za asili na maombi ili tuepuke wazungu wasije kuchukua nchi yetu.

Akili za viongozi wetu
 
sisi watanzania hatujajifungia ndani na hatutegemei kujifungia ndani na wala sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani kwa sababu Mungu wetu yuko hai
Yaani ktk hili niko na wewe JPM 100%. Japo sikupendi na wala sikukuchagua na hata sikubali ushindi wako ktk uchaguzi mkuu wa 2020.
 
Magu ni denialist, kama hataki chanjo sisi tunaitaka. Sisi wengine hatutaki kufa.

Magu anakiri kua corona ipo kuna watu wameileta ila hataki hata kuhamasisha watu wachukue tahadhari, anapongeza watu wasiovaa barakoa.

Yeye anaamini corona imeletwa na wazungu ili waje kuichukua Afrika.

Akili za viongozi wetu
Tatizo lake anajiona ni infinit
 
Magu ni denialist, kama hataki chanjo sisi tunaitaka. Sisi wengine hatutaki kufa.

Magu anakiri kua corona ipo kuna watu wameileta ila hataki hata kuhamasisha watu wachukue tahadhari, anapongeza watu wasiovaa barakoa.

Yeye anaamini corona imeletwa na wazungu ili waje kuichukua Afrika.

Akili za viongozi wetu
Nadhani wazungu wakitaka kuichukua Afrika hawashindwi, hata kwa mabomu ya maangamizi ya watu ..... weapons of mass destruction
 
Magu ni denialist, kama hataki chanjo sisi tunaitaka. Sisi wengine hatutaki kufa.

Magu anakiri kua corona ipo kuna watu wameileta ila hataki hata kuhamasisha watu wachukue tahadhari, anapongeza watu wasiovaa barakoa.

Yeye anaamini corona imeletwa na wazungu ili waje kuichukua Afrika.

Akili za viongozi wetu
Waoga saaana wa Corona inawasepesha!!

Inaonesha jinsi ulivyomuoga, Rais alivyosisitiza koote huko kuhusu kuchukua hatua na tahadhari juu Corona, wewe umeskia Neno la yeye kukataa kinga pekee??

Chukua tahadhari mpuuzi wewe
 
Back
Top Bottom