Rais Magufuli: Sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani (Covid19), tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya. Akemea Chanjo

Rais Magufuli: Sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani (Covid19), tutaendelea kuchukua tahadhari zingine za kiafya. Akemea Chanjo

Anayejiita Mwendawazimu anabishana na WHO!!! Sasa kwanini asitangaze Tanzania inajitoa WHO kwa kuwa ni WAONGO chanjo zao zote ni bomu? [emoji15]
Taahira kweli wewe
 
Mtatishwa sana ndugu zangu Watanzania lakini simameni imara, ninajua wapo baadhi ya Watanzania wameondoka ndani ya nchi na kukimbilia maeneo mengine na kwenda kuchanjwa na walipochanjwa huko, wamekuja huku wametuletea Corona ambayo ni ya ajabu ajabu, simameni imara.

Chanjo hazifai, kama wazungu wangekuwa na uwezo wa kuleta chanjo, hata chanjo ya Ukimwi ingekuwa imeshaletwa, hata chanjo ya kifua kikuu, kifua kingekuwa kimeshaondoka, hata chanjo ya maleria ingekuwa imeshapatikana, hata chanjo ya kansa ingekuwa imeshapatikana.

Ni lazma Watanzania tuwe waangalifu kwa mambo ya kuletewa letewa, msije mkafikiria mnapendwa sana. Taifa hili ni tajiri, Afrika ni tajiri, kila mmoja anaitamani, tuwe waangalifu na niiombe wizara ya afya isiwe inakimbilia mambo ya machanjo chanjo bila yenyewe kujiridhisha.
 
Correction: Mwanasiasa
Hivi ni sifa zipi zinazomtambulisha mtu ajulikane kuwa ni "mwanasiasa"?
Tunazijua sifa zinazomfanya mtu aitwe "mkulima", "mfugaji", "mvuvi" na hata "mfanyakazi".

Mtu anaweza kuitwa 'mkulima' hata kama hana ujuzi wowote wa kulima?

Hivi yeyote anayeingia kwenye uongozi hata kama hajui siasa, bado anastahili kupewa hadhi ya kuwa "mwanasiasa"?

Mimi sioni chochote kinachomtambulisha huyu kiongozi kuwa na sifa za kuitwa "mwanasiasa".
 
Amesema kwa sauti kubwa kuwa, Kuna watanzania walikwenda nje kupata chanjo ya corona na wametuletea Corona ya ajabu ajabu! Tafsiri yake hapa Tz cocona.....
 
Hao beberu zenu wenyewe wameshachoshwa na hayo masharti ndio maana unaona hata kwenye uchaguzi mkuu wa Marwkani watu wakikuwa kitaa bila hata barakoa, alafu wewe kajamba nani utatwambia nini sisi ambao hatuna hata vifo elfu 2?
Huna unalojua, halafu unajifanya wewe mjuaji! Hopeless kabisa.
 
Mara ipo mara haipo sasa tushike lipi? Hapa naona tu apply busara za JK "za kuambiwa changanya na za kwako"View attachment 1687354
Hakuna kitu ipo chache sema ipo au hakuna na kama ipo chache ndio unatakiwa kuwa makini isiwe nyingi kusema hata hapa hawana barakoa ni kwa sababu watu wanaogopa wanataka kumfurahisha mzee.

Tunataka utuambie corona hakuna basi sio chache. Utajuaje wingi wakati watu hawapimi? hii nchi tutakuja kupigwa marufuku hata kuingia Burundi.

Anasema sisi matajiri na africa matajiri, ni kweli lakini ajiulize mbona ni sisi huwa tunakimbilia kwao? wao kuja kwetu tunawaomba njooni mtalii sisi hatutakiwa hata kutalii kuomba visa utasema umeuwa mtu.
 
Mimi siku nikiwaona wanakataa vitu vya mabeberu kama VX-V8, Mabomu ya machozi, VIFARU, AK47, PESA etc

Hapo kweli nitaanza kuamini kweli wazungu ni wabaya, na hawana nia njema na sisi
Wamuulize Mugabe alipigwa vikumbo vya mbali tu wakaanza kufungia vitumbua pesa zao. Hospital zetu zote kila kitu kinachotusaidia pale kimetoka kwa haohao tunaowatukana hata sijui tuna nini kikubwa cha kutuvimbisha?

Hii nchi wakitaka turudi kwenye sukari guru kazi ndogo kwa hao mabeberu. wakisema tu hii nchi ban basi ujuwe ndio safari hiyo no return. Na kama ukiona sindano made in Tz basi ujuwe mtambo wa nje. Hatuna kitu chochote cha kutuvimbisha.
 
Kwahiyo kumbe tuna corona tena ya ajabu ajabu huyu baba hajui kabisa kuongopa,kipindi kile alisema mapapai yana korona naona sasa hivi atasema papuchi za wachga zina korona
🤣 Wacha nicheke tu.
Hii issue inaumiza sana kichwa
 
Back
Top Bottom