Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Ushawahi jiuliza kuwa tumuombee wa nani
 
Serikali iwasaidie lakini si vizuri kuwapa ahadi hewa hasa kujenga nyumba zao. Labda serikali iwaondolee kodi kwenye vifaa vya ujenzi hasa cement, bati na nondo
Nyie watu mna vituko sana !sasa ikiondolewa kodi ndio wale masikini ya mungu watajenga?wewe mtu kwa kujipangia tu kujenga unaanza unanyoa punk unakuja kumaliza nyumba una kipara cha uzee na mvi hadi kwenye nyusi!
Serikali isikwepe iwasaidie au watu kwa asilimia tele tu,sio kusubiri washindwe maana hatujui watatumia kipimo gani kuhakiki kama mwananchi huyu kashindwa!
 
Michango inapelekwa lkn haimaniishi wananchi wakae wabweteke kusubiri michango huo utakuwa ni upuuzi wa hali ya juu. Sio kosa ktk kauli ya rais
 
hii ni kweli ajali haikusababishwa na serikali ya CCM,je
ile balaa iliyo sababishwa kwa wakazi wa Mbagala na Gongo la Mboto walilipwa nini?Mbona wanaendelea na maisha....na hata wengine wamekwishisha sahau..
Hapa umenena mkuu kile kipindi serikali walirudishia miundo mbinu na kupiga X na kuzipa namba nyumba tu hakuna iliyojengwa licha ya kupewa ahadi, sasa serikali ya sasa haina ahadi za uwongo ,inachojua ni kukupa ukweli uliopo
 
Huko sumbawanga kuna kaya 24 nyumba zao paa zimechukuliwa na upepo. nao tena wanasubiri serikali ikawajengee mbona kazi ipo
Serikali itafilisika na itashindwa kuhudumia jamii maana kazi yake itakuwa ni kujengea waathirika wa maafa nyumba.
 
Kuwaambia wahanga wa tetemeko wafanye kazi na wasisubirie serikali hali ya kuwa wanatazama kwenye TV mapesa yao yanavyokusanywa ni kuwakosea kwa namna moja ama nyingine ,Ingawa kauli ilitawaliwa na upole ila naona kuna tatizo hapo huenda pesa hizi za wahanga hawa ZIKAELEKEZWA KATIKA JAMBO LINGINE hasa ukizingatia kauli kuwa tetemeko halikuletwa na serikali.
Inashangaza kuona mkuu huyu wa kaya anaonesha dhairi kuwa amegeuza tetemeko la Ardhi kagera kuwa source of Income katika taifa letu.
Sisi kma watanzania tunapaswa kujiuliza yale mapato yanayovuka malengo huwa yanakwenda wapi?
Iko wapi bajeti ya maafa na majanga kwa ujumla wake ili iweze kutumika katika wakati huu muafaka?
Kwanini serikali imeweza kutenga bajeti yake ya kuhamia dodoma kwa kipindi kifupi mno hali ya kuwa bajeti ya kuelekea huko haikuwepo wala kujadiliwa bungeni ?
Yapo mambo yanahitaji mwitikio wa haraka mno mfano hili la tetemeko kagera lakini serikali imetupa jukumu hilo kwa asasi za kiraia na mashirika mbalimbali ya kimataifa,hili swala halikuhitaji kujipanga zaidi ya siku tatu kwa wahanga hao.
Angalia misaada iliyotoka kwa watu wa sekta binafsi na wafanya biashara mbalimbali,hili linatosha kuonesha swala hilo halikuhitaji kujipanga kama serikali ya mkuu wa kaya inavyodai kutaka kufanya hivyo,sasa wafanyabiashara na asasi za kiraia zilizochangia zinajiuliza kama walichangia mbona watu wanasema misaada yetu haikuwafikia? Ndio maana leo ITV habari mbili za tetemeko kagera zinaonesha wanyonge wakilalamika kutofikiwa na misaada hiyo.
Tanzania sio nchi tajiri ni nchi masikini inayotaka kujikwamua.
Tanzania nchi yangu nitaipenda na kuitahamini kwa moyo wangu wote.
Magufuli rais wangu nitakusifia itakapobidi kwa furaha na shangwe.
 
Mbona hakuna baya aliloliongea hapo.....inawezekana kuna watu mna comment kabla hamkusikiliza hiyo clip.
 
Reactions: nao
Nakumbuka ule wa wimbo wa Abdul MIsambano na TOT 'masimango'
 
Ni bora anyamaze maana akiongea lzma alete mtafaruku
 
ni kushukuru kawambia kuhusu tetemeko kutoletwa na selikari. kama mbeza watu walidiriki kuishukuru serikal kwa kupeleka kupatwa kwa jua. hao kagera wangeshindwa kuilaani serikali kupeka tetemeko huko?
 
Mkuu waathirika wa ukimwi wanapewa dawa na serikali za kupunguza makali ya mashambulizi ya vinyemelezi sembuse Zilzala!!!
Hata kama huna akili lakini hapa umepitiliza.
 

OMUHAYA AKAGAMBA ATI: BAHAYA TWEMANYE!
 
Anapowaambia wajenge UKUTA nadhani anawatega tu ili wakamatwe na Polisiccm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…