Uchaguzi 2020 Rais Magufuli "theoretically" ameutangazia Ulimwengu kuwa tutakuwa na chaguzi zilzo huru, lakini "practically" hatutakuwa na uchaguzi ulio huru!

Kwa tume hii hats angesema hayo yesu mwenyewe original hakuna chochote kingefanyika.Jana yeye anawapangia washindani wake nini cha kufanya kwenye kampeni wakati naye Ni mgombea pia. Itapatikana haki hapo?
Ndio kusema unajifanya kuwa hujui kuwa JPM bado ni Amiri jeshi mkuu? Kwa hiyo lazima ahakikishe hakuna mtu anahatarisha usalama kwa namna yoyote?
 
we ukumsikia? kwamba kutakua na uchaguzi ulio huru kama chaguzi zilizopita...sasa unataka nini?
 
Serikali ya makaburu Africa kusini haikuruhusu mtu mweusi kupiga kura au kugombea nafasi ya utawala.Serikali ya Tanzania hairuhusu wapinzani haki ya kuandamana,kuitisha mkutano wa kisiasa mpaka wapende,hakuna tume huru ya uchaguzi.
Tofauti iliopo kati ya serikali hizo mbili ni kwamba Kaburu alikuwa muwazi na Tanzania ni mwongo lakini lengo ni mmoja tu kuweka kundi fulani nje ya utawala maisha.
 
Hakuna hakuna Uchaguzi huru Tanzania kama Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulivyokuwa na wakasema ni Huru basi na huu utakuwa kama ule.
 
Hakuna hakuna Uchaguzi huru Tanzania kama Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulivyokuwa na wakasema ni Huru basi na huu utakuwa kama ule.
Hao CCM ni wameshazoea wizi wa kura......

Ni sawasawa na mtu anayelula nyama ya mtu, hawezi kuacha.........
 
Anataka tu misaada ila watoa misaada wanajua kauli zake ,watatoa misaada baada ya uchaguzi, pili anataka ikifika september na October wanafunzi watakuwa wamefunga shule aanze kusema kuna corona na waangalizi wasije nchini ...mbinu zao za zamani sana.
 
kolola kama una mume muombe akuoe morning glory, huna hoja unabaki kusema tu upupu, tunataka tume huru, over
Hakuna cha Tume huru hapa, Pambana na hali yenu. Suala la kuwa na mume wakati mie ni mume unanitafuta
 
 
Kazi tunayo na safari bado ni ndefu kurekebisha elimu na elimu ya uraia hapa nchini ni msiba ambao serikali imeamua kuutelekeza.
 
Vonix said:
Kazi tunayo na safari bado ni ndefu kurekebisha elimu na elimu ya uraia hapa nchini ni msiba ambao serikali imeamua kuutelekeza.
Huyo jamaa hajui kwamba kushiriki kwenye uchaguzi, ndiyo kuna uhisiano wa moja kwa moja, maishani mwake
 
Hivyo kushinikiza uchaguzi huru ni kutukana, kubeza na kumkosea adabu mtu au kiongozi? Na hapo ndo hitaji lako litatimizwa? Be serious.
 

Well said comrade...nazi koroma nyingi bunge la 11 tunaitaji wawakilishi wenye fikra mapinduzi katika sera mbali mbali na si ndio au kukomeshana adhabu kila napoangalia bunge nikikuta kuna mswada wa sheria umepelekwa kwa hati ya dharura jua kuna funika kombe mwanaharamu apite...maazimio yana chukua siku nzima bila kupangiana mda ila hoja zinazowahusu walalahoi ni dakika 5 tuu maudhurio hafifuu ...wananchi huu ndio wakati wakuwanyoosha hawa mabwanyenyeeee ata akiiba kura basi chamoto awe amekiona
 
...Ukitaka kujua the highest order of hypocrisy ni kwa wanasiasa wetu wapinzani na chama tawala walipo ambiwa t-shirt zao zimeingia tangia saa nane usiku na zinendelea kuingia uliona makofi na meno yalivyowatoka njee...issue ni kuna walalahoi wana madai yao huko huko ila adi leo wanapigwa dana dana ...never send a monkey to do baboons job
 
Kalamu1
Wewe unasema watanzania tunalialia, basi pendekeza wewe nini kifanyike, ili pasiwepo uchaguzi wa maigizo?
Mkuu, Mystery, naona huwa hunisomi kwa makini. Mbona kila mara napendekeza, na hata kwenye mada yako hii pia nimependekeza?

Nimesema, badala ya kila mara kulalamika, kwa nini tusianze angalau kutafuta njia za kuzuia hayo tunayolalamikia? Hilo ni pendekezo au sio?

Nimeandika, tutafute njia za kuwa na ushahidi unaojitosheleza kuhusu hayo yanayofanywa; hilo sio pendekezo?

Kila mara huko nyuma humu humu JF nimekuwa nikihimiza kungali mapema kabisa, wapinzani na taasisi husika waweke wazi kwamba bila tume huru uchaguzi haufanyiki; yaani utazuiwa na nguvu zote za wananchi walioelimishwa na kuelewa kwamba kura zao zina thamani na haziwezi kuchezewa na yeyote; hii sio kulialia, ni kuchukua hatua. Lakini hakuna aliyesikiliza haya.

Tatizo ni kwamba viongozi wa vyama vya siasa wanataka kazi nyepesi nyepesi, kama hii ya kulalama; kazi ngumu ya kufanya kazi na wananchi hawaiwezi. Hili ndilo tatizo lililopo, na Magufuli anaipenda sana hali hiyo.
 
Huyo unayempapatikia hapa lugha yake huijui? Bure kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…