Rais Magufuli: Wanaoikosoa serikali kwa staha hatuwachukii

Rais Magufuli: Wanaoikosoa serikali kwa staha hatuwachukii

Kukosoa Serikali bila staha kwa maana nyingine ni kudharau mamlaka iliyoko madarakani. Katiba yetu inaruhusu hilo?
Staha ni subjective na inaweza kuwa perceived tofauti na watu tofauti

Kwa mfano, ukimwambia Magufuli “Mzee, unawakosea sana wasaidizi wako kukohoa mbele yao wakati hujavaa barakoa”

Kuna watu wataona umemkosoa Mheshimiwa bila staha wakati mwingine ataona kama umefikisha ujumbe stahiki kwa maslahi ya watu
 
Mimi naamini kila binadamu ana uwezo wa kubadilika labda mwenyewe awe hataki.

Nadhani Rais Magufuli, tangu aingie madarakani, anatambua kuwa kuna maeneo hakufanya vizuri. Japo hawezi kusema moja kwa moja, sisi raia tunaweza kutambua kutokana na kauli na matendo yake ya sasa ukifananisha na ya hapo awali.

Kwa mfano, kama kauli hii ameitoa toka moyoni na kwa dhamira njema, ni jambo lenye manufaa kwa Taifa. Taifa hili, safari yake ya kufikia maendeleo ya kweli itakuwa rahisi zaidi kama tukitambua kuwa tupo watu wengi, wenye mawazo mengi yanayotofautiana, ujuzi wa aina mbalimbali, tabia za aina mbalimbali na mitazamo mingi inayotofautiana. Tukizikubali tofauti hizi, basi hugeuka kama maua au mapambo kwenye vazi lako, na utaona ni baraka. Lakini ukizikataa, utayaona kama ni madoa na uchafu katika vazi lako.

Rais kama ameyanena hayo, kama namna ya kubadilisha mtazamo, nadhani kila mwenye hekima hawezi kukosoa kwa kutukana. Lakini hiki linatakiwa liende mpaka chini. Kuna wasaidizi wake wengine wana lugha chafu na za kejeli. Yaani mtu akitofautiana tu mtazamo au akakosoa, basi huyo ni kibaraka anayetumiwa na mabeberu au hana uzalendo. Kwa mtu ambaye una uhakika huna mawasiliano yoyote na beberu na wala hujawahi kutumiwa na mtu wala chombo chochote, na unajua Tanzania ndiyo nchi yako pekee, mtu akikutolea kauli chafu kama hizo, sidhani kama naye atakujibu kwa staha maana wewe umepanda uchafu, aghalabu utavuna uchafu.

Rais tunakuomba uheshima fikra za wengine, utumie lughabya staha dhidi ya wengine, himiza hivyo hivyo kwa wasaidizi wako, nina hakika nawe na Serikali yako mtakosolewa kwa staha.

Japo ukweli ni kuwa uchaguzi wa 2020 ulikuwa ni aibu kubwa kwa Taifa letu, na Ulimwengu wa demokrasia.
 
Mimi naamini kila binadamu ana uwezo wa kubadilika labda mwenyewe awe hataki.

Nadhani Rais Magufuli, tangu aingie madarakani, anatambua kuwa kuna maeneo hakufanya vizuri. Japo hawezi kusema moja kwa moja, sisi raia tunaweza kutambua kutokana na kauli na matendo yake ya sasa ukifananisha na ya hapo awali.

Kwa mfano, kama kauli hii ameitoa toka moyoni na kwa dhamira njema, ni jambo lenye manufaa kwa Taifa. Taifa hili, safari yake ya kufikia maendeleo ya kweli itakuwa rahisi zaidi kama tukitambua kuwa tupo watu wengi, wenye mawazo mengi yanayotofautiana, ujuzi wa aina mbalimbali, tabia za aina mbalimbali na mitazamo mingi inayotofautiana. Tukizikubali tofauti hizi, basi hugeuka kama maua au mapambo kwenye vazi lako, na utaona ni baraka. Lakini ukizikataa, utayaona kama ni madoa na uchafu katika vazi lako.

Rais kama ameyanena hayo, kama namna ya kubadilisha mtazamo, nadhani kila mwenye hekima hawezi kukosoa kwa kutukana. Lakini hiki linatakiwa liende mpaka chini. Kuna wasaidizi wake wengine wana lugha chafu na za kejeli. Yaani mtu akitofautiana tu mtazamo au akakosoa, basi huyo ni kibaraka anayetumiwa na mabeberu au hana uzalendo. Kwa mtu ambaye una uhakika huna mawasiliano yoyote na beberu na wala hujawahi kutumiwa na mtu wala chombo chochote, na unajua Tanzania ndiyo nchi yako pekee, mtu akikutolea kauli chafu kama hizo, sidhani kama naye atakujibu kwa staha maana wewe umepanda uchafu, aghalabu utavuna uchafu.

Rais tunakuomba uheshima fikra za wengine, utumie lughabya staha dhidi ya wengine, himiza hivyo hivyo kwa wasaidizi wako, nina hakika nawe na Serikali yako mtakosolewa kwa staha.

Japo ukweli ni kuwa uchaguzi wa 2020 ulikuwa ni aibu kubwa kwa Taifa letu, na Ulimwengu wa demokrasia.
Kwa nini mnamuita meko? Dikteta uchwara?
 
Rais wa JMT ameyasema hayo wakati akizungza na watanzania kupitia hadhara iliyokusanyika jana viwanja vya mnazimmoja.

Rais Magufuli amesisitiza kuwa kwa sasa hapa Tanzania kuna vyombo vingi vya habari ambavyo vimepewa leseni za kufanyia kazi na hii ni ishara kuwa kuna uhuru mkubwa wa habari hapa Tanzania.

Lakini jambo la kusikitisha ni kuona kuna upotoshaji mkubwa unaofaywa na baadhi ya vyombo vya habari. Mfano ni kuandika habari za uzushi juu ya vifo vya viongozi na kupotosha kuwa sasa kuna maambukizi makubwa ya Corona tofauti na hali halisi.

Hivyo ni wazi kuwa kama serikali inakubali kukosolewa ni jambo jema kutumia lugha nzuri kufikikisha ujumbe kwa viongozi wa serikali ili wajirekebishe.
Magufuli is a damn blasted liar
 
Rais wa JMT ameyasema hayo wakati akizungza na watanzania kupitia hadhara iliyokusanyika jana viwanja vya mnazimmoja.

Rais Magufuli amesisitiza kuwa kwa sasa hapa Tanzania kuna vyombo vingi vya habari ambavyo vimepewa leseni za kufanyia kazi na hii ni ishara kuwa kuna uhuru mkubwa wa habari hapa Tanzania.

Lakini jambo la kusikitisha ni kuona kuna upotoshaji mkubwa unaofaywa na baadhi ya vyombo vya habari. Mfano ni kuandika habari za uzushi juu ya vifo vya viongozi na kupotosha kuwa sasa kuna maambukizi makubwa ya Corona tofauti na hali halisi.

Hivyo ni wazi kuwa kama serikali inakubali kukosolewa ni jambo jema kutumia lugha nzuri kufikikisha ujumbe kwa viongozi wa serikali ili wajirekebishe.
Kuna magazeti yanaendeshwa na serikali Kama Hari leo, tanzanite, Uhuru, mzalendo, na hoja huwa yanawakosoa na kuwaandika kwa staha chadema???
 
Je, Katiba yetu tuliyonayo inaruhusu kutokuheshimu mamlaka iliyoko madarakani au kutokuwaheshimu wengine? Kukosoa Serikali bila staha kwa maana nyingine ni kudharau mamlaka iliyoko madarakani. Katiba yetu inaruhusu hilo?
Ni swali zuri, lakini katiba hiyo hiyo pamoja na mambo mengine inataka uhuru wa vyama vya siasa kufanya shughuli za siasa bila kuingiliwa, je hayo yanazingatiwa?
 
Tunatakiwa tunapokosoa tutumie lugha ya kusifu
 
Safi sana Mirembe
Safi sana NIMRI.
Yaani nimri taasisi iliyojaa madaktari bingwa wameishia kuchukua ndimu, pilipili, ukwaju, mbilimbi na tangawizi kutengeneza dawa ya corona. NIMRI wanakesha mitandaoni kuangalia vitu wanavyotumia watu kujitibu mafua then wao wanatangaza wamegundua dawa ya COVID. Aibu.
 
-Yako wapi hayo matusi?
-Amejuwaje kuwa wanaokufa hawafi kwa korona wakati vipimo vya Corona havifanyiki?
-wingi wa vyombo vya habari unahusianaje na uhuru wa vyombo hivyo?
- meko
-dikteta uchwara
-aliyekuambia wanakufa kwa korona nani?
- kutoa leseni ni uthibisho tosha
 
Hayo maneno kwenye KATIBA hakuna!!
kwenye katiba yapo tatizo hata katiba hamijui

Katiba inatamka wazi kuwa kila mtu anastahili heshima na kutovunjiwa utu wake sasa ukiongea na mtu maneno yasiyo na heshima unakuwa umevunja katiba na kumvunjia hshima utu wake

ina maana hata ukichora katuni ya kumdhalilisha umevunja katiba ya nchi
 
- meko
-dikteta uchwara
-aliyekuambia wanakufa kwa korona nani?
- kutoa leseni ni uthibisho tosha
  • ni tabia zake.
  • ni tabia zake.
-Aliyekwambia hawafi kwa Corona ninani?
-Wingi wavyo si uthibitisho wa uhuru wavyo.
 
Mwana kulitafuta mwana kuli get.

Yani kwenye mkutano Wa hadhara uwagombeze wakurugenzi kuwa nawalipa mshahara na Gari afu utangaze mpinzani mshindi.

Chuki ya wananchi naserikali ilianzia hapo,maana wanalipwa kwa kodi zao.
Hela haitoki mfukoni kwa mwenyekiti.
Tujiulize Tanzania tuna vyombo vya Habari credible vyenye uwezo wa kukosoa serikali yake ikanyamaza, magazeti kama Mawio, MwanaHalisi, Tanzania Daima yalifungiwa na serikali, sasa hivi serikali inapata upinzania mkali sana kupitia social media ndiyo maana wamejitokeza mawaziri watatu Nchemba, Bashugwa na Ndungulile wote wanatoa matamko juu ya mitandao. Serikali ijuulize kwa nini wanapata upinzania huko, imekosea wapi? ndiyo itakuwa suluhisho.
 
Kwa nini mnamuita meko? Dikteta uchwara?
Unasema kwa nini huwa tunamwita Dikteta uchwara au Meko - sijui unamaanisha ni nani hao ambao huwa wanamwita hivyo.

Sidhani kama kuna kundi lolote kwa misingi ya aina yoyote, waliwahi kukaa na kukubaliana kuwa Rais Magufuli aitwe Meko au dikteta uchwara. Ndiyo maana hata ukiwatafuta wapinzani au wanaomkosoa Rais Magufuli, wengi sana hawajawahi kumwita kwa majina hayo.

Lakini pia hakujawahi kuwa ns mkutano wa kukubaliana kuwa wanaCCM waitwe mataga au wanaCHADEMA waitwe nyumbu. Lakini pia katika ushindani, jokes na vitimbwi, hunogesha mijadala na upinzani.

Ukiwa kiongozi, huwezi kukwepa majina bandia, mengine ni ya kukukejeli lakini yapo pia kwa nia ya kukusifu.

Mwalimu Nyerere alikuwa akiitwa Mchongameno na majina mengine, lakini la Mchongameno lilifahamika kwa watu wengi. Mwalimu hakuwahi kukataa wala kukubali, na wengine walidhani hajui. Lakini baadaye wapo walianza kumwita Musa, hapo ndipo Mwalimu alipokemea. Kwa maneno yake alisema, 'mmeniita majina mengi, nimekubali. Mnaweza kuendelea kuniita kwa hayo majina, mara mchongameno, na mengine. Lakini hili la kuitwa MUSA, nalikataa'. Mwalimu alijiona hamkaribii kwa namna yoyote ile nabii Musa, aliyewaongoza wana wa Israel kutoka Misri kuelekea nchi ya ahadi.

Mzee Mwinyi alikuwa akiitwa Mzee Ruksa. Wapo waliomwita hivyo kama namna ya kumsifu alileta demokrasia, lakini wapo waliomwita hivyo kumkejeli kama mtu aliyeruhusu mambo yote yafanyike holela. Lakini Mwinyi, siku moja alipohojiwa kuwa anajisikiaje anapoitwa Mzee Ruksa? Alijibu nafarijika sana. "Maana unapita sehemu unaitwa Mzee Ruksa, Mzee Ruksa. Nafarijika kwa sababu wakati ule tulisema watu wasibanwebanwe, wawe huru".

Magufuli aliwahi kutamka mwenyewe kuwa yeye ni Jiwe, wapo baada ya pale wanaomwita hivyo. Wengine kwa kutaka kuonesha ni mtu asiyeyumbishwa, lakini wapo wanaomwita hivyo, wakimaanisha mtu asiyepokea ushauri. Lakini Rais mwenyewe anapoitwa Jiwe, anajisikiaje, hakuna aliyewahi kumwuliza. Hatujui anafurahia au anachukizwa.

Lakini ukiacha hoja za hapo juu, Rais Magufuli huenda ndiye Rais atakayeongoza kwa kuitwa majina mengi bandia. Ukumbuke, mwanzoni mwa utawala wa Rais Magufuli, wapo waliomkosoa Rais Magufuli kwa kumwandika jina lake halisi yaani Rais Magufuli, baadhi ya watu hawa walikamatwa, baadhi waliokuwa na bahati walishtakiwa, wengine mateso waliyoyapitia wanayajua wao. Lakini ikumbukwe mmojawapo alishinda kesi mahakamani kwa vile alimwandika Rais Magufuli kama Magu. Alishinda kwa sababu kisheria Magu, hakuna uthibitisho kuwa ni Rais Magufuli. Hiyo iliongeza sana tabia ya watu kumwita Rais Magufuli kwa majina mbalimbali ili tu kisheria wasionekana wanayemsema ni Rais Magufuli.

Ukitaka jambo liondoke au lipungue, ni watu kuwaacha wawe huru. Anayekosea ashtakiwa kwa kosa alilolitenda na siyo kumbambikia makosa ambayo hakuyatenda. Mtu amemkashfu Rais, halafu anakamatwa, mahakamani anashtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi ili tu akae ndani asipate mdhamana. Mambo hayo yanazidisha chuki na kuongeza lugha zisizo na staha.

Tukubaki tu kuwa Rais kuna wakati, nadhani kwa ghadhabu, anatumia lugha zisizo na staha. Mfano kule Tunduma, mama anamweleza Rais kero ya maji, yeye akamjibu, aende akamwombe mume wake! Jibu kama hilo halijengi mazingira ya chuki na lugha zisizo na staha? Lakini huenda Rais naye, alikuwa tayari ameaudhiwa na mambo mengine, ndiyo maana ile hekima ya uvumilivu ilimwondoka.

Mimi nimewahi kushuhudia, watu wanamwuliza mkuu wa wilaya maswali, mkuu wa Wilaya badala ya kujibu, anaanza kuwatukana waliouliza maswali na kuwaita wapumbavu na kuamuru wawekwe ndani. Kiongozi wa namna hii, nani atamheshimu? Nani atatumia kugha ya heshuma dhidi yake?

Kama tunataka kuanza upya, kila mmoja kuna mahali na namna ya kujirekebisha. Viongozi wawe wa kwanza kuonesha njia kwa kujirekebisha, raia watafuata. Na wale wabishi, watashtakiwa kwa haki kwa mujibu wa sheria kwa makosa yao hakisi waliyoyatenda, na siyo ya kuwatengenezea.

Kuna wakati niliwahi kutamka kuwa, binafsi, kidhamira naweza kupuuza mengi ambayo nahisi viongozi wamekosea (maana nia wao ni binadamu, lazima kuna makosa watafabya), lakini siwezi kuouuza wala kusamehe mambo ya kuteka watu, kuwapoteza, kuwaua, kuwatesa au kuwabambikia kesi. Huo ni unyama na ushetani ambao haustahili kuwepo kabisa katila jamii ya watu waliostaarabika, tena ambao zaidi ya 80% ni watu wanaomjua Mungu kuoitia imani mbalimbali. Nashukuru sana, na ninafarijika sana, kuwa hayo mambo kwa kiasi kikubwa mengine yamekoma, na mengine yamepungua.
 
Back
Top Bottom