Rais Magufuli: Wanaoikosoa serikali kwa staha hatuwachukii

Je, Katiba yetu tuliyonayo inaruhusu kutokuheshimu mamlaka iliyoko madarakani au kutokuwaheshimu wengine? Kukosoa Serikali bila staha kwa maana nyingine ni kudharau mamlaka iliyoko madarakani. Katiba yetu inaruhusu hilo?
Ni vigumu kuelewa Watanzania wengine akili zao wamewekeza wapi. Katiba ni waraka wa wananchi, siyo serikali. Wananchi wako juu ya Serikali, siyo kinyume chake. Serikali inawajibika kwa wananchi, siyo kinyue chake. Katiba inatoa uhuru kwa wananchi kupashana habari na kupeana taarifa, siyo kwa matakwa ya serikali. Sasa akina nyie mnataka serikali ikifanya maamuzi ya hovyo, na pengine maamuzi yanayohatarisha maisha ya wananchi (kwa mfano zigzag za COVID 19), wahanga waipigie magoti kuomba kuishauri serikali! Hopeless kabisa! Tabia hizi za maofisa wa serikali waliopo kazini na (the worst case scenario) wastaafu wa serikali, hazipaswi kuendekezwa na wananchi huru, katika taifa huru la kidemokrasia!
 
Hao mawaziri uliowataja watatu,sio rahisi wakatumia elimu Ama utaalamu wao katika awamu hii ya tano mkuu,mapambio na kusifu ndo yanawalinda kwenye hizo nafasi walizopewa,inawezekena kabisa wanajua wanakosea wapi,ila hawawezi kwenda kinyume na beat za baba mwenyenyumba.
 
Waliotumwa bungeni ambapo kuna staha hawapo sasa ustaha upi anamaanisha au anamanisha kwa unyenyekevu. Sayansi ya kijivujivu inasema jinsi utakavyo kuja ndivyo utakavyo pokelewa au nasema uwongo wajameni
 
Je, Katiba yetu tuliyonayo inaruhusu kutokuheshimu mamlaka iliyoko madarakani au kutokuwaheshimu wengine? Kukosoa Serikali bila staha kwa maana nyingine ni kudharau mamlaka iliyoko madarakani. Katiba yetu inaruhusu hilo?
Ambaye ameikosoa serikali bila staha ni nani toka january 2021
 
Ambaye ameikosoa serikali bila staha ni nani toka january 2021
Waliopo Serikalini na ambao wamekosolewa ndiyo wanaowajua wakosoaji wa aina hiyo, mimi siwajui ila nimesikia hoja zikitolewa tu na wale ambao wamekuwa wakikosolewa bila staha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…