Rais mstaafu, Jakaya Kikwete ahudhuria msiba wa Gabriel Ndugulile, Baba wa aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni

Rais mstaafu, Jakaya Kikwete ahudhuria msiba wa Gabriel Ndugulile, Baba wa aliyekuwa Mbunge wa Kigamboni

Kumbe mzee alichomoka na walinzi wake wale wale tokea akiwa madarakani?

Pole kwa mbunge na wanakigamboni kwa ujumla kwa msiba unaomhusu muwakilishi wao.

Siasa ikae pembeni kidogo mambo mengine yaendelee. Kuna watu watachukia kwanini kaenda kwenye huu msiba.
Pole kwa wafiwa,

Inavyoelekea huo ndio utaratibu wao, hata hawa wa sasa baadhi yao tu na sio wote wataondoka naye.
 
Afadhali alipata habari za ushindi wa Dr Ndungulile kwenye kura za maoni kabla mauti hayajamsibu.
 
Msibani wanashikana mikono, hawajavaa barakoa, wamekusanyika..

NB Nyumban kwa Dokta aliyetumbuliwa kwa kusimamia sayansi badala ramli za kienyeji..

Bado mnabisha Corona kasepa[emoji16]
 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Kikwete alipowasili eneo la msiba nyumbani kwa marehemu mzee Gabriel Ndugulile Ferry Kigamboni Jijini Dar es salaam kutoa pole kwa familia kwa msiba huo.

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Kikwete alipowasili eneo la msiba nyumbani kwa marehemu mzee Gabriel Ndugulile Ferry Kigamboni Jijini Dar es salaam kutoa pole kwa familia kwa msiba huo.


Ndugu Dkt. Ndugulile akitoa shukrani kwa watu wote kuhudhuria na kutoa salamu za pole na rambirambi kwa msiba uliowapata kuondokewa na Baba yao kipenzi marehemu Mzee Gabriel Ndugulile.

Pia ametoa shukrani kwa niaba ya familia kwa Mhe.Rais JP.Magufuli kuwapatia ndege moja ya serikali kasafiria kuelekea Mkoani Tabora kwa mazishi.

Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mhe.Sarah Msafiri akitoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Gabriel Ndugulile kwa niaba ya Serikali nzima ya Manispaa ya Kigamboni.

Mhe. Faustine Ndugulile Mbunge wa Jimbo la Kigamboni alifiwa na Baba Mzazi Gabriel S. Ndugulile Jumamos 18.07.2020 Asubuhi. Msiba upo Nyumbani Kwake Ferry, Kigamboni, Dar Es Salaam

' Mtia Nia ' namba Mbili Jimbo la Kigamboni kwa Tiketi ya CCM ( Yule Bwege Nazi ) alikuwepo Msibani au labda hana Habari na bado anaendeleza tu Maumivu kutoka kwa ' Kamati Ya Roho Mbaya ' ya CCM huko Kigambopni? Nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa upendo wake mkubwa kwa Familia ya Marehemu kwa kuwapa Bung'o / Ndege ya Serikali isafirishe Mwili hadi Mkoani Tabora. Ila niendelee tu Kumuomba Mwenyekiti CCM Taifa kuwa Upendo huu huu anaouonyesha sasa kwa Familia ya Wafiwa ( akina Ndugulile ) basi aendelee nayo hadi katika Siku ya Kuamua nani agombee Jimbo la Kigamboni na wala asipoteze muda wake bali aamue na aridhie tu Dokta Faustine Ndugulile agombee na siyo ' Mpuuzi ' mwingine yoyote Yule.

Kwa tuliobobea vyema katika Saikolojia hasa ile ya Kimawasiliano Kitendo tu cha Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne kwenda hapo Msibani ni Jibu tosha kuwa Dokta Faustine Ndugulile anaishi vyema na Watu, hana Makuu, anajiheshimu, Mkarimu na ni Mweledi mno. Lakini kwa Mheshimiwa Kikwete ( Rais Mstaafu ) kuwa hapo ni Ujumbe tosha kwa ' Bwege Nazi ' moja hivi kuwa hata Yeye JK hamkubali ( japo alishawahi Kumlea kupitia Uswahiba wa Kipopoma na Mwanae ) ila pia ni Meseji Kamilifu ambayo hata JK anaituma Kwake Mwenyekiti wake CCM Taifa kuwa Dokta Faustine Ndugulile anatosha na anafaa Kuendelea kuwa Mbunge wa Jimbo la Kigamboni.

Mwisho nitoe ANGALIZO langu kwake ' Mtia Nia ' Mwongozaji katika Kura za Maoni kwa CCM huko Kigamboni ( Dokta Faustine Ndugulile ) kuwa ukiweza kuanzia sasa jitahidi mno Kubadili Ratiba zako, ongeza Umakini na ukiweza ishi kwa Machale Machale sana, usiwaamini Watu wote, Mwogope huyo Dada mwenye eneo lake ' Kiutendaji ' huko unakoishi kwani Yeye na Unayemtimulia Vumbi ni ' Maswahiba ' wakubwa hadi na ule ' Uswahiba ' wa ' Kibaiolojia ' pia namaanisha ule wa Adam na Hawa wanao, hivyo kutokana na Rekodi ya ' Kimatukio ' aliyonayo ' Unayemtimulia Vumbi ' hasa ya ' Kimafia ' ukizingatia ana Pesa nyingi na Mtandao wake mkubwa wa ' Mafia ' ndani na nje kwa Tamaa yake na Azma yake huko mnaposhindana ' nae hakawii na wala hatoona shida yoyote ile ya ' Kukupiga Tukio ' akishirikiana vyema na huyo Dada. Kuwa Makini Dokta Fau.
 
Ndege ndio zinatumika hivyo au mimi sijaelewa?

Wamepewa au wameicharter?
 
Asante sana kumbe ni yule alikuwaga ticha.Thanks.
Hajawahi kuwa ticha Sara. Alikuwa investigation officer Time ya haki za binadamu then akachaguliwa mbunge viti maalumu awamu ya nne . Awamu hii akapata ukuu wa wilaya na alianzia mbulu then Kigamboni. Hajawahi kuwa ticha.
 
Back
Top Bottom