Rais mstaafu Jakaya Kikwete amesema iwapo Watanzania wangekuwa na ari ya kujituma kama wanavyofanya Wachaga, nchi ingekuwa mbali kimaendeleo

Rais mstaafu Jakaya Kikwete amesema iwapo Watanzania wangekuwa na ari ya kujituma kama wanavyofanya Wachaga, nchi ingekuwa mbali kimaendeleo

#Repost @mwananchi_official
——
Rais mstaafu Jakaya Kikwete amesema iwapo Watanzania wangekuwa na ari ya kujituma kama wanavyofanya Wachaga, nchi ingekuwa mbali kwa maendeleo.

Kikwete ametoa sifa hizo kwa Wachaga, huku akiyahusisha baadhi ya makundi ya watu nchini, ambayo hata kulima kwa ajili ya mlo wao wanalazimika kusukumwa.

Kikwete ametoa kauli hiyo jana Jumatatu, Desemba 23, 2024 alipowaongoza maelfu ya wanariadha katika mbio za Rombo Marathon zilizofanyika katika Hifadhi ya Msitu wa Rongai wilayani Rombo, Kilimanjaro.

"Kuna maeneo hapa nchini watu hata kujilimia chakula chao inabidi usukumane nao, lakini hakuna Mchaga utakayemsukuma kwa kujiletea maendeleo, na hiyo ndio siri, uzuri Wachaga hawasahau kwao kila mwaka wanakwenda kuhesabiwa," amesema.

Kwa mujibu wa Kikwete, mtindo wa kwenda nyumbani kila mwisho wa mwaka unajenga ushawishi kwa wengine kuonyesha hatua za maendeleo walizopiga.

"Niwapongeze wananchi wa Rombo kwa moyo wenu wa kujituma na kujiletea maendeleo, mimi nimefanya kazi wilayani, mkoani, wizarani na katika ngazi ya juu kabisa ya uongozi wa nchi yetu, Watanzania wote wangekuwa na ari ya wachaga nchi yetu ingepiga hatua kubwa, endeleeni na moyo huo," amesema.

(Imeandikwa na Janeth Joseph)
#mwananchiupdates
#tunaliwezeshataifa
Yuko sahihi kabisa
 
Wivu 🙄 really?
Ukweli mchungu, kuna siku niliwaza kwanini familia nyingine zipo benki kuu, bandarini, mahakamani, taasisi kubwa kubwa

Wazee wao waliotangulia waliweka nafasi kwa watu wa chini yao, sio kwa wepesi kuna gharama zake pia, maisha ya watu, kutapeli, kuumizwa, kufosi

Sasa tujiulize wazee wetu walikuwa wapi miaka hiyo...?
 
JK kwenye hili ninamwelewa,Mimi Mdigo.Yaaani ukitoa Wachaga makabila mengine yanamambo ya ajabu sana ambayo yanazima maendeleo.Mfano unyagoo et unapewaa kipaombele na jamii kuliko kujenga nyumba zaoo,kuoa hovyooo hovyooo,kuchunga ming'ombe 100 halafu nyumba ya nyasi.

NB: Kikawaida popote penye minazi hapaswi kutoka Rais wa nchi.Viva JK watu wanashambulia familia yake wakati yeye ametoa mtazamo wake ambao Hauna biasness,Mimi sio mchaka ila Jamaa wanajitambuaa sana.

Hutakuta kwa mchaga amekusanya ndugu ambaoo Hawana kazii wanamtegemea,mabinamuu mashemeji,.....
 
Kama mikoa ya Manyara, Arusha Kilimanjaro na Tanga kaskazin yangekuwa nchi inayojitegemea, ndio ingekuwa first world country kusini mwa jangwa la Sahara. Kuna wavivu wanakwamisha maendeleo kiu yao ni kuiba na kula jasho la wengine na bado ni masikini. Bravo JK kwa kuwa muwazi.
Huo uwazi angeenda nao mbali zaidi kwa kuwataja hao wavivu wa kutafuta kwa majina ya makabila na maeneo Kama alivyofanya kwa kuwataja wachagga.

Tunasubiri…. Na awe mkweli tupu beyond any reasonable doubt.
 
Amesahau Wasukuma,Wakinga, Waha na makabila mengine ila anakotokea (Kikwete) ukanda wa pwani Mungu aliwanyima maarifa ya kupambania maisha kutwa kucha kijiweni kuteta umbeya sio rahisi kumtofautisha mwanaume na mwanamke wa pwani kwa umbeya wote wapo frontline.
 
Ukweli mchungu, kuna siku niliwaza kwanini familia nyingine zipo benki kuu, bandarini, mahakamani, taasisi kubwa kubwa

Wazee wao waliotangulia waliweka nafasi kwa watu wa chini yao, sio kwa wepesi kuna gharama zake pia, maisha ya watu, kutapeli, kuumizwa, kufosi

Sasa tujiulize wazee wetu walikuwa wapi miaka hiyo...?
Kwahiyo njia zingine za halali wanazotumia watu kujitafutia chochote chao ni upuuzi?!

Material things for a plastic generation!!

Kwamba kumiliki vitu imekua ni muhimu zaidi ya utu to the extent that it doesn’t really matter how you acquire them?!

Kweli kudos kwa waChagga.
 
Material things for a plastic generation!!

Kwamba kumiliki vitu imekua ni muhimu zaidi ya utu to the extent that it doesn’t really matter how you acquire them?!
Ndio ni muhimu, utu haukupi ugali mezani, utu haulipi ada tuache siasa za kiimani, kuna watoto wamesomeshwa kwa hela za wizi ni madaktari wazuri na wanatutibu tunapona
 
#Repost @mwananchi_official
——
Rais mstaafu Jakaya Kikwete amesema iwapo Watanzania wangekuwa na ari ya kujituma kama wanavyofanya Wachaga, nchi ingekuwa mbali kwa maendeleo.

Kikwete ametoa sifa hizo kwa Wachaga, huku akiyahusisha baadhi ya makundi ya watu nchini, ambayo hata kulima kwa ajili ya mlo wao wanalazimika kusukumwa.

Kikwete ametoa kauli hiyo jana Jumatatu, Desemba 23, 2024 alipowaongoza maelfu ya wanariadha katika mbio za Rombo Marathon zilizofanyika katika Hifadhi ya Msitu wa Rongai wilayani Rombo, Kilimanjaro.

"Kuna maeneo hapa nchini watu hata kujilimia chakula chao inabidi usukumane nao, lakini hakuna Mchaga utakayemsukuma kwa kujiletea maendeleo, na hiyo ndio siri, uzuri Wachaga hawasahau kwao kila mwaka wanakwenda kuhesabiwa," amesema.

Kwa mujibu wa Kikwete, mtindo wa kwenda nyumbani kila mwisho wa mwaka unajenga ushawishi kwa wengine kuonyesha hatua za maendeleo walizopiga.

"Niwapongeze wananchi wa Rombo kwa moyo wenu wa kujituma na kujiletea maendeleo, mimi nimefanya kazi wilayani, mkoani, wizarani na katika ngazi ya juu kabisa ya uongozi wa nchi yetu, Watanzania wote wangekuwa na ari ya wachaga nchi yetu ingepiga hatua kubwa, endeleeni na moyo huo," amesema.

(Imeandikwa na Janeth Joseph)
#mwananchiupdates
#tunaliwezeshataifa
Kujituma kivipi sasa,mbona watu wengi wanajituma sana au kujituma kwa kila mwisho wa mwaka kwenda makwao,tumeshawahi kujiuliza kwanini wanatumia nguvu nyingi sana kuhakikisha kuwa mwisho wa mwaka lazima warudi kwao.....
 
Huo uwazi angeenda nao mbali zaidi kwa kuwataja hao wavivu wa kutafuta kwa majina ya makabila na maeneo Kama alivyofanya kwa kuwataja wachagga.

Tunasubiri…. Na awe mkweli tupu beyond any reasonable doubt.
Mimi bila kupepesa macho naanza na Wazaramo, Wandengereko, Wamatumbi,Wangindo.. kidogo kabila lake (Wakwere) wana unafuu kuliko hao niliowataja.
 
Mabilionea Tanzania
1.Mo Dewji
2.Rostam Aziz
3.Bakhresa
4. Ghalib-GSM
Hao wote ni Asian Tanzanian.. wengi wa hawa matajiri wamerithi utajiri toka mababu zao wakati wa ukoloni , walipewa haki ya kununua mazao kutoka kwa makabwela waafrika, mkoloni alitenga madaraja ya raia kama ifuatavyo...Fist class (Europian) Second Class (Asian) na Third Class walikuwa Waafrika..Asian wamefika hapo kwa kupendelewa fursa na mkoloni.
 
Back
Top Bottom