Rais Mwinyi kuongezewa muda: Dr Mdimwa nani alikutuma? Au ni kiherehere chako tu!

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594


Huyu Dr Mdimwa hajulikani siasa za nchi hii.
Kwzmba ni naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar, bado ni mwanasiasa mchanga sana nchi hii.
Tamko alilotoa kutaka Rais wa Zanzibar Dr Mwinyi aongezewe muda wa utawala toka miaka mitano hadi saba, inaonekana kama tamko la mtu asiyeelewa siasa na mipaka ya kuongea mbele za umma wa Kitanzania.

Huyu Dr Mdimwa kakosea big time.
Kakanushwa na Rais Mwinyi mwenyewe, CCM yenyewe, na hata wakongwe kama mzee Msekwa.

Mzee Msekwa kaenda mbsli na kusema Katiba haichezewi chezewi vile mtu apendavyo.

Yakhe, Dr Mdimwa NANI ALIKUTUMA?
Au ni kiherehere chako tu!
 
Kuna watu wa ovyo wengi kwenye uongozi nchini kwa sasa. Yaani mtu akikupa ulaji unakua chawa na kupoteza akili yako hata kama una elimu kubwa kiasi gani. Yaani unapoteza ule uwezo wakuchambua lipi sawa lipi sio sawa. Kwako unaona njia ile inaleta msosi tumbomi kwako tu ndio sahihi hujali maslahi ya taifa hata tone. Kwa viongozi wa aina hiyo ndio maana mnaona Speaker mwenye Phd ya sheria anakua mstari wa mbele kupitisha bungeni mkataba kama ule ulikua unawapa dubai bandari zetu zote wamiliki kama mali yao. Kigogo mmoja mzalendo aliita kwa usahihi mkataba huo kama haufai hata kulumangia ugali. Mungu ambariki kigogo huyo.
 
Huyo atakuwa shoga anatafuta basha
 
Mi ccm Ina akili za, kichawi, huyo hajasema kwa bahati mbaya,ametumwa atikise kiberiti kwanza, sie kwetu tunaita, "shake the tree and see what falls"
Wanapima, upepo, waone, muitikio wa, mazombi ya zenj,
 
Mi ccm Ina akili za, kichawi, huyo hajasema kwa bahati mbaya,ametumwa atikise kiberiti kwanza, sie kwetu tunaita, "shake the tree and see what falls"
Wanapima, upepo, waone, muitikio wa, mazombi ya zenj,
Swali ni katumwa na nani?
 
Labda alitumwa kupima maji ya moto au la kama Ndugai na Jiwe
 
Labda alitumwa kupima maji ya moto au la kama Ndugai na Jiwe
Kweli siyo bure, mtu katoka kula tende zake mara anataka Rais wa miaka saba.
Anajamba na kuhara kisiasa.
Ameiaibisha CCM.
 
Nenda YouTube kwenye channel ya Asbert Ngurumo nadhani inaitwa SK media, kaelezea vizuri sana ni nini kiko nyuma ya hili.
 

..kuna mwingine ni Naibu Katibu Mwenezi wa Ccm amesema Tume Huru ya Uchaguzi itaanza kazi baada ya 2025.

..Makamishna walioteuliwa ktk Tume ya zamani hawatabadilishwa pamoja na kwamba sheria ya kuanzisha Tume Huru imeshapitishwa.

..pia Uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu utasimamiwa na Tamisemi, kwa maana Ofisi ya Rais ambaye ni Mwenyekiti wa Ccm.

..sasa unajiuliza kulikuwa na ulazima gani kusumbua wananchi kutoa maoni kuhusu Tume Huru ya uchaguzi?

..Je, waliotoa maoni lengo lao lilikuwa Tume Huru iwe hivi ilivyopitishwa na ianze kazi baada ya uchaguzi wa 2025?
 
Kuna watu wanawashwa washwa kutaka kubaka demokrasia.
 
NADHANI HII SIYO HUZUNI TU BALI NI MSIBA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…