Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
Nina laani kwa nguvu zote kitendo cha vurugu za mgambo na watu wa jamii ya kimasai kwakupigana hadharani, Nina laani Masai kushambulia Mgambo, Nina laani kwa nguvu kubwa Mgambo wa Zanzibar kushanbulia watu wa jamii ya kimasai! Jambo hili halikubaliki kwa mjibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazokataza kupigana hadharani au kificho.

Lakini naomba nitofautiane na hatua iliyochukuliwa na serikali ya Zanzibar, Amri kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime/visu vyao, Ni Kauli Haramu na ya kibaguzi inayohatarisha muungano wa Tangabyika na Zanzibar.

Ifahamike kuwa Fimbo na Sime kwa Jamii za kimasai ni sehemu ya “vazi lao la asili”, ni Sehemu ya utamaduni wao, Ni Identity yao, na hivyo kujaribu kwa aina yoyote kuondoa kimoja wapo katika hivyo vinavyokuwa ndani ya mwili wa Masai ni kutangaza kuwafukuza Wamasi Zanzibar, Hili ni tangazo la kijinga limekurupukwa na mamlaka za Zanzibar!

Kwamiaka yote tangu kabla ya uhuru hadi leo, Jamii za Wamasai wapo Zanzibar na utamaduni wao wa visu/Sime na Fimbo, hakujawahi kuwa hatari kwa raia yoyote, Kwanini iwe leo baada ya Masai kujihami waliposhambuliwa na mgambo wa mji? Serikali ya Rais @dr.hmwinyi itafute jawabu la kumaliza mzozo huu sio kufunika kwakuwafukuza Wamasai, Tatizo liko kwa mamlaka za jiji, Tatizo liko kwa Wakuu wa Mikoa, na mamlaka zingine za jiji.

Unawazuia Wamasai wasibebe fimbo unataka Wabebe Vikapu vya Nazi na vigemeo vya Litembo? Unataka wabebe Usinga? Unataka wabebe karafuu? Noooo nooo tukatae unyanyasaji huu kwa jamii ya kimasai! Ukamilifu wa Masai ni fimbo na sime. Sasa unaka awe na shuka tu kama dera?

Kesho yataibuka Bara Wapemba watashambuliwa, Je serikali iweke amri wapemba wasizaliane kwa Wingi Bara ambao ni sehemu ya utamaduni wao? Nooo Nooo! Tukatae ubaguzi huu.

Mh Rais @dr.hmwinyi ili kunusuri maafa zaidi na kuoondoa hii taswira mbaya ya ubaguzi iliyotengenezwa na mamlaka za mji hapo Unguja, Ninakuomba na kukusihi Mh Rais, tengua hii kauli ya kibaguzi, Haifai kutolewa na kiongozi wa serikali katika ulimwengu wa leo! Madhara yake ni makubwa zaidi mbeleni.

Serikali ijifunze kutatua migogo kwa hekima na busara, Majibu ya hasira ya kiserikali yanaweza kuleta maafa zaidi kuliko kutatua, Nimeisikiliza kauli ikitolewa na yule kiongozi wa mjinibZanzibar (Unguja) ni wazi alitawaliwa na ghadhabu zaidi kuliko hekima ya kiuongozi, Amewahukumu Wamasai bila kujaribu kujua undani na kutafuta jawabu, Badala yake ametafuta jibu ambalo ni la hovyo zaidi!,

Nimesikitika sana kwa kauli hii ya serikali ya Zanzibar katika zama hizi za utandawazi na utandaridhi! Utengamano wa taifa letu ni muhimu kuliko hizi chuki zinazokolezwa na namlaka za nchi!

Na Yericko Nyerere
IMG_0164.jpeg
 
Hata Kanuni ya adhabu(Penal Code) ya Tanzania bara(acha zanzibar), nadhani ni sura ya kumi na sita (Cap 16.R.E. 2019) pia hairuhusu.

Na zanzibar kama nchi wana haki ya kuwa na utaratibu wao. La msingi tu, wakae nao wawaelimishe. Wasiweke matumizi makubwa ya nguvu
 
Ukimsikiliza ni chuki tu za kibaguzi. Eti kama wanataka kufanya biashara wafungue maduka na wasibebe sime wala marungu. Hiv nchi hii wamasai wamewakosea nini. Maana porin kwao wamefukuzwa na huku mjin wanakojitafuta hawatakiwi. Mnataka wafanye nini waende wapi.
 
Hata Kanuni ya adhabu(Penal Code) ya Tanzania bara(acha zanzibar), nadhani ni sura ya kumi na sita (Cap 16.R.E. 2019) pia hairuhusu.

Na zanzibar kama nchi wana haki ya kuwa na utaratibu wao. La msingi tu, wakae nao wawaelimishe. Wasiweke matumizi makubwa ya nguvu
Wawaelimishe kuacha utamaduni wao? We mzima? Kwani utamaduni wao ni sababu ya kukosa elimu? Kuna machizi mengi sana Tanzania.
 
Wawaelimishe kuacha utamaduni wao? We mzima? Kwani utamaduni wao ni sababu ya kukosa elimu? Kuna machizi mengi sana Tanzania.
Mbona ukeketaji watu wameelimishwa, wakaacha,na ilikuwa utamaduni wa baadhi ya jamii.

Sasa kwa dunia ya artificial intelligence, hayo mafimbo na marungu, na mavisu yana faida gani? Ni sawa na kukomalia kulala porini Ngorongoro, bila nyumba eti utamaduni

Hizo fimbo ni za kuchungia ngombe, wana ngombe huko zanzibar hao wamasai? Kuna simba zanzibar kwamba watakutana naye wapambane naye kwa kutumia hizo silaha?

Utamaduni wa konyo
 
Mbona ukeketaji watu wameelimishwa, wakaacha,na ilikuwa utamaduni wa baadhi ya jamii.

Sasa kwa dunia ya artificial intelligence, hayo mafimbo na marungu, na mavisu yana faida gani? Ni sawa na kukomalia kulala porini Ngorongoro, bila nyumba eti utamaduni

Utamaduni wa konyo
Yaan we jombaa ni kiaz hebu nenda China vijijin huko au hata Japan au hata sehem za Scotland au hata uarabuni hasa jamii za mabedui. Au Namibia. Sio kila mtu anataka kuvaa hayo masuti ni ishu kwake au nyumba za block. Kuna watu kuishi kienyeji ndio furaha yake. Ndio jamii za asili wameamua wao kwanini wewe uwapangie furaha yao hapa dunian. Na ninan kakuambia kuvaa kizungu ndio umeendelea.
 
Mbona ukeketaji watu wameelimishwa, wakaacha,na ilikuwa utamaduni wa baadhi ya jamii.

Sasa kwa dunia ya artificial intelligence, hayo mafimbo na marungu, na mavisu yana faida gani? Ni sawa na kukomalia kulala porini Ngorongoro, bila nyumba eti utamaduni

Hizo fimbo ni za kuchungia ngombe, wana ngombe huko zanzibar hao wamasai? Kuna simba zanzibar kwamba watakutana naye wapambane naye kwa kutumia hizo silaha?

Utamaduni wa konyo
He he he..... Leo atakutambua jinsi unavyomchamba... Hawajui ninyi wapemba.... 🤣
 
Hakuna uhatari wowote kwa muungano wetu adhimu, hakuna Jamii sikivu na yenye umoja na pia isiyotaka Shari kama masai, ukiona umegombana nao basi elewa wewe binafsi ndiye mshari, ufanywe mkutano waitwe wapewe taratibu za kiusalama, case closed!, hutasikia tena tatizo lolote mbeleni. (hayo mavazi na rungu na sime ni Utamaduni wao adhimu).
 
Kesho yataibuka Bara Wapemba watashambuliwa, Je serikali iweke amri wapemba wasizaliane kwa Wingi Bara ambao ni sehemu ya utamaduni wao? Nooo Nooo! Tukatae ubaguzi huu.
Siyo Tanganyika, sisis ni matakataka, makondoo, rubbish tumetawaliwa na woga and CCM makes advanage of this. nani aamke awafukuze wapemba? na sasa mpemmba anatawala bara sahau
 
Yeriko Nyerere give us a break
Fimbo na sime za kina Ole Ngurumwa zinahatarisha Muungano?🤧
Hivyo Wamarekan/Watanzania wasizuiwe kutembea na AR-15 machine guns barabarani
Maasai sio watu exceptional zaidi ya WaTz wengine
 
Hakuna uhatari wowote kwa muungano wetu adhimu, hakuna Jamii sikivu na yenye umoja na pia isiyotaka Shari kama masai, ukiona umegombana nao basi elewa wewe binafsi ndiye mshari, ufanywe mkutano waitwe wapewe taratibu za kiusalama, case closed!, hutasikia tena tatizo lolote mbeleni. (hayo mavazi na rungu na sime ni Utamaduni wao adhimu).
Nitajie faida 10 za Huu muungano adimu?

Ikiwezekana taja foida za muungano Kwa upande wa Bara!
 
Ukimsikiliza ni chuki tu za kibaguzi. Eti kama wanataka kufanya biashara wafungue maduka na wasibebe sime wala marungu. Hiv nchi hii wamasai wamewakosea nini. Maana porin kwao wamefukuzwa na huku mjin wanakojitafuta hawatakiwi. Mnataka wafanye nini waende wapi.
Wamasai wapo ZNZ kwa miongo kadhaa sasa, kwanini hiyo chuki ianze leo? Acheni kujizima data. Hivi ni mara ngapi nchi hii Wakulima wamekuwa wakishambuliwa na hata kuuawa na jamii ya wafugaji hususani Wamasai? Ni kipi kinawawezesha Wamasai kufanya mashambulizi yao kirahisi hivyo kama sio hiyo the so-called utamaduni wv kutembea na silaha? Acheni ku-justify ujinga kwa kigezo eti cha utamaduni kwa sababu hata huo utamaduni lazima uendane na mazingira. Kwenye yale mazingira yao ya asili ni sawa tu hata kutembea na bunduki kwa sababu you never know ni wakati gani wanyama wakali watatokea mbele yao, sasa Zanzibar unatembea na silaha kwa sababu zipi? Halafu kwanini mnaona ni Wamasai ni exceptional community ambapo sheria zingine ziwaguse wengine tu lakini sio Wamasai? Hii nchi kila kabila lina maeneo yake ya asili, na baadhi yao wamekuwa wakihamishwa vile vile lakini hatujawahi kusikia haya madai ya "mnatuhamisha maeneo yetu ya asili". Wamasai ni jamii ya kwanza kuhamishwa kwenye maeneo tengefu au kwenye hifadhi za taifa?
 
Nina laani kwa nguvu zote kitendo cha vurugu za mgambo na watu wa jamii ya kimasai kwakupigana hadharani, Nina laani Masai kushambulia Mgambo, Nina laani kwa nguvu kubwa Mgambo wa Zanzibar kushanbulia watu wa jamii ya kimasai! Jambo hili halikubaliki kwa mjibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazokataza kupigana hadharani au kificho.

Lakini naomba nitofautiane na hatua iliyochukuliwa na serikali ya Zanzibar, Amri kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime/visu vyao, Ni Kauli Haramu na ya kibaguzi inayohatarisha muungano wa Tangabyika na Zanzibar.

Ifahamike kuwa Fimbo na Sime kwa Jamii za kimasai ni sehemu ya “vazi lao la asili”, ni Sehemu ya utamaduni wao, Ni Identity yao, na hivyo kujaribu kwa aina yoyote kuondoa kimoja wapo katika hivyo vinavyokuwa ndani ya mwili wa Masai ni kutangaza kuwafukuza Wamasi Zanzibar, Hili ni tangazo la kijinga limekurupukwa na mamlaka za Zanzibar!

Kwamiaka yote tangu kabla ya uhuru hadi leo, Jamii za Wamasai wapo Zanzibar na utamaduni wao wa visu/Sime na Fimbo, hakujawahi kuwa hatari kwa raia yoyote, Kwanini iwe leo baada ya Masai kujihami waliposhambuliwa na mgambo wa mji? Serikali ya Rais @dr.hmwinyi itafute jawabu la kumaliza mzozo huu sio kufunika kwakuwafukuza Wamasai, Tatizo liko kwa mamlaka za jiji, Tatizo liko kwa Wakuu wa Mikoa, na mamlaka zingine za jiji.

Unawazuia Wamasai wasibebe fimbo unataka Wabebe Vikapu vya Nazi na vigemeo vya Litembo? Unataka wabebe Usinga? Unataka wabebe karafuu? Noooo nooo tukatae unyanyasaji huu kwa jamii ya kimasai! Ukamilifu wa Masai ni fimbo na sime. Sasa unaka awe na shuka tu kama dera?

Kesho yataibuka Bara Wapemba watashambuliwa, Je serikali iweke amri wapemba wasizaliane kwa Wingi Bara ambao ni sehemu ya utamaduni wao? Nooo Nooo! Tukatae ubaguzi huu.

Mh Rais @dr.hmwinyi ili kunusuri maafa zaidi na kuoondoa hii taswira mbaya ya ubaguzi iliyotengenezwa na mamlaka za mji hapo Unguja, Ninakuomba na kukusihi Mh Rais, tengua hii kauli ya kibaguzi, Haifai kutolewa na kiongozi wa serikali katika ulimwengu wa leo! Madhara yake ni makubwa zaidi mbeleni.

Serikali ijifunze kutatua migogo kwa hekima na busara, Majibu ya hasira ya kiserikali yanaweza kuleta maafa zaidi kuliko kutatua, Nimeisikiliza kauli ikitolewa na yule kiongozi wa mjinibZanzibar (Unguja) ni wazi alitawaliwa na ghadhabu zaidi kuliko hekima ya kiuongozi, Amewahukumu Wamasai bila kujaribu kujua undani na kutafuta jawabu, Badala yake ametafuta jibu ambalo ni la hovyo zaidi!,

Nimesikitika sana kwa kauli hii ya serikali ya Zanzibar katika zama hizi za utandawazi na utandaridhi! Utengamano wa taifa letu ni muhimu kuliko hizi chuki zinazokolezwa na namlaka za nchi!

Na Yericko Nyerere
View attachment 2890368
Wamasai wanatembea na vifimbo zao kwa sababu ya kuchunga ngombe zao. Jee zanzibar huwa wanachunga ngombe? Acheni hoja za kitoto. Mambo yanabadilika.
 
Ukimsikiliza ni chuki tu za kibaguzi. Eti kama wanataka kufanya biashara wafungue maduka na wasibebe sime wala marungu. Hiv nchi hii wamasai wamewakosea nini. Maana porin kwao wamefukuzwa na huku mjin wanakojitafuta hawatakiwi. Mnataka wafanye nini waende wapi.
Nenda ukoo MBONA nyinyi mliwahamisha Wamasai Toka maeneo Yao ya ASILI hamkuita ubagizi watanganyika mmmechanganyikiwa chukibza wazi Kwa wazanzibar lakini bure tuu sisi tiutalinda IYAMBULISHO wetu DAIMA
 
Back
Top Bottom