Rais Nicolas Maduro wa Venezuela Anusurika Kuuawa

Rais Nicolas Maduro wa Venezuela Anusurika Kuuawa

Nalendwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2016
Posts
7,467
Reaction score
13,026


Rais wa Venezuela amenusulika katika jaribio linalosemekana la kutaka kumuua kwa kutumia drone device, wakati akihutubia mkutano mjini Caracas. Rais Maduro hakupata madhara yoyote katika tukio hilo ingawa wanajeshi saba waliumia.

Television ya Taifa ilionyesha hotuba ya Rais ikikatishwa ghafla wakati wa sherehe (National Guard's 81 anniversary)
Waziri wa habari wa Venezuela amenukuliwa akisema, "There had been an "attack" against the president involving drones loaded with explotives. Maduro is "fine" and continuing to work"

==========

Maduro.jpg

Rais wa Venezula Nicolás Maduro anasema amenusurika jaribio la kumuua kwa kutumia ndege isiyokuwa na rubani iliyokuwa na vilipuzi.

Bwana Maduro alikuwa akizungumza wakati wa warsha moja ya kijeshi mjini Caracas wakati jaribio hilo la kumuua lilitokea.

Video ya hotuba yake inaonyesha rais akitazama juu ghafla kwa hofu huku wanajeshi kadhaa wakikimbia.

Bw Maduro ameilaumu Colombia kwa shambulizi hilo madai ambayo yakananushwa na Colombia.
Wanajeshi saba walijeruhiwa na watu kadhaa wakakamatwa kwa mujibu wa mamlaka za Venezuela.

Kipi kinafahamika kuhusu shambulizi hilo?
Kisa hicho kilitokea wakati Bw Maduro alikuwa akizungumza kwenye warsha ya kuadhimisha miaka 81 ya jeshi la taifa.

Ndege mbili zisizokuwa na rubani zilizokuwa zimejazwa milipuko zililipuka karibu na jukwaa la rais, kwa mujibu wa waziri wa mawasiliano Jorge Rodriguez

Bw Maduro baadaye alisema kuwa "kifaa kilichokuwa kinaruka kililipuka karibu na mimi, mlipuko mkubwa. Sekunde chache baadaye kulikuwa na mlipuko wa pili."

Picha kwenye mitandao wa kijamii zilionyesha walinzi wakimlinda Maduro wakitumia vifaa visivyopenya risasi baada ya shambulizi hilo.

Bw Maduro aliilaumu nchi jirani ya Colombia na vikundi vingine vyenye uhusiano na Marekani kwa njama hiyo ya kutaka kumuua.

Aliongeza kuwa haka shaka kuwa rais wa Colombia Juan Manuel Santos alihusika na jaribio hilo.

Rais huyo wa Venezuela awali ameilaumu Marekani kwa kupanga kumuua lakini hajatoa ushahidi kuhusu hilo.
Serikali ya Colombia imekanusha kuhusika ikisema hakuna ushahidi kwa madai yake Maduro.
 
inakoendea venezuela lazima wataanza kuzichapa wao kwa wao, maisha magumu inflation inakaribia asilimia milioni moja, kila kukicha watu wanakimbia nchi, colombia mpk sasa ishapokea wakimbizi laki nne, kwakweli maduro yupo kwe wakati mgumu sana na hivi assassinations attempts zimeshaanza duh cjui itakuwaje
 
inakoendea venezuela lazima wataanza kuzichapa wao kwa wao, maisha magumu inflation inakaribia asilimia milioni moja, kila kukicha watu wanakimbia nchi, colombia mpk sasa ishapokea wakimbizi laki nne, kwakweli maduro yupo kwe wakati mgumu sana na hivi assassinations attempts zimeshaanza duh cjui itakuwaje


Halafu hii ni mara ya pili?!, wanamtafuta haswa!
 
Mnaojuaga kuchambua siasa mtufundishe.

Nini kimefikisha Venezuela ilipo?

We acha tu, uzuri wanaitwa wachambuzi na sio mafundi au wataalam. Siasa kama mpira tu. Wachambuzi wengiiiii.

Venezuela hii hii wakati wa Hugo ilikua imenawiri kiasi cha yule rais kuwafukuza mashirika kama WB kwamba haihitaji msaada wao ndio imefikia hapa?

Acha tusubirie wachambuzi tu..haina namna.
 
We acha tu, uzuri wanaitwa wachambuzi na sio mafundi au wataalam. Siasa kama mpira tu. Wachambuzi wengiiiii.

Venezuela hii hii wakati wa Hugo ilikua imenawiri kiasi cha yule rais kuwafukuza mashirika kama WB kwamba haihitaji msaada wao ndio imefikia hapa?

Acha tusubirie wachambuzi tu..haina namna.

Thanks. That much I know kwamba Venezuala ilikuwa inafanya vizuri.

I guess bila stability ya nchi hamna kinachoweza kusogeza nchi mbele.

Walikuwa na proper housing system na medical facilities zilikuwa njema sana kama sijakosea.
 
Thanks. That much I know kwamba Venezuala ilikuwa inafanya vizuri.

I guess bila stability ya nchi hamna kinachoweza kusogeza nchi mbele.

Walikuwa na proper housing system na medical facilities zilikuwa njema sana kama sijakosea.
Yaani inafika mahali ni kuombea amani tu katika nchi ndogo zenye utajiri mkubwa maana mdhungu ndio anaziwinda kama simba.
Ni kuomba ulinzi wa kimungu tu walahi!
 
Yaani inafika mahali ni kuombea amani tu katika nchi ndogo zenye utajiri mkubwa maana mdhungu ndio anaziwinda kama simba.
Ni kuomba ulinzi wa kimungu tu walahi!

Of course. Pata picha Venezuela ndo wanashika namba 5 kwa ku export crude oil,kwenda Kwa Trump.

Na kwa Europe ni exporter namba 3 baada ya Marekani na China wa bidhaa zake.

Lazima wampangie mkakati wa kum destabilize wajinyakulie chao mapemaaaa.😕😕
 
Back
Top Bottom