Rais Putin aihakikishia Afrika kuilinda kwa Chakula na Mbolea. Asema Russia na Afrika ni marafiki wa Kufa na Kupona!

Kwa chakula gani alichokuwa nacho Russia kuweza kusaidia Africa

Ngano kwa Africa sio kipaumbele sn, atafute namna ya kupambana na hali yake
 
Kwa Mara ya kwanza wa afrika wanejitambua rafiki wa kweli ni nani!
Russia ni rafiki wa kweli kwa Africa!

Russia ni rafiki wa kweli kwa viongozi wa kiafrika wanaokaa madarakani kwa shuruti. Viongozi wanajua kabisa Russia hana tabia ya kuhoji chaguzi za kihuni, hivyo kwao Russia ni rafiki. Cha ajabu wakiiba pesa wakiwa madarakani, hawaweki kwenye bank za Russia, bali huweka kwa wazungu wa magharibi.
 
Kwani mack Sall katuma na Nani umoja wa. Africa au kaenda kivyake vyake
 
Mimi siiungi hoja.
Simpendi Rais Putin huyu mfalme wa madaraka milele. Wa kuvamia wazungu Ukrain na nchi huru. Wa kutishia kupiga unclear dunia.
Ni hatua ngapi tumetoka na Ulaya wakitusaidia? Yeye Putin kama kiongozi hata Africa hajakanyaga
Utakuwa hata elimu yako ni tatizo, kama sio elimu basi hata taarifa za kidunia hufuatirii, huwezi kuilaumu russia kwa inachokifanya bila kuwasahau NATO ama mataifa ya ulaya& USA, hawa ndio madicteta kwa mgongo wa Democracy uchwara, hawa ndio wauwaji na washenzi kulko hata huyo putin ambaye anafanya hayo kwa maslahi ya ulinzi wa nchi yake.

Alafu ni nani aliwadanganya mtu kukaa madarakani milele ni udicteta? Haya ninyi ambao si madicteta mnawazid vip chinese wanaoongozwa na rais wa milele? Hiyo demokrasia yenu inawazid vip russia? Saud arabia je? Haya basi hata huwaoni hao Uingereza ambao cheo cha urais hakipo kipo cheo cha Prime minister ambaye yuko chini kimamlaka na malkia wa uongoz usio wa kidemocras, je huoni hapo kuna uongoz wa rais dicteta aliye kwenye kivuli na kificho cha umalikia?

Haya na huko USA kwenye demokrasia kipindi cha uchaguz kati ya donard trump na clinton unajua wazi aliyeshinda ni huyo mwanamke clinton, je kwanini uongoz apewe ambaye hakushinda ambaye ni trump? je huo si udicteta na kuhujumu haki za wapiga kura?

Kama hamjui mambo yanavyokwenda duniani ni bora muwe mnakaa kimya kuliko kujiaibisha hapa mitandaoni
 
haya ni maendeleo ya kifikra ya mtu mweusi mahali penye ugali ni muhimu kupatambua na kujipendekeza maana ukivunga huna njaa tajiri Russia anapita 120!
 
Wewe ndiye ambaye shule haijakusaidia.mwenzako kaeleza jinsi ambavyo hapendi viongoz wanaoumiza wengine nakung'ang'ania madaraka wewe unakuja na ngonjera zakumchagulia upande kwani amekwambia anaunga hao wazungu kwa wanayoyafanya.Mambo mengine uliyoyaandika ni mtazamo wako ila kama kuna mambo mabaya yanafanywa na kiongozi yoyote yule duniani watu wanapaswa kusema na kukemea.Russia analaumiwa kwasababu kaanzisha vita yakuua watu wasio na hatia bila sababu za msingi.Hoja yake ni nyepesi sana ukilinganisha na hoja zilizowahi kutumiwa na wengine kuzivamia nchi zingine.Japo yote hayo ni makosa kwasababu wanaoumia ni raia wasio na hatia.Hizo nchi ulizotaja bado wana demokrasia kubwa kulingana na katiba zao.Uingereza ni nchi ya kifalme hadi watakapobadilisha hiyo katiba yao.ata china wanaenda kulingana na katiba yao.siku watakayoona kuna haja yakubadilisha muundo wa serikali zao watafanya hivyo.mengine umeleta story za vijiweni.
 
Sasa kama ni lafiki wa afrika si atuletee mafuta ya bei nafuu mambo ya mbolea yatajipa unafuu yenyewe,

Kama alitaka kuyauza india kwa pipa dola 30-35 si atuuzie sisi hiyo bei aone kama hatuendi kumsaidia vita hukohata kupigana tu?
 
Nakuona leo meno yote 18 ya watu wa kibera yapo nje[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji1787][emoji1787][emoji1787] MK254 Tony254
 
Jiran zetu wanapaswa kutochukua hiyo misos+mbolea ili kumuonyesha Putin kuwa hakuwa na taarifa sahih wakat anawajibu kuhusu mtazamo wa kenya ktk op inayoendelea
 
Respect kwako kaka, umeainisha masuala yote muhimu na za msingi, kujikomba ndio jadi ya jamii yetu, bahati mbaya mambo hayakuwa hivyo miaka ya nyuma maana wazee wetu walikuwa radhi kufa kuliko kumsujudia huyo fake messiah (white man).

“Here's a message to the newborns waitin' to breathe
If you believe, then you can achieve just look at me!
Against all odds, though life is hard we carry on
Livin' in the projects, broke with no lights on
To all the seeds that follow me, protect your essence
Born with less, but you still precious
Just smile for me now!” Tupac
 
Mimi siiungi hoja.

Simpendi Rais Putin huyu mfalme wa madaraka milele. Wa kuvamia wazungu Ukrain na nchi huru. Wa kutishia kupiga unclear dunia.

Ni hatua ngapi tumetoka na Ulaya wakitusaidia? Yeye Putin kama kiongozi hata Africa hajakanyaga
Ukiwapenda wazazi wako inatosha Acha kiherehere cha kupenda watu wasiokujua
 
Ukiona mtu haingilii mambo yako ya ndani hata yawe mabaya ujue anakuheshimu na anaheshimu utashi wako na privacy Zako, na huo ndio uungwana! Na ukiona mtu anahangaika na mambo yako haswa ya ndani ujue amekuzoea vibaya na hakuheshimu na anakuona huna akili!
Kwa Aafrika hii tabia ukifinywa unapayuka ili jirani aje amgombeze mama yako au baba yako na u mtu mzima huu ni ulemavu wa akili na kiroho! Afrika lazima tubuni mfumo wa kukomesha uonevu baina yetu bila kubadili rasilimali zetu kwa gombezo au kemeo la mzungu!
Kuhusu kuiba na kuficha pesa nje ya Russia huo ni wizi tu kama wizi mwingine hapa Tanzania maana nazo hufichwa hukohuko nje! Hivyo ni mambo yao huko binafsi huko Russia wanajua wana dili nayo vipi!
 
Mimi siiungi hoja.

Simpendi Rais Putin huyu mfalme wa madaraka milele. Wa kuvamia wazungu Ukrain na nchi huru. Wa kutishia kupiga unclear dunia.

Ni hatua ngapi tumetoka na Ulaya wakitusaidia? Yeye Putin kama kiongozi hata Africa hajakanyaga
Ww kiazi mbatata kweli. Putin amekaa/ameishi Africa miaka mitano mfululizo
 
Achana nawo awoo boss wao wanamuona Putin dicteta vp malkia pale uingereza naye si dicteta, vp mfalme pale uhispani, uholanzi, Denmark, watu ni wapumbavu sana wengi wamesoma lkin akili hawana wanakuja na hadithi zao kuwa matajiri WA urusi wanawaibia wananchi na Kula pesa za mafuta yani matajiri WA nchi za wenzao ni wezi Ila mabilionea wao pale Marekani na ulaya wao ni wasafi na hawanashida yoyote wamejilimbilizia mabilioni ya Dola Ila bado wanailaumu matajiri WA nchi za wengine et kisa wako karibu na raisi WA nchi yake useless kabisa
 
Anaweza akavileta na viongozi wa Afrika wakashindwa kupokea, kama mafuta wameshindwa kununua ya Russia ambayo ni bei rahisi hizo mbolea na chakula wataweza kuvichukua?
Hivi hayo mafuta ya bei rahisi toka Russia ni yapi?
Africa tukisema tunaacha kununua mafuta toka Opec na kwenda Russia lazima bei itapanda na hii no kutokana na distance of Transportation, the same case kwa European countries kuacha mafuta ya Russia na kununua ya waarabu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…