Rais Putin kutangaza usiku huu Russia kutambua rasmi majimbo huru yaliyojitenga ya Donetski na Luhansk

Rais Putin kutangaza usiku huu Russia kutambua rasmi majimbo huru yaliyojitenga ya Donetski na Luhansk

Putin: "We've made it clear that any further movement of NATO to the East is unacceptable. Is there anything unclear about this? Are we deploying missiles near the US border? No, we are not. It's the US that has come to our home with its missiles and is standing at our doorstep." https://t.co/BXTya1yGOZl
 
Not cancel, suspend. Wanahitaji gesi hao mzee.
Hii ultimatum Putin alishapewa mapema kabisa na Nato akiivamia ukranie Nord stream 2 is dead...Labda hufuatilii vitu...
We unafkiri Russia hataki kuuza gas ulaya?...Tena in long run Nato watatafuta alternative ya Nord Stream 1 halafu nayo waipige chini
 
Ukraine ni lost territory na Russia wataichukua ikiwa wataingia Kyiv kupitia ardhini, majini na hewani -land sea and air invasion.

Hivi sasa wameweka kitu chaitwa corridor au springboard yaani eneo maalum la kupita kuingia rasmi ndani zaidi ya eneo la Donbass.

Upo sahihi majeshi ya Ukraine yapo sawasawa yanasubiri na itakuwa vita kwelikweli na wengi raia wa Ukraine watapoteza maisha.

Putin sio mjinga amepanga hii mavitu tangu 2020 na Marekani wanafahamu hilo kupitia CIA na majasusi wa NATO.

Akifanikiwa next, regime change na kumuondoa Zelensky, kumbuka jana amesema serikali ya sasa ya Ukraine ni ya vibaraka na wameifanya Ukraine koloni la Marekani.

Baada ya hapo kuna kitu chaitwa "incorporate lost territory".

Mwisho Ukraine itakuwa kama Crimea.

Mimi sipendi vita ila napenda kuona haki sawa na kwamba hizi vita za kijiografia ili mataifa makubwa kujiweka sawa zina ulazima endapo taifa jingine latumia hila dhidi ya taifa jingine.

NATO, West na Marekani lazima waiheshimu Russia kama ni superpower na ana mabomu ya nyuklia pamoja na kiti cha kudumu UN.

Pia Russia ana kura ya Veto UN hivyo jaribio lolote la kuishinikiza kuhusu masuala yoyote yanotishia usalama wake atapinga.
Shida ni kwamba hawa watu wa mashariki wanajiona wao ndo kila kitu, hawataki hata kumsikiliza Putin, kumbuka wiki 2 au 3 nyuma wakati Urusi wanaomba Diplomasia itumike walijibu nn? Zaidi ndo wakaanza kutoa misaada ya vifaa vya kivita kw ukraine na kupeleka majeshi. Walimuona kama mwehu asiye na chochote na ha2ana muda wa kumsikiliza leo wanalalamika kwamba kavubja international law nk. Usimdharau mtu maishani siku zote
 
Je kama Putin amesaini mkataba wa kuyatambua hayo majimbo, Ukraine bado inasubiri nini kuwa mwanachama wa NATO au NATO wanasubiri nini kutompa uanachama Ukraine? , hebu wataalamu wa geopolitics mnidadavulie hapa.
Hawezi na Ulaya haiwezi kuchukua hiyo risk kumoa uanachama Ukraine,hadi Dunia inaisha haitakuja kutokea Ukraine kujiunga na NATO na ikitokea basi hiyo itakuwa WWW3.
 
Nimeangalia TV ya Urusi. Ziko nyingi tv Urusi. Kama unafahamu kirusi , angalia au Kama Una mtu Urusi mpigie simu atakuambia maisha yalivyoanza kuwa magumu
Hahaaaa....ety kama Nina MTU urusi nimpigie simu. Umetisha sna
 
Uchumi wa Russia kwa mujibu wa WIKIPEDIA.

1. Russia ni nchi ya 11 kwa uchumi mkubwa duniani kwenye GDP na PPP.

2. GDP - sekta ya huduma ni 62%, sekta ya viwanda 32% na sekta ya kilimo ni 5% na watu wasoajiriwa ni 4.3%

3. Akaunti ya fedha za kigeni ni bilioni 638 na ni ya 4 kwa ukubwa huo duniani.

4. Wafanyakazi au "labour force" ni milioni 70 na inaifanya Russia kuwa ya 6 duniani.

5. Russia ni ya 10 duniani kwa utengenezaji magari.

6. Russia ni moja ya nchi duniani zenye madeni madogo sana.

7. Russia ni nchi ya 20 duniani kwa uingizaji na usafirishaji bidhaa duniani.
Mkuu waache waendelee kuamini uchumi wa Urusi ni mbovu mana anayewaaminisha ndo katuaminisha pia kuwa tuko uchumi wa kati[emoji28]
 
Kuupata uanachama wa NATO huwa ni mchakato mrefu. Kwanza kuna vigezo kadhaa ambavyo lazima nchi husika iwe imekidhi vigezo hivyo. Pia, lazima kuwe na makubaliano ya pamoja (consensus) ya wanachama wote waliopo ndani ya jumuiya hiyo.

Nchi wanachama zitaendesha mchakato maalumu wa kukubaliana na ombi hilo la uanachama kutoka kwa nchi husika. Mfano; kwa Marekani, mchakato utahusisha bunge (congress) pia. Nchi zingine zitafanya mchakato huo pia baada ya kupitia katika vyombo vyao vya maamuzi.

Moja ya vigezo vya kupewa uanachama ni nchi husika kutokuwa na migogoro hasa ya kimipaka inayoweza kuchochea nchi kugawanyika. Hili ndilo linalosababisha baadhi ya nchi za NATO kama Ujerumani na Ufaransa kutilia mkazo kuwa Ukraine haistahili kupewa uanachama kwa sasa mpaka hapo baadaye.

Ukraine kwa sasa imewekwa katika mpango maalumu wa NATO wenye nchi sita unaofahamika kama Enhanced Opportunities Partnership (EOP) kama mpango maalumu wa ushirikiano wa karibu baina ya NATO na Ukraine pamoja na baadhi ya nchi zingine.
Hayo ni maneno tu Nchi gani ya Ulaya inaweza kukubali Ukraine kupewa uanachama.
 
And you think Russia doesn't need Europe Money?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Shida unashundwa kuelewa haya mavuguvugu huwa yanatengenezwa. Marekani walitengeneza vuguvugu mwaka 2014 ivyo hata russia haya mavuguvugu anayatengeneza, wahuni wa Cremia, ndo walipomaliza kazi wakaenda kuongeza nguvu donetsk na donbass. Pia washamaliza wanahamishia nguvu jimbo lingine, hii Ukraine itaisha tu ikiendelea na ujinga wake wa NATO
Akatengeneze vurugu kyiv basi[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Anazidiwa kutokana na vigezo walivyo viweka IMF&WB inayomilikiwa na USA au sio?.
USA yenyewe inacho ibeba sasa hivi ni matumizi ya dola -China amisha mpita muda au wewe upo Dunia ya ngapi ndugu.
Sasa ni vigezo gani vitumike yaani kwamba IMF/WB waseme china ni ya pili india brazili zipo top ten ila wanaposema Russia hayupo top ten kuna vigezo!! namba zinaongea mkuu hakuna longolongo !!! basi Russia ajiwekee vigezo vyake ajipe namba 1 ikimpendeza North Korea iwe ya pili kiuchumi kwa vigezo vya Kirusi🤣😂😅
 
Anazidiwa kutokana na vigezo walivyo viweka IMF&WB inayomilikiwa na USA au sio?.
USA yenyewe inacho ibeba sasa hivi ni matumizi ya dola -China amisha mpita muda au wewe upo Dunia ya ngapi ndugu.
Mbona Russia au china ndo hivyo hivyo anavyovitumia, tupe basi hizo takwimu za china kumpita marekani ana gdp ya sh ngapi nasubiria
 
Huyu andunje haachi vituko. Bei za petrol [emoji618]️ zitapanda kwa ufala wake.
 
Hawezi na Ulaya haiwezi kuchukua hiyo risk kumoa uanachama Ukraine,hadi Dunia inaisha haitakuja kutokea Ukraine kujiunga na NATO na ikitokea basi hiyo itakuwa WWW3.
Mkuu samahani sana naomba niulize tena, ikiwa tayari Urusi imeshatia nanga Ukraine, na inaonekana NATO na washirika wake hichi ndicho walichokuw wakihofia na sasa kimefanyika, ni kwa nini nchi za ulaya haziwezi kukubali?, kwamba endapo NATO itatangaza kwamba Ukraine ni mwanachama wake, Russia itatangaza vita rasmi na Ukraine? Ni nini sababu ya msingi haswa ya kuendelea kukwamisha Ukraine asiwe mwanachama, ingali haya yameshatokea.
 
Aliongea Russia kujiunga NATO kwa namna ya kudhihaki,sasa wewe ndugu anavyoelezea ni kana kwamba kweli Russia alitaka kujiunga NATO.

Sasa Russia atajiungaje kwenye muungano ulioindwa na Nchi 28+ kwa lengo la kumdhibiti yeye mwenyewe(Russia)-kutakuwa na umuhimu gani wa huo muungano kama hiyo adaui wenu naye anajiunga?.
Ni Putin yupi huyo aliyeongea maneno hayo kwa namna ya kudhihaki? Huyu wa jana, ama yule wa kabla ya jana?!

Hata hivyo, nimejibu kuendana na kile kilichoandikwa na mchangiaji niliyemjibu. Huyo niliyemjibu anasema kwamba, Clinton alipoulizwa kuhusu Urusi kujiunga NATO alikaa kimya, kitu ambacho ni tofauti na maelezo ya Putin ya miaka ya nyuma. Maelezo yake hayako consistent!
 
Back
Top Bottom