Rais Ruto aapa kuwachakaza wapinzani wakiendeleza maandamano

Rais Ruto aapa kuwachakaza wapinzani wakiendeleza maandamano

Kenyan

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2012
Posts
414
Reaction score
314
Rais William Ruto ameapa kutumia nguvu zote alizonazo kuhakikisha maandamano ya Azimio yaliyopangwa kufanyika Jumanne wiki ijayo, hayatazidi kuwa machafuko na ghasia.

Hisia za Ruto zinafuatia hatua ya Muungano wa Azimio la Umoja kurejesha maandamano nchi nzima juu wakidai Kenya Kwanza kushindwa kufanya mazungumzo yenye manufaa ya pande mbili.

Akizungumza mjini Malava, Kaunti ya Kakamega siku ya Jumamosi, Rais Ruto alisema aliwasiliana na kiongozi wa Azimio, Raila Odinga katika juhudi za kutafuta suluhu ili kumaliza mzozo unaoendelea kati ya upinzani na serikali yake.

Licha ya juhudi zake, Ruto anasema Raila ameonekana kukataa n kuwaelekeza wafuasi wake kushiriki maandamano hayo.

"Mimi niliwaambia ile wiki ingine; nikaita yule mzee wa kitendawili na nikamwambia wewe wacha hii maandamano tupeleke hii maneno yote unasema bunge; wabunge waangalie kama kuna maneno ya ukweli," alisema Ruto.

"Sasa ati wamekataa hiyo ya kwenda kuongea kwa amani kwa bunge. Ati wanataka kurudi maandamano. Ati waende wavunje mali na kuharibu biashara ya wananchi. Mimi ndio commander-in-chief. Nyinyi mtajua hamjui. Wawache hiyo mchezo."

Huku akiyafananisha maandamano ya Azimio na uhujumu uchumi, Ruto aliongeza kuwa kipaumbele cha serikali yake ni kuboresha maisha ya Wakenya na kutokuwa na ugomvi na upinzani.

"Mambo ya uchaguzi tulimaliza last year. Ile kazi imebaki sasa si ya viongozi; kazi imebaki ni maendeleo ya wananchi," aliongeza.

"Hakuna mali au biashara ya wananchi itaharibika tena. Serikali ya Kenya itasimama imara kuhakikisha inalinda maisha, mali na biashara ya kila mwananchi."
 
Rais William Ruto ameapa kutumia nguvu zote alizonazo kuhakikisha maandamano ya Azimio yaliyopangwa kufanyika Jumanne wiki ijayo, hayatazidi kuwa machafuko na ghasia.

Hisia za Ruto zinafuatia hatua ya Muungano wa Azimio la Umoja kurejesha maandamano nchi nzima juu wakidai Kenya Kwanza kushindwa kufanya mazungumzo yenye manufaa ya pande mbili.

Akizungumza mjini Malava, Kaunti ya Kakamega siku ya Jumamosi, Rais Ruto alisema aliwasiliana na kiongozi wa Azimio, Raila Odinga katika juhudi za kutafuta suluhu ili kumaliza mzozo unaoendelea kati ya upinzani na serikali yake.

Licha ya juhudi zake, Ruto anasema Raila ameonekana kukataa n kuwaelekeza wafuasi wake kushiriki maandamano hayo.

"Mimi niliwaambia ile wiki ingine; nikaita yule mzee wa kitendawili na nikamwambia wewe wacha hii maandamano tupeleke hii maneno yote unasema bunge; wabunge waangalie kama kuna maneno ya ukweli," alisema Ruto.

"Sasa ati wamekataa hiyo ya kwenda kuongea kwa amani kwa bunge. Ati wanataka kurudi maandamano. Ati waende wavunje mali na kuharibu biashara ya wananchi. Mimi ndio commander-in-chief. Nyinyi mtajua hamjui. Wawache hiyo mchezo."

Huku akiyafananisha maandamano ya Azimio na uhujumu uchumi, Ruto aliongeza kuwa kipaumbele cha serikali yake ni kuboresha maisha ya Wakenya na kutokuwa na ugomvi na upinzani.

"Mambo ya uchaguzi tulimaliza last year. Ile kazi imebaki sasa si ya viongozi; kazi imebaki ni maendeleo ya wananchi," aliongeza.

"Hakuna mali au biashara ya wananchi itaharibika tena. Serikali ya Kenya itasimama imara kuhakikisha inalinda maisha, mali na biashara ya kila mwananchi."
Ruto akijaribu huo ujinga ndo mwishi wa Taifa la Kenya, Kenya sio kama TZ, Kenya nikama ka-single room.

.
 
Ruto anamtisha nani? Odinga? Huyo anacheza na moto. Odinga Hana Cha kupoteza pia hao waandamanaji hawana Cha kupoteza maana hawana ajira Wala mitaji ya biashara huku gharama za maisha zipo juu. So akitumia mabavu ajue atasababisha Nairobi iwake moto na kutapakaa nchi nzima.
 
Ruto anamtisha nani? Odinga? Huyo anacheza na moto. Odinga Hana Cha kupoteza pia hao waandamanaji hawana Cha kupoteza maana hawana ajira Wala mitaji ya biashara huku gharama za maisha zipo juu. So akitumia mabavu ajue atasababisha Nairobi iwake moto na kutapakaa nchi nzima.
Ndo uhuru alimchukua raila na kumuweka upande wake ilimsaidia sana kutawala nchi
Raila alishakaa jela miaka 10 huwez mtishia tishia kirahis, moi aliua watu wengi kenya waliokua wanampinga/kumkosoa ila hakuthubutu kumgusa raila
 
Ruto anamtisha nani? Odinga? Huyo anacheza na moto. Odinga Hana Cha kupoteza pia hao waandamanaji hawana Cha kupoteza maana hawana ajira Wala mitaji ya biashara huku gharama za maisha zipo juu. So akitumia mabavu ajue atasababisha Nairobi iwake moto na kutapakaa nchi nzima.
Hapa ni mapokezi toka JKIA kwenda kwa mkewe mama Ida, si maandamano.... Hiyo J4 itakuaje?
 

Attachments

  • IMG-20230429-WA0038.jpg
    IMG-20230429-WA0038.jpg
    248.5 KB · Views: 4
Hiki ni kilio cha mtu mzima.
Niliona hii habari sehemu nikaona mr Ruto anatishia nyau, maybe tusubiri jumanne tuone nani mkubwa.

Japo kwa mtizamo wangu wataandamana na risasi zitaougwa sana tu, yaani vifo lazima vitakuwepo, leo na kesho jeshi linagawa bunduki na kwa askari ili wazisafishe teyari kwa zoezi la kuua raia!.
 
Yaani kenya,kuanzia viongozi mpaka raia wake wote ni vichwa maji,wamevurugwa hatari,ngoja waandamane,watajua hawajui 😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom