Rais Ruto aliyetutamanisha na Hotuba yake nzuri alipoapishwa ndiyo huyu anayelalamika hali mbaya Kenya?

Rais Ruto aliyetutamanisha na Hotuba yake nzuri alipoapishwa ndiyo huyu anayelalamika hali mbaya Kenya?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
GENTAMYCINE ni Mtu ambaye huwa kwa 95% siziamini Hotuba za Marais pale wakiwa Wanaapishwa kwakuwa kwa Uzoefu wangu huwa ni Hotuba ya Asali Tamu kwa Kuiona ila Kimatumizi huwa ni Chungu na Mbaya kwa Mlaji / Walaji.

Nimemsikiliza na Kumtizama Rais wa Kenya Ruto katika Mkutano wake wa IGAD na kugundua ya kuwa kumbe yale mengi aliyokuwa akituhutubia kwa Mikogo mingi Siku anaapishwa huenda hata asiyakamilishe na asiyakabili hata kwa 25% kutokana na Hali Ngumu ya Uchumi inayoikabili Kenya kwa sasa, Njaa na Tatizo Kubwa la Ajira.

Kuna nchi Moja hivi ( nimeisahau ) na yenyewe mwaka 2025 inafanya Uchaguzi Mkuu wake hivyo GENTAMYCINE namuomba mapema sana huyo atakayeshinda kwa Msaada wa Polisi Wao, Idara yao Nyeti, Uwizi wa Kura na Kusaidiwa na Tume yao ya Uchaguzi kuwa Siku ya Uapisho na Yeye pia asije na Hotuba Asali kama ya Mwenzake Rais Ruto bali awaambie tu Ukweli Wananchi wake kuwa hali itaendelea kuwa mbaya, Kodi zitazidi na Wahalifu kama akina 'Nyapa Diro' ndiyo Wataongezeka maradufu huku Upigaji ukiendelea.

Rais Ruto huku Kwetu nchini Tanzania Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alishasema na kutuambia kuwa Ikulu si mahala pa mchezo mchezo na hapakimbiliwi hovyo nadhani huko Kenya hamkubahatika Kumsikia au Kuusikia hivyo nami GENTAMYCINE leo nakuambia Ikulu hapakimbiliwi na bahati mbaya Kubwa uliyonayo ni kwamba Adui yako Rais Mstaafu Kenyatta si tu kwamba ni Mafia lakini pia ni Mtoto wa Mjini na karibia 85% ya Watu wa 'System' ya Kenya ni loyal Kwake hivyo kuwa makini na una Kazi ya ziada pia katika Uongozi ( Urais ) wako kwa nchi ya Kenya na Wakenya wote.
 
GENTAMYCINE ni Mtu ambaye huwa kwa 95% siziamini Hotuba za Marais pale wakiwa Wanaapishwa kwakuwa kwa Uzoefu wangu huwa ni Hotuba ya Asali Tamu kwa Kuiona ila Kimatumizi huwa ni Chungu na Mbaya kwa Mlaji / Walaji.

Nimemsikiliza na Kumtizama Rais wa Kenya Ruto katika Mkutano wake wa IGAD na kugundua ya kuwa kumbe yale mengi aliyokuwa akituhutubia kwa Mikogo mingi Siku anaapishwa huenda hata asiyakamilishe na asiyakabili hata kwa 25% kutokana na Hali Ngumu ya Uchumi inayoikabili Kenya kwa sasa, Njaa na Tatizo Kubwa la Ajira.

Kuna nchi Moja hivi ( nimeisahau ) na yenyewe mwaka 2025 inafanya Uchaguzi Mkuu wake hivyo GENTAMYCINE namuomba mapema sana huyo atakayeshinda kwa Msaada wa Polisi Wao, Idara yao Nyeti, Uwizi wa Kura na Kusaidiwa na Tume yao ya Uchaguzi kuwa Siku ya Uapisho na Yeye pia asije na Hotuba Asali kama ya Mwenzake Rais Ruto bali awaambie tu Ukweli Wananchi wake kuwa hali itaendelea kuwa mbaya, Kodi zitazidi na Wahalifu kama akina 'Nyapa Diro' ndiyo Wataongezeka maradufu huku Upigaji ukiendelea.

Rais Ruto huku Kwetu nchini Tanzania Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alishasema na kutuambia kuwa Ikulu si mahala pa mchezo mchezo na hapakimbiliwi hovyo nadhani huko Kenya hamkubahatika Kumsikia au Kuusikia hivyo nami GENTAMYCINE leo nakuambia Ikulu hapakimbiliwi na bahati mbaya Kubwa uliyonayo ni kwamba Adui yako Rais Mstaafu Kenyatta si tu kwamba ni Mafia lakini pia ni Mtoto wa Mjini na karibia 85% ya Watu wa 'System' ya Kenya ni loyal Kwake hivyo kuwa makini na una Kazi ya ziada pia katika Uongozi ( Urais ) wako kwa nchi ya Kenya na Wakenya wote.
Reject la SAUT popoma katika ubora wake
 
Back
Top Bottom