Rais Samia aagiza Darasa la Saba waliofutwa kazi walipwe stahiki zao

uongo kwa hiyo kule mtu yeyote aweza kuwa daktari wa operation au rubani bila cheti? vyuo vikuu wanafundisha wasio na vyeti?
Mwendazake angeendelea kuwepo angeambukiza watu wengi Sana roho yake mbaya ya kihutu ndio maana Mungu akaamua ampe umalaika mkuu , ona majitu kwenye huu uzi yanavyoshabikia watu wasilipwe stahiki zao , ndio miaka mitano tu , je angekaa kumi atake asitake si angezalisha maakina Yehodaya mengi sana .
 
Sijui hapa ume-post nini mkuu.
 
Umeongea ukweli kabisa kiongozi. Mwendazake asingekufa angezalisha majitu mengi sana yenye roho mbaya na yasiyozingatia utu wala haki za binadamu. Lazima angezalisha ma Idd Amini ya kutosha katika nchi hii na ipo siku watu wangekuja kuchinjana kuliko ilivyokuwa kwenye mauaji ya kimbari kule Rwanda. Mungu hadhihakiwi ndio maana aliamua kumuondoa duniani kwa maslahi mapana ya taifa hili.
 
Je aliyegushi thesis akawa daktaribwa falsafa kwa njia za kiujanjaujanja ni muhalifu au malaika?
 
Kwa kweli wafungue vifua vyao. Laana nyingine ni za kujitakia.

Zuluma sio nzuri.
 
Wote ni wahalifu na wanatakiwa wawe jela ikithibitika kuwa ni kweli.....
Wa thesis mlimfanyia Nini Kama hai wa vyeti feki mnawahukumu? Basa mmeshawatoa kazini walipeni mafao yao. Kumbuka ni wengi wameumia. Waliohusika na ambao hawakuhusika.

Magereza sio mahali pa kuombeana. Kwa hili kwa sababu nila wengi ni kiasi Cha kurekebishana na serika iweke sheria ya kuwabana waajiri wanapo hakiki. Ila endelea kuwaombea wenzako mabaya kuna siku utajikuta segerea.

Hata wa kisongo Arusha alikuwa anarukaruka na kujiplaudi kila alichokifanya kinapendeza watanzania. Hakuna anaejua na ukweli wa haya mambo zaidi ya mwenye cheti na mwajiri. Watanzania bado ni waoga sana. Wangeitwa wakaonywa na kupewa adhabu ya kurudi darasani na kupewa mtihani kulingana na kazi wanazofanya, ilikuwa ni adhabu tosha. Sio kuwafukuza kazi.

Na waajiri pia wale waliofanya huo uharamia Kama bado wapo kazini wangepewa adhabu kulingana na kutokufuata maelekezo. Inawezekana wamepokea mlungula.

Ila tukumbuke tunachowaombea wenzitu kipo nyuma yetu. Tukumbukae Mdomo unaumba.

Waliokaa wakaona kunaumuhimu wa Hawa watu kulipwa sio wajinga.
 
Nadhani hukuelewa andiko langu......kughushi nyaraka ni kosa kwenye macho ya kisheria haijalishi ni nani amefanya hivyo.......kulipwa au kutokulipwa hakuondoi uharamu wa walichokifanya......
 
Nadhani hukuelewa andiko langu......kughushi nyaraka ni kosa kwenye macho ya kisheria haijalishi ni nani amefanya hivyo.......kulipwa au kutokulipwa hakuondoi uharamu wa walichokifanya......
Sawa sikatai ila kutokana na kuwa wengi halikuwa tatizo lao. Lilikuwa tatizo la mfumo. Anza kunyooshea mfumo uliowaajiri Kwanza ndiyo uwanyooshee wao. Wangekuwa making wakati wanaajiri Hawa watu wasingekuwepo. Sasa tuangalie na aliewaajiri anapewa adhabu gani kwa kumpotezea muda?

Hayo ni maoni yangu ninajiuliza rohoni. Sheria ile pande zote mbili.

Naomba serikali ikubali kuwa kulikuwa na makosa na iwe ni mwanzo na mwisho. Wafunge macho wawalipe stahiki zao Kama mama alivyoagiza.
 
Je mtu akikutapeli na akafanikiwa.....lakini baadae ukija kugundua kuwa alikutapeli ni nani kati yenu anayestahili adhabu.......??
 
Mtu anamdanganya mwajiri kuwa na sifa ambazo Hana ili apate ajira halafu analipwa??

Only in Tanzania,
 
Je mtu akikutapeli na akafanikiwa.....lakini baadae ukija kugundua kuwa alikutapeli ni nani kati yenu anayestahili adhabu.......??
Umeshasema mtu. Semea wengi. Halafu kuna ukaguzi au uhakiki. Kumbuka walikuwa hawahakikiwi na mtu mmoja ni watu wengi walikuwa wanakagua. Bado akafanyakazi miaka 40.

Ndiyo maana nikakuambia tatizo lilikuwa ni mfumo.
 
Kwa Nini Nyerere aliajiri waliokuwa wanajua kusoma na kuandika. Tujiulize je vyeti walivyotumia vilikuwa sahihi?

Na huu ugonjwa wa vyeti feki uliingia je hapa nchini?
 
MDOGO WANGU UNA ROHO MBAYA SANA HAO WATU WAKILIPWA UTAPUNGUKIWA NINI?
 
Mungu akubariki sana Mama,

Hili jambo lilikuwa ni ubatili mkubwa kwenye jamii yetu hebu fikiri mtu amefanya kazi zaidi ya miaka 30 amabakisha mwaka mmoja astaafu anafukuzwa kwa vyeti feki na stahiki zake zote anapoteza
Je ni kweli hawakufanya kazi hawa, wakati ki ukweli kuna watu tunawafahamu walikuwa wazuri sana kwenye kazi,
Kibaya zaidi mbona kuna wapendwa wengi tu na vyeti feki na bado waliendelea kufanya kazi
 
MDOGO WANGU UNA ROHO MBAYA SANA HAO WATU WAKILIPWA UTAPUNGUKIWA NINI?
Mbona mimi sijazuia mtu kulipwa ndugu.....mimi nimetoa tu maoni yangu kama ambavyo wengine wamechangia kulingana na maoni yao.....kumbuka huu ni mjadala unaohusisha mawazo tofauti tofauti......don't take it personal
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…