Rais Samia afanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri. Angellah Kairuki aenda TAMISEMI, Balozi Mulamula atemwa, Bashungwa ahamishwa

Rais Samia afanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri. Angellah Kairuki aenda TAMISEMI, Balozi Mulamula atemwa, Bashungwa ahamishwa

Mula mula kakosana na mama wapi tena

Huko TWEETER "Kigogo" kamwaga Habari kwamba Waziri kanunua Nyumba Marekani yenye Dhamani ya Dola 1.7M na kufanya Sherehe Siku 4 Mfululizo. Labda hili nalo limechangia Kumwagwa.
 
Bashungwa anatafutiwa sababu atemwe mazima
Hakuna kitu kama hicho Raisi akiamua anaweza kumtengea waziri yoyote muda wowote alijisikia bila kushauriana na mtu yoyote katiba imempa nguvu Raisi, ata leo anaweza kumteua Makonda kuwa mbunge na kumpa uwaziri au anaweza kunichagua mimi kuwa mkuu wa mkoa na hakuna atakaye hoji.
 
Kuteua na kutengua ni jadi yetu Tanzania.

MulaMula alikuwa anafuatilia sana swala la uraia pacha, nadhani hilo ni moja ya yaliyomponza ingawa yanaweza kuwapo mengine.
Mzee mkubwa hebu fafanua kidogo hapo kwenye uraia pacha.
Kuna siri gani mpaka serikali iogope huo mchakato kiasi cha kutimua waziri?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri Kama ifuatavyo:

Amemteua Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali Mhe. Dkt.Tax alikuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Aidha, Mhe. Tax anachukua nafasi ya Mhe. Balozi Liberata Mulamula.

Amemteua Mhe. Innocent Lugha Bashungwa kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Awali Mhe. Bashungwa alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Amemteua Angellah Jasmine Kairuki kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia amemteua kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Mawaziri wote hao walioteuliwa wataapishwa tarehe 03 Oktoba, 2022 saa 3:00 asubuhi Ikulu Jijini Dares Salaam.

View attachment 2375256
Haya mabadiko huwa yanafanywa sijawahi kuona chochote chamaana
 
Pongezi kwa wote walio endelea kubaki.

Jambo la msingi wafanye kazi kwa bidii na kwa maarifa.

Wasijisahau kuwa Mama hufoka kwa KALAMU.........

Chapeni kazi, tatueni kero za wananchi kwani utendaji kazi kwa nia ya dhati bila unafiki ndio utakao wabeba, unafiki na uzandiki hauwezi kuwasaidia.
 
Siku Mwigulu na Makamba aakiondoka nitampongeza Rais kwa kupiga kitimoto roast kilo mbili na Wind hoek bariiiid nne.

Hawa watu wamejaa kiburi na dharau huku utendaji wao ukiwa ni dhaifu, dhaifu mno sijui wamempa nini mama
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri Kama ifuatavyo:

Amemteua Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali Mhe. Dkt.Tax alikuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Aidha, Mhe. Tax anachukua nafasi ya Mhe. Balozi Liberata Mulamula.

Amemteua Mhe. Innocent Lugha Bashungwa kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Awali Mhe. Bashungwa alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Amemteua Angellah Jasmine Kairuki kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia amemteua kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Mawaziri wote hao walioteuliwa wataapishwa tarehe 03 Oktoba, 2022 saa 3:00 asubuhi Ikulu Jijini Dares Salaam.

View attachment 2375256
Badala ya kumtumia mwizi Mwigulu, anamtambua mwanamme mwenzake. Huenda Mulamula alikuwa hansifii kama wenzake
 
Back
Top Bottom