Rais Samia afanya uteuzi: Masauni aondolewa Wizara ya Mambo ya ndani, Kabudi apelekwa Wizara ya Habari na Michezo, Janabi kuwa mshauri wa Rais

kweli haijakaa vizuri..bora marufuku iwekwe kwenye katiba kabisa
 
Nawaza tu maana waliosikiliza Askari Magereza Walivyosikitikia Matendo ya Polisi kwamba waliwafuata na " mabunduki na Mabomu" kama majambazi, hawatashangaa Masauni kuhamishwa

Vinginevyo lingejengeka Bifu la kutisha
 
Huyu atatuulia Rais wetu,hivi kweli mh.Rais anywe maji asubuhi,ale mchana kidogo na usiku asile kitu anywe maji peke yake.....
Lucas Mwashambwa alitakiwa kuupinga huu uteuzi kwa nguvu zake zote. Maana Mama anaenda kushindia maji na viubwabwa kiduchu tu kila siku eti kwa lengo la kulinda afya!!

Hivi ilikuwaje adui wa chakula akateuliwa kwenye hiyo nafasi!!
 
Nawaza tu maana waliosikiliza Askari Magereza Walivyosikitikia Matendo ya Polisi kwamba waliwafuata na " mabunduki na Mabomu" kama majambazi, hawatashangaa Masauni kuhamishwa

Vinginevyo lingejengeka Bifu la kutisha
Hilo sakata ni la Mtwara ambapo alikamatwa askari Magereza akiendesha pikipiki bila helmet.... ndo mkasa mzima
 
Wewe Mzee Mgaya ndiyo hamna kitu kabisa!! Na hao wengine wamehamishwa sababu gani? Usikute mkeka ulishakuwepo kitambo tu! Halafu unatuletea visababu vyako visivyo na kichwa, wala miguu!
 
Isinge kuwa hii kuangaliana usoni, Masauni alitakiwa aende zake Zanzibar.
Huyu jamaa ame haribu sana jeshi la polisi.
Kila kitu simu ya maagizo.
Polisi hawakuwa waki fanya kazi zao kwa mujibu wa PGO bali kwa maagizo.
Rais ame chelewa sana kumuondoa huyu jamaa.
 
Kama uliamua kusoma ili uwe mwanasiasa juwa kabisa kuwa unaenda kuua kipaji chako,leo utamaduni,kesho sheria,kesho kutwa mambo ya nje,hapo hakuna kitu kabisa,utabakia tu kugangaa njaa ili familia yako iishi...
Hata Prof. Sarungi waliwahi mfanyia hivyo hivyo.

Mtaalmu wa mifupa, akala wizara ya michezo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…