Rais Samia afanya Uteuzi na Mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala na Kaimu Kamishna (TANAPA)

Hatimaye nimelamba Uteuzi 😁😁
 
Ngorongoro imefumuliwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiki ndio anchoweza KIZIMKAZI anatamani iwe kila wiki. Mm na family yangu pamoja na ukoo wangu tunaona ni Aibu tu. Mambo mazito analeta maneno tu mkeka hatoi. Pole kwa watanganyika
 
Siku hz wanatambulika kama Afisa tarafa
Kwenye taarifa hii kutoka Ikulu kuna sehemu imetaja 'Afisa tarafa' na sehemu nyingine 'katibu tarafa'.

Inamaana hata ikulu haielewi umuhimu wa kutambua cheo/nafasi ya Uongozi?
 
Si alisema ataki teuzi alipo panamtosha
 
Hivi kwanini lakini ndg yetu na kipenzi chetu Pascal Mayalla hawampi nafasi ktk teuzi zote hizi?!!

Mkuu Pascal Mayalla uliwafanya nini watu wa system? kwanini wanakunyanyapaa ndg yangu?
Mkuu Kisima , sijawahi kuwafanya kitu chochote, kinachofanyika kwenye vetting, kitu cha kwanza ni kufungua file lako, kitu wanachokutana nacho ni bandiko hili kuwahusu TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!, hata ungekuwa wewe, jina kama hili ungeli forward?.

Kwenye sehemu ya mwenendo wa maisha binafsi, wanakuta taarifa Pasco ni mtu wa viti virefu kwa mwendo wa Joni Mtembezi. Anapenda sana kula, Uliwahi kula vyakula gani kutoka sehemu mbalimbali Duniani ukafaidi? sijui chakula gani hajawahi kula!. Enzi akiwa kijana ni foleni mpaka Feri!, hata ungekuwa wewe, ungefowarward jina kama hili?.

Na wanapozidi kupekua file wanakutana na nyuzi kama hizi Pongezi Zangu ni Bonafide-Genuine! Sisaki Teuzi, Sitaki Teuzi, Niko Naye Mbeya, Nitamweza! wanafunga kabisa faili!.
Jifunze kuwa chawa.
Duh...!, mtu hajawahi kuwa chawa, sasa anelekea 60 ndio aanze kujifunza uchawa!
Badilika, jishushe na uchague kujipendekeza na kusifia.
Ukiwa sio kujipendekeza type ni kutojipendekeza, mimi niko down to earth, kosa langu ni mkweli too much na sijaweza kujigunza kunyamaza.
Ikiwezekana waone wazee wakutambikie. Halafu waganga nao wana nafasi yao
It's very unfortunately, I'm not a believer!
ktk safari yako ya kufukuzia teuzi.
Sijawahi kufukuzia teuzi!. Mfano sasa, macho yote ni 2025 watu wasio na jicho la 3, wanajua 2025 ni Mama, mtu anayefukuzia teuzi anaweza kupandisha bandiko kama hili Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke

Mimi hivi hivi nilivyo kwa capacity yangu kama mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, naweza kumsaidia sana Rais Samia na kulisaidia sana taifa letu bila position yoyote ya uteuzi!.

P
 
Kwa juhudi zako za huku unastahili sasa sijui kama unaifaa nchi au inafaa maslahi binafsi😆
Kuitumikia Nchi sio lazima uteuliwe japo ukiteuliwa ni vyema zaidi na maslahi ya Umma na ya binafsi yote yanatumikiwa Kwa pamoja🔥🔥

Kama bro Pascal
 
Huyo hamza anapelekwa ngorongoro kwenda kuwabeba waarabu na kuwafukuza wamasai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…