Rais Samia afanya Uteuzi na Mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala na Kaimu Kamishna (TANAPA)

Huyo alishavuka hizo level za uDC,yeye anapambania jimbo,japo wajumbe hawajaridhia
 
Kilasiku teuzi tu kwani hakuna kingine cha kufanya
 
Hii nchi kwa hapa tulipofikia, tunahitaji haraka Katiba Mpya iliyotokana na wananchi, kabla mambo hayajaharibika kabisa.
 
Pascal Mayalla yupo kwenye list ya wanaofanya vetting, au unataka ajiteue? Hiyo kazi ya kuwafanyia vetting wengine inamtosha sana...make ina marupurupu na takrima kibao kuliko hizo teuzi zenyewe.
 
kuna mapungufu kadhaa kwenye hiyo taarifa. mfano hakuna halmashauri ya Tanga Mjini bali Halmashauri ya Jiji la Tanga'
hakuna cheo cha Katibu Tarafa bali Afisa Tarafa
pia cheo cha DED (district Eecutive Director) hutumika kwa wakurugenzi wa halmashuri za wilaya tu. Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji, Manispaa na Jiji haitwi DED
 
Hizi teuzi za uDED naona sasa zinawaendea ma DAS......wakuu wengine wa idara kwenye halmashauri na kwingineko naona mambo yanazidi kuwadodea...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…