Pre GE2025 Rais Samia afunguka ya Moyoni: Kuna waliosema tuna Rais wa kuambiwa afanye na mwenye maamuzi ya Kitchen Party, hatuna Rais tuna House girl…

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kama anajiamini kiasi hicho ,kwanini amevuruga mchakato wa kuteua mgombea urais ndani ya chama chake na kujipendekeza mwenyewe?
Katiba imemruhusu kufanya vile kuanzia kwa Chama mpaka kwa Nchi !
Hata watakao kuja baada yake watafanya kama hivyo na hata zaidi ya hivyo !!

Katika maisha kila mtu anapendelea apate heshima na favour kwa baadhi ya mambo !
Kama kuna nafasi na ruhusa ya kuvipata vitu hivyo hakuna atakaye chagua kwenye ugumu wa kuvipata bali atachagua kwenye urahisi wa kuvipata !

Katiba mpya bora ni muhimu 🙏 !
 
Wayahudi hawakutaka kabisa kuhesabu wanawake na watoto, makabila yetu mengi wanaonwa kwa namna tofauti, dini zetu zingine zinawatenga kabisa wanawake. Hili jambo limetoka mbali mno, haliwezi kuondoka kirahisi.
Ndio linaondoka hivyo taratibu !
Hata Wayahudi wameongozwa na Mwanamke zaidi ya miaka kumi na mpaka amepiganisha vita vya waarabu na Israël vya mwaka 1967 !
Na akawa anasifiwa kwa kuitwa “ The Iron Lady “ 😳!

Margareth Thatcher naye huko Uingereza aliwaburuta wanaume kwa zaidi ya miaka 10 akiwa ni Waziri Mkuu !!
Akawa anaitwa ni Mwanamke wa shoka !
Mambo yanabadilika Ndugu !
Zamani huwezi kuona vijana wanatukana Wazee maana ilikuwa inaaminika kuwa ile ni laana kufanya vile , lakini kwa sasa kutukana Wazee inaitwa ni propaganda ya Chama ili kiendelee kuaminika na kuogopewa 😳🙄😱 !

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Farao wa kule Misri !
Dunia rangilangire 😳🙄!
 
Kifuani kwake kuna mengi hayasemi,
Huwa anadondosha moja moja
 
Kama kweli alitaka watu waamini tofauti na kwamba anaweza bila kuwezeshwa yaani hakuna mwanaume au wanaume nyuma yake wanaoamua nini afanye na nini asifanye angekubali kupambana na wengine kwenye mchakato wa kumteua ndani ya chama chake ili tuone.
 
Toka nchi hii imepata uhuru, lini kulikuwa na tume huru ya uçhaguzi? Kwanini mnata Samia ndo awe na tume tofauti na Marais wote waliopita? Huo ndio utaratibu wa tanganyika msimuonee mzanzibar.
 
Kumbe ndio maana waliamua kumpitisha juu kwa juu kuwa mgombea! Inaonekana kuna wahafidhina walikuwa wamejipanga kumuangusha Mama. Lakini hawaachi kusema kinafiki "Mitano tena kwa Mama"
 
Anaona kila kitu kipo sawa wanamdangana sana wasaidizi Wake
Wanaume waliomzunguka ndio wanatawala nchi sio yeye!! Anajilisha upepo tu, wenyewe wakina Kikwete wanamuamlisha mpaka kuteua watoto wao kwenye cabinet ingawa hawana uwezo!
 
Kizazi kikorofi
 
Sumu haijaribiwi kwa kuonjwa hata siku moja! Kule kwa jirani hawaelewi ni kimbunga au ni kitu gani kimeng'oa mwamba wa Nshara. Moyo wa mtu ni kichaka cha aina yake. Ile ilikuwa ni trial of democracy!
 
Kumbe ndio maana waliamua kumpitisha juu kwa juu kuwa mgombea! Inaonekana kuna wahafidhina walikuwa wamejipanga kumuangusha Mama. Lakini hawaachi kusema kinafiki "Mitano tena kwa Mama"
Iko vile na wanajua kabisa bila chembe ya shaka kwamba Mwenyekiti wa Chama ambaye pia ndiye Mkuu wa Nchi na ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi yote Nchini hakuna namna wao ndani ya Chama wanaweza kumbabaisha au kumtingisha 😅😅🤣🤣 !!
Kinachofuata ni wimbo wetu maarufu :- “Tuna imani na …………. Oya oyaaaa oyaaaa 😳👍🙌🙏 !

Katiba haijavunjwa kwahiyo wakae kwa kutulia ! 😳
 
Sasa haya yanatusaidia nini?

Watanzania tunalia na Utekaji, utesaji na Mauwaji ya kila leo.

Watanzania tunalia na Ufisadi ndani ya nchi, kukosekana kwa utawala bora haki na amani.

ATufanyie hayo tu Inatosha.

Kula tunajitafutia sisi wenyewe kula.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…