Rais Samia ahutubia mkutano wa tabia nchi, asema 30% ya pato la Taifa sio endelevu

Rais Samia ahutubia mkutano wa tabia nchi, asema 30% ya pato la Taifa sio endelevu

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo Rais wa Tanzania, Samia Suluhu amehutubia mkutano wa Tabia nchi unaofanyika Scotland, katika hotuba yake fupi na kuongelea Tanzania ilivyoathirika na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo kuongezeka kwa kina cha bahari na kutafuna ardhi yenye rutuba, kuyeyuka kwa barafu ya mlima Kilimanjaro pia kukumbwa na mafuriko na njaa visivyotabirika.

Kasema hayo yanaamaanisha 30% ya pato la taifa litokanalo na kilimo, uvuvi na misitu sio endeleevu.

 
Mama kang'aa haswaa[emoji16]
Screenshot_20211102-131535.jpg
 
Mama rekebisha kwanza nyumbani kwako, mstakabali wa taifa letu kisiasa si mzuri, taifa limegawanyika vipande vipande, huu haukuwa wosia wa baba wa taifa.
 
Nchi za dunia 3 walivyo wanakata miti, magari ya zamani yatozwa kodi ndogo ilihali ndio yanachafua mazingira, gesi wanapandisha bei, umeme nao tozo kila mwezi buku buku
 
Climate change ni agenda inayowapa mwanya mabeberu waendelee na mfumo wao wa kuziburuza nchi zinazoendelea na zile emerging economies kama China na India kwa kuweka masharti kibao yanayolenga kushusha kiwango cha uzalishaji kwa kisingizio cha carbon emission targets ili kudidimiza chumi zao....​
 
Sisitizo la Rais wa Tanzania kwa mkutano wa COP26: Tunapimwa kwa vitendo vyetu, si kwa ahadi kubwa kubwa tunazotoa

Nov 02, 2021 07:39 UTC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaeleza viongozi wa mataifa ya dunia wanaohudhuria mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP26 huko Glasgow, Scotland, kwamba mshikamano na juhudi zao kama viongozi katika kukabili mabadiliko ya tabianchi vitapimwa si kwa ahadi kubwa wanazotoa kwenye mkutano huo bali kwa jinsi watakavyotekeleza vipengele vyote vya mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi.

Rais Samia ametaja vipengele hivyo kuwa ni pamoja na kupunguza makali ya mabadiliko ya tabianchi, kuhimili mabadiliko hayo sambamba na uchangiaji wa fedha kulingana na kiwango cha changamoto zilizoko hivi sasa.

Rais wa Tanzania amefafanua kwa kusema ,“mabadiliko ya tabianchi ni suala la dunia nzima na hivyo majawabu yake ni lazima yawe ya kimataifa; na hivyo tunatoa wito kwa nchi zilizoendelea ambazo ndizo zinazoongoza kwa uchafuzi, zitekeleze kwa vitendo ahadi zao za kupunguza madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa kutoa fedha za kutosha kutuwezesha sisi nchi za kipato cha chini kufanikisha malengo yetu kwenye michango ya kitaifa ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa uendelevu.”

Katika sehemu nyingine ya hotuba yake, Samia amesisitiza kuwa, fedha za kutosha hususan kupitia misaada ya fedha itakuwa ni msingi katika mikakati ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Rais Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa COP26 Glasgow, Uskochi

Amesema nchi yake ya Tanzania na nyingine za kipato cha chini zimeandaa mipango ya kina ya NDCs ikiwa na mikakati dhahiri ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi.

Aidha ametahadhrisha kuwa bila kuchukuliwa hatua sasa tena kwa mshikamano, lengo la kuwa na kiwango cha joto katika nyuzi joto 1.5 katika kipimo cha selsiyasi litatoweka punde na halitafikiwa.

Viongozi kutoka nchi zaidi ya 100 duniani wanahudhuria mkutano huo wa 26 wa kujadili mabadiliko ya tabianchi, ulioanza tarehe 31 Oktoba na kuendelea hadi tarehe 12 ya mwezi huu wa Novemba mjini Glasgow, Uskochi.../

Tags
 
02 November 2021
Glasgow, Scotland

UN CLIMATE CHANGE CONFERENCE





The UN Climate Change Conference COP26

Overview :
The UN Climate Change Conference (COP 26) in Glasgow, United Kingdom is a crucial opportunity to achieve pivotal, transformational change in global climate policy and action.

It is a credibility test for global efforts to address climate change and it is where Parties must make considerable progress to reach consensus on issues they have been discussing for several years.

COP 26 comes against the background of widespread, rapid and intensifying climate change impacts, which are already impacting every region on Earth.

Also, COP 26 comes against the background of the COVID-19 pandemic, with the urgent need to build back better for present future generations to ensure a safe future. The UNFCCC secretariat (UN Climate Change) is the United Nations entity tasked with supporting the global response to the threat of climate change. UNFCCC stands for United Nations Framework Convention on Climate Change.

The Convention has near universal membership (197 Parties) and is the parent treaty of the 2015 Paris Agreement. The main aim of the Paris Agreement is to keep the global average temperature rise this century as close as possible to 1.5 degrees Celsius above pre-industrial levels. The UNFCCC is also the parent treaty of the 1997 Kyoto Protocol.

The ultimate objective of all three agreements under the UNFCCC is to stabilize greenhouse gas concentrations in the atmosphere at a level that will prevent dangerous human interference with the climate system, in a time frame which allows ecosystems to adapt naturally and enables sustainable development.
Source : UN Climate Change
 
Back
Top Bottom