Rais Samia aidhinisha zaidi ya billioni 39 kwa ajili ya miundombinu ya barabara Ilala

Jina lako linaonesha ulivyo hasara kwako na kwa familia yako, mbaya zaidi kwa taifa. Nisamehe kwa kufanya personal attack, but this was necessary
Nadhani kama Taifa,
Hakuna hasara yoyote Dr.Samia Suluhu Hassan kupitia serikali sikivu ya CCM kujenga barabara za lami nchi nzima πŸ’
 
It's there since mwalimu Nyerere
Tunanufaika na Kodi zetu kupata maendeleo

Nothing special, au Kwa upande wako unaona Jambo gani ni special?
Special zaidi ni kuhakikisha barabara za lami zinajengwa Dar es salaam na maeneo mengine nchini nzima. Na hayo ndio malengo na madhumuni ya serikali sikivu ya CCM chini ya kiongozi wetu makini na kipenzi cha wananchi wote Tanzania Dr.Samia Suluhu Hassan πŸ’
 
Nadhani kama Taifa,
Hakuna hasara yoyote Dr.Samia Suluhu Hassan kupitia serikali sikivu ya CCM kujenga barabara za lami nchi nzima πŸ’
Katika nchi ambayo viongozi wanasifiwa kwa serikali zao kujenga barabara katika karne hii ya 21 na kusahau availability, reliability na affordability ya huduma muhimu kwa ustawi wa watu kijamii na kiuchumi, hakika hilo bado litabakia kuwa taifa maskini zaidi duniani kuanzia umaskini wa akili, umaskini wa kipato na umaskini wa vitu (material properties) Kuwa na Zahanati ya kijiji ambayo hata mtendaji anaoopa kumpeleka mtoto wake sio zahanati ni jengo kama majengo mengine and so the roads kama gharama za usafirishaji zinapaa kila siku kutokana na kupaa kwa gharama za mafuta na gesi ni dhahiri kwamba watu hawawezi kuwa mobile na shughuli zao za kiuchumi ikiwemo bidhaa na huduma. Amka acha Tlaatah
 
Hii inchi ina Mataahira wengi kuliko Timamu na hii ndo shida, Jingine hili hapa...

Samia ana hela za kutoa kila siku kwajili ya umma?, afu zaid ya billioni 49 ndio shi ngapi sema kama ni 50 ueleweke yanini kukoleza mambo...?.

Tunajadili maendeleo wakati kodi zinaijenga simba na yanga kwa mgongo wa Goli la Mama Na Mataahira wanasherehekeaπŸ™„
 
Afu vile vikao vya bunge vya kuset bajeti ya Taifa huwa vinafaida gani kama pesa zinatolewa kiholela tu mtu akijisikia na atakapojisikia kupeleka, zile za kwenye Bajet ya kila Wizara zinaendaga wapi na hizi zinazotoka hovyo zinatoka wapi...?
 

Barabara tunalipia, ni mikopo, na sisi tunakatwa Kodi kwenye kila kitu Kwa ajili ya barabara

So hata kama inchi ingekuwa chini ya jeshi barabara zingejengwa tu
 
Barabara tunalipia, ni mikopo, na sisi tunakatwa Kodi kwenye kila kitu Kwa ajili ya barabara

So hata kama inchi ingekuwa chini ya jeshi barabara zingejengwa tu
Infact,
Barabara na huduma muhimu nyinginezo za kijamii ni kwaajili ya waTanzania wote kama ambavyo hata uhuru na haki ya kutoa maoni na mtazamo humu JF ni kwa waTanzania wote gentleman...

hakuna mbambamba yoyote kwenye hilo πŸ’
 
Badili, weka SERIKALI YAIDHINISHA.....hivi nyie CHAWA mnatumia ubongo au MBOJI??? kufikiri???πŸ˜…πŸ€”πŸ˜…πŸ€”
 
Infact,
Barabara na huduma muhimu nyinginezo za kijamii ni kwaajili ya waTanzania wote kama ambavyo hata uhuru na haki ya kutoa maoni na mtazamo humu JF ni kwa waTanzania wote gentleman...

hakuna mbambamba yoyote kwenye hilo πŸ’

Sasa umeeleweka na umeanza kujua majukumu ya serikali yako kwenye maisha yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…