Rais Samia aipandisha hadhi wilaya Rufiji kwenda kwenye hatua ya kuwa Mji

Rais Samia aipandisha hadhi wilaya Rufiji kwenda kwenye hatua ya kuwa Mji

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Rais Samia Suluhu Hassan siku ya leo ameidhinisha kupandishwa hadhi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji, na Halmashauri ya Mji wa Geita kuwa Manispaa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, alitoa taarifa hiyo leo, Disemba 13, 2024, wakati wa hotuba yake kwa wananchi wa Rufiji.

Tukio hilo lilifanyika katika uwanja wa Ujamaa, Ikwiriri, ambapo mamia ya wananchi walikusanyika kushuhudia uzinduzi wa Tamasha la Bibi Titi Mohamed.

"Bibi Titi Mohamed huko aliko atakuwa anafurahia sana maendeleo ya Rufiji maana ndiye Mbunge wa kwanza aliyeasisi jimbo hili alifanya kazi kubwa sana na mimi Mbunge wa tisa naendeleza kazi aliyoianza Hayati Bibi Titi na pia Mhe. Rais amefanya kazi kubwa kwa kuleta miradi mingi katika Wilaya yetu na sasa ameipandisha hadhi kuwa Halmashauri ya Mji." amesema Mchengerwa

Ameeleza kuwa Rufiji kuwa halmashauri ya mji kutawezesha ufadhili wa miradi mikubwa ya Benki ya Dunia, kuharakisha maendeleo, kujenga masoko, kuboresha huduma za afya, na kuimarisha sekta ya elimu.

Samia Rufiji.png

"Hivyo tunamshkuru Mhe. Rais kwa kuiona Rufiji na kuipa hadhi ya kuwa Mji na sasa maendeleo katika Wilaya hii katika nyanja zote yataenda kwa kasi zaidi." ameongeza Mchengerwa

Source: Jambo TV
 
Hivi Majukumu ya Msemaji mkuu wa Serikali ni yapi sasa...

Mbona Wanaingilia majukumu ya Msigwa kikazi.

Kumbe sasa Msigwa ni msemaji wa ATCL tu...tofauti na kurupa updates za ndege zetu hana kingine anacho tuhabarisha.
 
Wakuu,

Rais Samia Suluhu Hassan siku ya leo ameidhinisha kupandishwa hadhi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji, na Halmashauri ya Mji wa Geita kuwa Manispaa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, alitoa taarifa hiyo leo, Disemba 13, 2024, wakati wa hotuba yake kwa wananchi wa Rufiji.

Tukio hilo lilifanyika katika uwanja wa Ujamaa, Ikwiriri, ambapo mamia ya wananchi walikusanyika kushuhudia uzinduzi wa Tamasha la Bibi Titi Mohamed.

"Bibi Titi Mohamed huko aliko atakuwa anafurahia sana maendeleo ya Rufiji maana ndiye Mbunge wa kwanza aliyeasisi jimbo hili alifanya kazi kubwa sana na mimi Mbunge wa tisa naendeleza kazi aliyoianza Hayati Bibi Titi na pia Mhe. Rais amefanya kazi kubwa kwa kuleta miradi mingi katika Wilaya yetu na sasa ameipandisha hadhi kuwa Halmashauri ya Mji." amesema Mchengerwa

Ameeleza kuwa Rufiji kuwa halmashauri ya mji kutawezesha ufadhili wa miradi mikubwa ya Benki ya Dunia, kuharakisha maendeleo, kujenga masoko, kuboresha huduma za afya, na kuimarisha sekta ya elimu.


"Hivyo tunamshkuru Mhe. Rais kwa kuiona Rufiji na kuipa hadhi ya kuwa Mji na sasa maendeleo katika Wilaya hii katika nyanja zote yataenda kwa kasi zaidi." ameongeza Mchengerwa

Source: Jambo TV
Ni kwa mkwewe mohamed mchengerwa. Hovyoo kabisa. Keshobutasikia kizinkazi nao mji.
 
Back
Top Bottom