Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Rais Samia akataa mwananchi kueleza shida kwenye mkutano, amtaka amfikishie kupitia mbunge

Tatizo ni wasaidizi wa rais. Inakuwaje hawajutafuta hizo info mapema. Clip kama hizi zitammaliza rais Dkt Samia 2025. Maana kauli ka hiyo inaonesha ukaidi. Jamani hakika Dkt Samia anahujumiwa.
Anahujumiwa na nani? Alishasema mabango ya malalamiko hataki! Anataka mabango yale ",Unaupiga mwingi, Umeunganisha Taifa" na hataki ata kusikia wananchi wake wanasemaje! Ila kusaini mikataba ya ovyo na kuja kuitetea aaanhh hapo ndo pake.
 
Huwezi kuongoza nchi kubwa kama Tanzania kwa mfumo wa Rais kusikiliza matatizo binafsi ya watu nchi ikasonga mbele.

Wenzetu wanaojua maana ya Rais, waziri mbunge inapofanyika town Hall meeting watu wanauliza, wanatoa malalamiko yao mapendekezo kwa masuala ya mtaa, mji, jimbo au taifa. Sio malalimiko ya umenyang'anywa kiwanja na tajiri au umefukuzwa kazini ambayo ni masuala ya polisi na mahakama.
Halafu 2025 mnaanza kupita nyumba kwa nyumba kumwombea kura sio?
 
Rais Samia leo September akiwa Nangurukuru mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo kama shukrani ya kutimiza ahadi ya kufanyia kazi dukuduku lake na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

Wtf
 
Ili iweje? Rais hawezi kusikiliza kero za mtu mmoja mmoja, na hata akisikiliza hawezi kufanya maamuzi hapo kwa hapo, maana inawezekana huyo mwananchi akawa anapotosha pia. Kama yule mama wa Tanga alivyompotosha Magufuli
Subiri apotoshe ndipo useme amepotosha kusikilizwa ni lazima. Na mtu sahihi wa kusema atamletea alikuwa ni mkuu wa wilaya, mbunge anaweza asifikishe malalamiko kwa kwa rais kwani anajua 2025 sirudi tena bungeni ya nini kuangaika na hawa wananchi.
 
Pamoja na mazuri na mabaya ya the late JPM,
Tulipata rais wa aina yake na alikua raisi na mtetezi wa wanyonge.....

Magufuri alikulia maisha ya kimasikini masikini udogoni mpaka alikua anasemaga aliwai kuuza NTALALI NA NS'UNGWI na NFULU wasukuma wanaelewa......

Hata kuja kupatikana kama JPM yaan hakuwa anajitenga na watu alikua ni msikivu na katili sometimes.........

Najua hata nisipo kuja kua kiongozi au Rais wa JMT ila moyo wangu una amani sababu Kuna mtu ameishi maono yangu Mimi ni kama JPM tunafanana kwenye misimamo, kuongoza, udikteta, kusimamia nacho amini...

JPM nilitofautiana nae kwenye mengi kimtazamo sometimes ila namkubali sana Huyu BABA angu mdogo JPM

RIP JPM
 
Huwezi kuongoza nchi kubwa kama Tanzania kwa mfumo wa Rais kusikiliza matatizo binafsi ya watu nchi ikasonga mbele.

Wenzetu wanaojua maana ya Rais, waziri mbunge inapofanyika town Hall meeting watu wanauliza, wanatoa malalamiko yao mapendekezo kwa masuala ya mtaa, mji, jimbo au taifa. Sio malalimiko ya umenyang'anywa kiwanja na tajiri au umefukuzwa kazini ambayo ni masuala ya polisi na mahakama.
Akili ndogo sana hii
 
Tatizo ni wasaidizi wa rais. Inakuwaje hawajutafuta hizo info mapema. Clip kama hizi zitammaliza rais Dkt Samia 2025. Maana kauli ka hiyo inaonesha ukaidi. Jamani hakika Dkt Samia anahujumiwa.
Anajihujumu.
Angesikiliza kisha maamuzi yangetolewa baadae. Hii ingeonesha anajali.
 
Anahujumiwa na nani? Alishasema mabango ya malalamiko hataki! Anataka mabango yale ",Unaupiga mwingi, Umeunganisha Taifa" na hataki ata kusikia wananchi wake wanasemaje! Ila kusaini mikataba ya ovyo na kuja kuitetea aaanhh hapo ndo pake.
Kuna wakati mambo haya yanatia kichefu chefu.
Unatia saini mkataba wa hovyo pili unatoa pesa mkataba ukatetewe kumbafu sana
 
Amesimama kuwasalimia wananchi
Sasa pale kasimama kufanya nini!?....kama anajua Mbunge yupo, why bother kusimama barabarani kusikiliza kero za wananchi?...mimi naamini kuna wananchi wameshazunguka ngazi za chini na hawapati msaada, Kiongozi wa nchi akisikiliza hizo special cases,anaweza kutoa msukumo mwananch asaidiwe.
,malalamiko na shida zao zina mifumo yake ya kupokelewa.
 
Tatizo walijazwa upepo na yule mwigizaji au bwana yule
Yule mhuni alikuwa comedian pro max. Alikuwa anaandaa wauliza maswali na anakuwa ameandaa script ya namna ya kutatua "changamoto" fake anayopewa.

Kuthibitisha hili, angalia majibu ya mhuni huyu alipokuwa anakutana na changamoto halisi. Mfano pale Mbezi stendi kuna mwananchi alilalamikia gharama kubwa ya kulipia choo (sh 500/=). Mhuni alimfurishia matusi mwananchi yule mbele ya kamera huku TV zote zikiwa live. Alisema "kama unaona kubwa beba mavi yako peleka nyumbani".

Kuna pahala pengine (sikumbuki ni wapi). Aliamuru mwananchi awekwe ndani baada ya jiwe kutwangwa na changamoto ngumu.

Jiwe alikuwa siyo mtu. Afe tena huko aliko.
 
Rais Samia leo September akiwa mkoani Mtwara alisimamisha msafara wake kuongea na wananchi wa eneo hilo. Moja wananchi hao aliomba kuongea jambo ambapo Rais alimwambia mambo ni mengi na Tanzania ni kubwa.

Rais Samia alimtaka mwananchi huyo ampatie jambo lake mbunge kisha amfikishie Rais au wasaidizi wake.

Mwaka 2017 Rais Magufuli akiwa anaelekea Mtwara alisimamishwa Somanga na mwananchi aliyeelezea changamoto ya zahanati katika eneo hilo kutokamilika kwa miaka mingi. Rais Magufuli alichangia na kuamrisha ikamilike.

Alipopita tena barabara hiyo miaka 3 baadae mwananchi huyo alimzawadia jogoo kama shukrani ya kutimiza ahadi ya kufanyia kazi dukuduku lake na Magufuli alimsubiri mpaka alipomkamatia na kumpa. Alipofariki, mwananchi huyo alifunga safari kumzika Rais Magufuli mwaka 2021.

Rais hajatokana na kura za wananchi ili kuwa rais hivyo hawezi kujua shida za wananchi zikoje.
 
Anasimama barabarani kusalimia, au kutoa majibu ya matatizo aliyopewa na kuhusu hilo eneo na mbunge wao... Ndio maana ya representative democracy
Kama ni hivyo huyo mbunge si ndio angepeleka hayo majibu? Au ni mambo ya kujimix?
 
Pamoja na mazuri na mabaya ya the late JPM,
Tulipata rais wa aina yake na alikua raisi na mtetezi wa wanyonge.....

Magufuri alikulia maisha ya kimasikini masikini udogoni mpaka alikua anasemaga aliwai kuuza NTALALI NA NS'UNGWI na NFULU wasukuma wanaelewa......

Hata kuja kupatikana kama JPM yaan hakuwa anajitenga na watu alikua ni msikivu na katili sometimes.........

Najua hata nisipo kuja kua kiongozi au Rais wa JMT ila moyo wangu una amani sababu Kuna mtu ameishi maono yangu Mimi ni kama JPM tunafanana kwenye misimamo, kuongoza, udikteta, kusimamia nacho amini...

JPM nilitofautiana nae kwenye mengi kimtazamo sometimes ila namkubali sana Huyu BABA angu mdogo JPM

RIP JPM
Umechanganyikiwa
 
Dalili za moyo kukata tamaa.

Hivi wale wazee wa ule moshi wa wakati ule ni kweli wote walikimbilia malawi?
 
Back
Top Bottom