Rais Samia akiri kuwepo upungufu wa umeme, Makamba alisema ni 'scheduled maintainance'

Rais Samia akiri kuwepo upungufu wa umeme, Makamba alisema ni 'scheduled maintainance'

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Rais Samia akiwa mkoani Mwanza amesema anatambua uwepo wa upungufu wa umeme ikimaanisha vyanzo vilivyopo havikidhi mahitaji yaliyopo. Waziri wetu wa nishati aliliongelea suala la kukatikatika kwa umeme chanzo chake ni marekebisho ya mfumo wa zamani.

Tunaandaliwa kwa umeme wa dharura?


Symbion.jpg
 
Huwa nasikitika Sana wanapolaumiwa wachezaji football wa Tanzania kuwa hawajui au hawapo serious pale timu yetu ya taifa inapofanya vibaya. Vijana hawa hulaumiwa sababu kazi yao hufanyikia hadharani ambapo na mashabiki hualikwa kushuhudia matokeo ya kazi yao.

Naamini kama na watendaji wa ofisi za umma wangekuwa wanafanyia kazi zao za kitaalam ktk majukwaa ya wazi na si ktk vi ofisi tena vyenye mafaili yaliyoandikwa SIRI wallah Watanzania tungeitisha mjadala wa kitaifa kutafuta suluhu ya matatizo ya uwajibikaji kati yetu. Serikalini kuna watendaji wabovu zaidi ya hawa wacheza football tunao watukana kila uchao.

Ni watendaji hawahawa wameshindwa kutengeneza miundombinu ya kuandaa wachezaji watetezi wa taifa wa kesho. Badala yake huishia kufanya mipango ya zimamoto kutaka matokeo ambayo wenzetu wamewekeza akili, maarifa, pesa na utaalam kuyapata.
 
Hali si hali, mabwawa maji hamna umeme mgao ni mkali hivyo serikali iwashe mitambo iliyotufilisi hapo awali, mitambo ya Mafuta mazito, pia waziri mkuu awajibike
 
Makamba: Hakuna mgao wa umeme bali ni matengenezo ya kawaida.

Samia: Kuna upungufu mkubwa kwenye vyanzo vya maji hali inayopelekea mgao wa umeme na maji kutoepukika.

Tumwamini nani kati ya mkuu wa Nchi na Waziri wake?!

Juzi niliuliza humu hivi Makamba anatufanya sisi ni mapunguani na hadi muda huu anasubiri nini ofisini?!
 
Rais Samia akiwa mkoani Mwanza amesema anatambua uwepo wa upungufu wa umeme ikimaanisha vyanzo vilivyopo havikidhi mahitaji yaliyopo. Waziri wetu wa nishati aliliongelea suala la kukatikatika kwa umeme chanzo chake ni marekebisho ya mfumo wa zamani.

Tunaandaliwa kwa umeme wa dharura?
Rais anasema kuna upungufu wa umeme, Waziri Mkuu anaita Wawekezaji waje kwa wingi kwani umeme upo wa kutosha, Waziri wa Nishati anasema kukatika kwa umeme ni sababu ya Scheduled Maintenance tena akilaumu hapakuwa na Preventive Maintenance ktk mitambo yetu ya kuzalisha umeme akiulenga utawala wa JPM.

Mwanza kuna Ziwa Victoria lkn kuna tatizo kubwa la upatikanaji wa maji lkn Rais anaongelea tatizo la maji kwa Dar hafusii Mwanza. Hapa Watanzania tumepigwa ndo maana Rais kwa huko Mwanza hapendwi hata na mtoto mdogo
 
Umeme wa maji ni wa hovyo na bado Jiwe akatumbukiza mahela kibao kwenye tatizo lile lile.
Mabadiliko tabia nchi acha kabisa, ukitaka kulijua hilo vizuri njoo uone huo mto huko kwenye bwala la Nyerere kamebaki kamchirizi tu katikati hata likiisha bado tunaweza kuishia kwenye mgao tu.
 
Back
Top Bottom