Rais Samia akiwaapisha Mawaziri wateule Ikulu, Dar es salam leo Oktoba 3, 2022

Rais Samia akiwaapisha Mawaziri wateule Ikulu, Dar es salam leo Oktoba 3, 2022

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwaapisha Mawaziri wateule Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 03 Oktoba, 2022



Nawapongeza kwa walio hapa. Mhe. Angela siyo mgeni kwenye kazi hii, umejifunza mengi ukiwa nje. Nimeona uje unisaidie. TAMISEMI ni ileile uliyoiacha.

Katika viapo tunaapa kulinda na kutetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kile kiapo ni chenu. Ni katiba ya JMT, Muungano wenye pande mbili, na mtatumika sehemu zote sawa kwa jinsi katiba ilivyogawa majukumu.

Mnapaswa kujua mipaka kwamba nchi hii ina Mamlaka, na mamlaka uliyowekewa ina mipaka yake, unapotaka kuvuka lazima upate ruhusa ya Mamlaka ya Juu. Sasa kujua mipaka yenu wakati mnafanya kazi, kwenda juu lakini pia kushuka chini, lazima mjue.

Tunzeni siri, aidha imesemwa kwenye Baraza la Mapinduzi, aidha umeitwa ukaelezwa, hiyo ni siri. Unapotaka kuisema, au kuifanyia kazi ujue jinsi ya kuitumia hiyo siri. Linaloamuriwa na Serikali ni lako, lazima ulibebe na ulifanyie kazi kwa misingi ile uliyoelekezwa. Huwezi kusema nilielekezwa hivi, mimi sikutaka hivi lakini imebidi nifanye hivi kwa sababu nimeelekezwa, huwezi kujitoa.

Mnapaswa kuheshimu Katiba, kujua mipaka na kutunza siri.
 
Kuna kaduara fulani kadogo kanachotumika kutuletea wateuliwa wapya kwenye kila eneo, mteuaji huwa hapati shida kuumiza kichwa, anatazama palepale bila kujali mteuliwa aliwahi kuwa asset au liability.
Naona kama tunashida kubwa kwenye vetting.

Watu hawajiishughuliishi kutengeneza viongozi wanazunguka na walewale kuendellea ni ngumu bila mawazo mapya
 
Tutajua tu ni kua na subira... kwamba. Je mulamula alipewa maelekezo gani ambayo binafsi hakubaliani ila anatekeleza tu kwa kua ni maelekezo ya mkuu na akaropoka ikawa sio siri.

Kwa jinsi mama kaeleza kwa mfumo wa kijembe ndio picha maamuma tunapata huku mtaani.

Kama ni jambo la maslahi kwa umma kafanya mulamula tutajua uzalendo wake siku moja ijayo. Kama ni utovu wa nidhamu tutakuja jua tu. Nchi hii ina kina kigogo tutajua tu kwa nini mwanamama rais wetu kamtema mwenzake.

Hakika mama rais wetu aliongea kwa donge na kapiga kijembe cha juu kama kawaida yake.
 
Itakuwa kuna vitu kavisema ama kuvifanya huko Marekani alipohudhuria mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNGA) ambavyo havijamfurahisha Bi Mkubwa
 
Itakuwa kuna vitu kavisema ama kuvifanya huko Marekani alipohudhuria mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNGA) ambavyo havijamfurahisha Bi Mkubwa
Inawezeka na kigogo kapost eti kanunua mjumba wa usd 1.5 na kufanya sherehe na familia yake. Lipi ni lipi tutapata uhakika tu.
 
Inaonekana Tanzaia ikiwa na watu takribani Mil.60 bado hatupati watu wazuri wa kuendesha Wizara zetu.

Bado tuna -'recycle' tu sijui kwa nini.. Kama hatuta badilika basi nchi kuendelea itachukua muda mrefu sana..
Tatizo hamjui kwamba kuteua mawaziri wapya ni kuongeza mzigo kwa serikali.
 
Tutajua tu ni kua na subira... kwamba. Je mulamula alipewa maelekezo gani ambayo binafsi hakubaliani ila anatekeleza tu kwa kua ni maelekezo ya mkuu na akaropoka ikawa sio siri...
Mbona mnaongea kwa mafumbo.

Hapa JF bwana, mtambo wa kuweka mambo uwazi.
 
Tatizo hamjui kwamba kuteua mawaziri wapya ni kuongeza mzigo kwa serikali.
Mzigo kivipi mkuu wakati waziri mulamula katumbuliwa lazima akabidhi gar na nyumba na ulinzi na sina uhakika kama atalipwa fao ya uwaziri
 
Tutajua tu ni kua na subira... kwamba. Je mulamula alipewa maelekezo gani ambayo binafsi hakubaliani ila anatekeleza tu kwa kua ni maelekezo ya mkuu na akaropoka ikawa sio siri.

Kwa jinsi mama kaeleza kwa mfumo wa kijembe ndio picha maamuma tunapata huku mtaani.

Kama ni jambo la maslahi kwa umma kafanya mulamula tutajua uzalendo wake siku moja ijayo. Kama ni utovu wa nidhamu tutakuja jua tu. Nchi hii ina kina kigogo tutajua tu kwa nini mwanamama rais wetu kamtema mwenzake.

Hakika mama rais wetu aliongea kwa donge na kapiga kijembe cha juu kama kawaida yake.
Linaihusu Zanzibar. Cheki muungano umerudiwa kwa msisitizo na baraza la mapinduzi pia limetamkwa. Hakuna waziri wa muungano anaingia kwenye baraza la Mapinduzi. Kuna jambo hapo Watanganyika
 
Madam president ameweka bayana kila kitu ila kiutu uzima
Kazi iendelee
 
Back
Top Bottom