Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo mfanyabiashara Alhaj Aliko Dangote

Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo mfanyabiashara Alhaj Aliko Dangote

Nadhani hi sasa ndio kazi ya serikali kuhakikisha wafanyabaishara nao wanafuata sheria; kama kuna loop holes, mfanyabaishara atazitumia, kwanini EWURA, TCRA nk vilianzishwa? Kazi yake ni ku regulate mambo ya sekta husika. wizara ya kazi na vijana na hasa kitengo cha kazi (of course na vyama vya wafanyakazi, in this case ni TAMICO ) ndio kazi zao hizi, wasikae tu ofisini, watembee kwa waajiri na kwenda kuwatia moyo, kuwarekebisha, kuwashauri na hata kutumia nguvu ili wao wafuate sheria. Hapa sasa ndio tutamuelewa profesa Asad alivyokua kule USA kwenye ile interview iliomletea matatizo na watawal pamoja na bwana Ndugai (naogopa kulihusisha bunge hapa ), jamaa alishauri kwamba, Africa tunawekeza kwenye strong personalities badala ya kuwekeza kwenye strong institutions, hi ndio mahala pake.
I agree
 
Afadhali,, cement itashuka bei, maana walimfanyia figisu mwanzoni, wakati ule cement ya dangote imeshamili mtaani, tulinunua mfuko wa saruji hadi Tsh 10,000 kutoka 15000.

Dikteta alimfanyia figisu za kutisha.
Hilo jina dikteta utalitapika siku...waulize Libya kinachowakuta sasa hv.... nao walisema Gaddafi ni dikteta
 
Hilo jina dikteta utalitapika siku...waulize Libya kinachowakuta sasa hv.... nao walisema Gaddafi ni dikteta
Haitatokea kumkumbuka magufuli, ila atakumbukwa ni dikteta wa kwanza kutokea Tanzania,

Na kwa upande wa ccm washajifunza, nimeambiwa kwenye katiba ya Ccm wanataka kuweka kipengele cha waomba kuteuliwa wawe wanapimwa afya ya akili
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassani amekutana na kufanya mazungumzo na Mfanyabiashara maarufu kutokea Nigeria Alhaji Aliko Dangote

Mazungumzo hayo muhimu yalifanyika leo Mei 24, 2021 Ikulu Jijini Dar es salaam

Alhaji Dangote ni mfanyabiashara mkubwa duniani aliyewekeza nchini Tanzania kwenye sekta mbalimbali ikiwemo Kiwanda cha kuzalisha Saruji Mkoani Mtwara

Alhaji Dangote amemshukuru sana Rais Samia kws kuboresha mazingira ya Uwekezaji nchini na ameahidi kuwa ataendelea kuwekeza Tanzania kwenye maeneo tofauti ikiwamo ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea

Rais Samia aliahidi kuwa Serikali yake itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini kwa faida ya pande zote na alwaagiza Mawaziri husika kushughulikia changamoto zinazoikabili Kampuni ya Dangote

Taarifa zaidi kutolewa na Mamlaka husika

Kazi Iendelee
Kwenye barakoa ndipo sijaelewa, wakiwasilisha wawili wamevaa barakoa, kwenye kundi la kupinga picha hawajavaa barakoa.
Only in Africa.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Haitatokea kumkumbuka magufuli, ila atakumbukwa ni dikteta wa kwanza kutokea Tanzania,

Na kwa upande wa ccm washajifunza, nimeambiwa kwenye katiba ya Ccm wanataka kuweka kipengele cha waomba kuteuliwa wawe wanapimwa afya ya akili
Shida za watu kama wewe ni ukabila tu ndo unakusumbua. Nakumbuka uchangiaji wako, umekuwa ni wa mlengo wa kikabila tu! Subili siku urais utakapoangukia kwenu.
 
Haitatokea kumkumbuka magufuli, ila atakumbukwa ni dikteta wa kwanza kutokea Tanzania,

Na kwa upande wa ccm washajifunza, nimeambiwa kwenye katiba ya Ccm wanataka kuweka kipengele cha waomba kuteuliwa wawe wanapimwa afya ya akili
Haitatokea kumkumbuka Magufuli....kwako sio kwangu na wengine wote waliomuelewa...

Km kuwabana watu wasitafune hii nchi ni ugonjwa wa akili basi CCM watupe vichaa maana ndio tunawahitaji..

CCM wapime raisi ambae anauchungu wa hii nchi na anatambua km hii nchi ni ya wakulima na wafanyakazi ambao ni maskini...na infact ingependeza zaidi wangetupatia kiongozi mwenye background ya ukulima...mabraza meni waliosoma mjini baadae wakapelekwa nje na baba zao hatuwataki maana hao hawaijui nchi hawajui umaskini tulionao vijijini...watakaa kuwaza wazungu/wawekezaji ndio watatukumboa...wengine tumesomeshwa na mifugo mpaka sasa tunapumua kwa mifugo huyo mzungu tunamsikia radioni tu..

Nasikia tuna madini ila mpaka leo mkulima trekta ni anasa...anakuja kiongozi anatuambia tunaibiwa tujenge ukuta tulinde madini yetu anaitwa dikteta..hv tumelogwa
 
Sasa Dangote anasema kaja kumsapoti Samia Suluhu. Unatafuta hela unajifanya umekuja kumsapoti Rais wa Tanzania. Nenda kamsapoti Muhammad Buhari huko kwenu anahitaji sapoti! Unamsapoti Rais wa Tanzania wewe nani kwa Watanzania kujifanya unajali ?????

Serikali hii nayo inayopelekeshwa na busara za Kikwete inasema itahakikisha inamlinda Dangote na kumwondolea kero zote.

Why Dangote ? Kwa nini isilinde wenye boda boda imlinde Dangote ? Kwa nini isiondoe kero za ushuru wa wavuvi badala ya Dangote ???

KWA NINI Dangote anahitaji kulindwa kuliko wachuuza korosho wa Nachingwea au wauza spea wa Shaurimoyo ?????

Kwa nyongeza: tuna viwanda vikubwa vya Saruji km Twiga, Tanga na Mbeya. Nasubiri kama navyo vitalindwa kwa nguvu ile ile au vitaachwa vimezwe na Dangote!
 
Shida za watu kama wewe ni ukabila tu ndo unakusumbua. Nakumbuka uchangiaji wako, umekuwa ni wa mlengo wa kikabila tu! Subili siku urais utakapoangukia kwenu.
Tanzania ya leo inao wapuuzi wengi sana haswa mitandaoni wanaowasakama sana wasukuma, kama vile ni watu fulani wachache sana.

Tushukuru Mungu msingi wetu ni umoja, vinginevyo wasukuma kama wangekuwa ni watu wajeuri siku nyingi sana wangeshaiharibu hii amani tunayojivunia.

Ni hulka mbovu sana kuwasakama wasukuma kama vile ni watu fulani wasio na hisia zozote. Kuna watu wanaiombea nchi hii kila wakati ndio maana inaweza kuvipita vipindi vingi vya hatari.
 
Mkuu mbona hakuna chuki ni ushauri tu! angalia Pinda alikuja na sera ya kilimo kwanza iko wapi? mwendazake viwanda vikowapi? mama hata halijulikani anasimamia nini? miradi kibao ilianzishwa Chato toka mwendazake ameondoka kuna mtu anataja Chato tena? tuwe na mikakati/sera ambayo kila mtawala akija iwe ni kuisimamia na siyo kuja na sera zake, JK ilikuwa bandari ya Bagamoyo na gesi ya Mtwara sasa hakuna hata mtu anaviongolea.

Nakubaliana na wewe kwa kuwa mikakati ya Serikali ya utekelezaji wa Ilani ya Chama chake, km Kilimo kwanza, usimamizi wake umekuwa ya kudodora. Ili kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo (Development Vision) 2025, ni dhahiri tunahitaji Kiongozi jasiri, anayethubutu kufanya maamuzi magumu, na mwenye Utashi wa Kisiasa.

Kwangu mimi, ukiacha Baba wa Taifa ambaye pamoja na mengi aliyofanikisha, alijenga utaifa kupitia Siasa ya Ujamaa na kujitegemea (Azimio la Arusha), ni Hayati Magufuli. Hayati Magufuli pamoja na mapungufu makubwa katika kukuza demokrasia, alifanya na kusimamia maamuzi magumu ya kujenga Taifa linalojitegemea. Wakati Hayati Mkapa yeye alijikita kwenye Utawala bora.

Kuhusu swali lako mama hata halijulikani anasimamia nini? jibu yawezekana ikawa ni kubomoa misingi ya "Taifa la kujitegemea" iliyowekwa na mtangulizi wake kama ambavyo wafuasi wa Baba wa Taifa na Hayati Mkapa walivyobomoa misingi yao (Azimio la Arusha na Utawala Bora).
 
Investment inahitaj mazingira wezeshi na support kutoka serikali husika, huez ku investment kwa kutegemea figusu.
Ni kweli uwekezaji unahitaji mazingira rafiki ya kijumla siyo ya kibaguzi. Mazingira ya uwekezaji kwa mwananchi ni magumu sana kuanzia kupata ardhi, leseni hadi mikopo ya mitaji.

Kwa hali inavyoonekana na kuelekea, wananchi wataendelea kuwa wajiriwa kwenye nchi yao yenye fursa nyingi za uwekezaji katika Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Viwanda, Madini, na Utalii. Hata sekta ya Sanaa na Mziki ambayo imevamiwa na vijana wengi, mazingira ya uwekezaji nayo si rafiki kwa wawekezaji wa ndani.
 
Waziri wa Mambo ya Nje ya Saudia Arabia Mwana wa mfalme Mhe. Faisal Bin Farhan Al Saud azungumza leo Ikulu Dar es Salaam Tanzania kuhusu uwekezaji na mahusiano baina ya nchi hizi mbili:



25 May 2021
Dar - es Salaam, Tanzania

Tanzanian President Samia Suluhu Hassan receives Saudi Arabia’s Foreign Minister Prince Faisal bin Farhan.



Source : michuzi tv
 
Madereva wake wameajiriwa kama contractors badala ya kupewa full time employment, hilo linawakosesha haki zao za kisheria nyingi ikiwemo uhakika wa kazi zao, kuingizwa kwenye pension schemes, kwenda likizo ya malipo, sick pay na faida wanazopewa wafanyakazi wenzao; bila ya kusahau kupoteza PAYE za TRA.

Hayo ndio mambo ya kumkubusha na yeye. Juzi tu madereva wa Dangote walikuwa kwenye mgomo kisa kuchukuliwa kama vibarua wakati watu wanafanya kazi sehemu moja zaidi ya miaka miwili, hakuna madereva wenye mkataba wa kudumu na kampuni; kuna middleman anaewapa ajira na kuwapunja kwa kuwakata kilicho chao, bila ya ulazima.

Wafanyabiashara sio kuja kuomba mazingira mazuri tu, bali na wao waweke mazingira mazuri kwa waajiriwa, sakata lote la mgomo limeenda karibu week nzima Mhagama kama alikuwa aoni vile na nina uhakika wale madereva madai yao ya msingi ayajatatuliwa.
Wewe umeajiri wangapi unadhani ni rais hivyo wakati kipindi cha mwendazake kufanya biashara? wengi walikimbia na hata Dangote alisema ni vigumu kufanya biashara Tanzania
 
Unaota ww unadhan huyu ni ngichiro kama ww
Hivi Kwa nini hawa wafanya biashara wakubwa huwa wanakaa kudekadeka saana!!!

Huyu jamaa anaongoza Kwa kudeka, haishiwi kulalama kama litoto Fulani hivi, Mo, na Bakhlesa, sjawahi kuona wakideka hivyo
 
Sema Dangote naye ni mtu asiweza kabisa figisu. Biashara zake nyingi ustawi wake unategemea sana kulelewa na serikali. Hata Nigeria iko hivyo.

Ingawa ndio kazi ya serikali kulea sekta binafsi lakini ukipata mtawala roho mbaya kama Magu mambo yanayumba sana.
Je, mwekezaji anaweza kwenda kufanya figisu kwenye nchi ya kigeni? Si ataswaga fasta!
 
Nakubaliana na wewe kwa kuwa mikakati ya Serikali ya utekelezaji wa Ilani ya Chama chake, km Kilimo kwanza, usimamizi wake umekuwa ya kudodora. Ili kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo (Development Vision) 2025, ni dhahiri tunahitaji Kiongozi jasiri, anayethubutu kufanya maamuzi magumu, na mwenye Utashi wa Kisiasa.

Kwangu mimi, ukiacha Baba wa Taifa ambaye pamoja na mengi aliyofanikisha, alijenga utaifa kupitia Siasa ya Ujamaa na kujitegemea (Azimio la Arusha), ni Hayati Magufuli. Hayati Magufuli pamoja na mapungufu makubwa katika kukuza demokrasia, alifanya na kusimamia maamuzi magumu ya kujenga Taifa linalojitegemea. Wakati Hayati Mkapa yeye alijikita kwenye Utawala bora.

Kuhusu swali lako mama hata halijulikani anasimamia nini? jibu yawezekana ikawa ni kubomoa misingi ya "Taifa la kujitegemea" iliyowekwa na mtangulizi wake kama ambavyo wafuasi wa Baba wa Taifa na Hayati Mkapa walivyobomoa misingi yao (Azimio la Arusha na Utawala Bora).
Sawa
 
Unaota ww unadhan huyu ni ngichiro kama ww
Mkuu, nataka kukuuliza, unadhani Lugha ya kuudhi kiasi hiki imewahi kukusaidia chochote...! Je, unadhani unaowaambia maneno hayo, bila kujali mchango wao hawakutoa tusi wala Neno la kuudhi, halafu wewe unakuja kuwatusi maneno ya kuudhi, kwani wao hawafahamu kutokwa maneno hayo?

Mkuu, jiheshimu basi ili uheshimiwe...!
 
Pamoja na mapungufu yake kama binadamu sote tulivyo, lakini tukubali kwa kauli moja kwamba Dk. Magufuli hakuwa binadamu wa kawaida kimaono, kiutendaji kazi na ufatiliaji wa karibu.

Baadhi ya watu wanajaribu kumsema mambo mengi mabaya Magufuli walwatu,lakini nawakumbusha kwa mara nyingine tena kwamba hakuna Rais yeyote Tanzania pamoja na barani Afrika ambaye aliwahi kuwa mbunifu na muona mbali kama Magufuli - miradi yote mikubwa ya kimkakati inayo endelea hapa Tanzania mwanzilishi wake si mwingine bali Magufuli - ndani ya utawala wake mfupi wa miaka mitano amebuni na kutekeleza miradi mikubwa mikubwa ambayo kwa akili za kawaida uwezi kui-comprehend hata kidogo - halafu watu wenye akili za ajabu wana beza beza miradi na maendeleo yaliyo letwa na mzalendo wa kweli wa Taifa hili.

Wengi wanao mchukulia Magufuli for a ride wanashindwa mpaka na Umoja wa mataifa ambao ulimuenzi wakati alipo aga Duniani kwa kutambuwa sana mchango wake wa kuwaletea maendele binadamu wenzake specifically Tanzanians - kila mara Magufuli alikuwa anatukumbusha kwamba tutakuja kumkubuka - na kweli!! Bottom line ni kwamba: tunapo mlahumu the late Dk. Magufuli tujifunze kubakiza hakiba ya maneno.

Kitu kingine ambacho huwa akina ukweli wowote ni hiki cha kudai eti ukoo wa Magufuli hauna asili ya Tanzania - huu ni uzushi husiokuwa na kichwa wala miguu - ukweli wa mambo ni kwamba kabila la Magufuli ni Mzinza, sio Msukuma mama yake ndio Msukuma na Magufuli alikuwa fluent kwenye lugha ya Kisukuma kutokana na mama yake kuwa Msukuma, kabila la Kizinza has nothing in common na kabila la Kisukuma, mila za Kizinza zinarandana zaidi na mila za Kihaya, hata lugha ya Kizinza haina tofauti sana na lugha ya Kihaya.
Hayati Magufuli ni mmoja wa watanzania ambao wanajitambua na yeye alikuwa ni mtu aliejitambua.

Hii ni sifa moja kubwa sana ya binadamu, kujitambua.

Hayati Magufuli alijitambua na hata wengine kama mimi Richard najitambua.

Watanzania waafrika wengi na hata baadhi ya wazungu waliweza kuona hilo kuwa hayati Magufuli alijitambua na aliweka alama ya bara la Afrika kwenye koti lake.

Sasa baadhi ya wazungu na waafrika wengine hawapendi kuona waafrika wenzao wanajitambua maana wanahisi hapatashikika.

Kama hayati Magufuli aliweza kutikisa kila mahali na pakatikisika na akaja nchini bwana mkubwa wa uchimbaji madini kutoka Canada, basi alikuwa ni yeye na hatatokea Magufuli mwingine tena ndo imetoka hiyo.

Lakini bara la Afrika bado lina waafrika na watanzania wengi ambao bado hawajajitambua na ikifika siku wanajitambua itakuwa ni siku ya kiama na tutakuwa tumechelewa maana yeye alikwishasema tumecheleweshwa mno.

Ushuhuda ni madudu ambayo yameanza kurudi baada ya kuondoka kwake duniani, mara TRA kuna mitambo imeharibika, mara TANESCO mfumo wa LUKU umeingiliwa, mara majambazi yamerudi na mara bandarini kuna figisu zimerudi hii yote ni kuonyesha kuwa watanzania bado hawajaweza kujitambua.

Hapo awali , tulisikia mara Kitalu C kilianza kuingiliwa mpaka pale mama Samia alipoamuru ulinzi uimarishwe.

Pia tumesikia wizara ya fedha watu wamesimamishwa kazi kwa ubadhilifu wa fedha na hiyio ni wizara ya FEDHA yaani hazina ya nchi!

Hivyo, kwanza watanzania waweze kujitambua kuwa wao ni nani na wapo Tanzania kwa kusudio la Mungu ambae amewapa rasilimali na uwezo mkubwa wa kumiliki rasilimali hizo hivyo wahitaji usimamizi.

Kinachohitajika ni kujitambua, kisha kuhakikisha twazisimamia rasilimali hizo na kuzigeuza kuwa utajiri kiasi cha kumsaidia kila mtanzania aliezaliwa Tanzania na yule alie na vinasaba vya utanzania kwa elimu bora, makazi bora na maisha bora.
 
Back
Top Bottom