Rais Samia alimtumbua DED Msongela Nitu Palela kwa utendaji na usimamizi mbovu na Ufisadi, leo amemteua Palela Msongela Nitu

Rais Samia alimtumbua DED Msongela Nitu Palela kwa utendaji na usimamizi mbovu na Ufisadi, leo amemteua Palela Msongela Nitu

Mimi Huwa nikiwaambia, Tuna Rais Kazi yake ni KUSAINI TU muwe mnanielewa, yaan tuna Rais akiletewa makaratasi hajishughulishi kwenda Ndani zaidi ,ajiridhishe Kisha atoe ruksa !!.

Ebwana eeh Leo katika Kupitia majina ya UDED japo nione jina langu ,kijana Mzalendo kama Mimi, nikakutana na hili jina la Palela , haraka haraka nikakumbuka aliwah kutumbuliwa !!


Mwezi wa kwanza alitumbuliwa Kwa jina la Msongela Nitu Palela .
Wahuni ameona sio tabu, wakajua wakianza Kwa jina la Msongela ,watashtukiwa.


Kwenye mkeka wamemuanzia
PALELA MSONGELA NITU .
Hivi ni kwamba Hii Nchi Haina watu ?? Mpaka muwarudishe madaraka watu ambao mliwatumbua Kwa makosa yako ya kibadhirifu, wizi wa Pesa za umma, usimamizi mbovu wa miradi ???


Hivi Rais Samia yeye Huwa hajipi muda wa Kusoma na kupitia anacholetewa ??.

Unamtumbua mtu mwenyewe Kwa sababu ya Makosa makubwa aloyatenda, Ndani ya miezi minne, unamchagua upya ?? Kwamba kakuomba msahama?? Kakiri hatorudia, alisingiziwa ??.




Mama Samia jamani, mbona unatutia hasira sana sisi wananchi ??,. Kwanini watu wasiseme, Nchi inaongozwa na JK??.



Yaan DED alipata Hati Chafu, ukamtumbuaga baadae, Tena baada ya Waziri Bashungwa akiwa TAMISEMI kugundua matakataka ya DED huyu, Leo unamrudisha ??.


Sawa, ngoja waendelee kula, ngoja wananchi Tuendelee kutaabika.

2.Msongela Palela wa zamani
View attachment 2649078

80 Palela Msongela Mpya🤣
View attachment 2649079



Mambo ya Ovyo kabisa !!.

Naamini hapa kuna makosa ktk teuzi mpya, lazima utasikia atamtoa, jamani, Mh. Rais ni binadamu kama sisi, hivyo makosa kwa bahati mbaya anaweza kufanya, naamini hili atarekebisha na kumtoa kabisa.
 
Hivi watu wazima na ndevu zao wanakubalije kazi za kuteuliwa, kutumbuliwa na kuhamishwa anytime as though hawana maisha mengine? Huwa Nashangaa zaidi Hilo kuliko hizi teua tengua.
Upo sahihi Kwa Upande huo.... Haya unapoteuliwa Sasa kwann usiwawajibikie Watu wako?
 
Kawawa royal family inaendelea na status ago yao,shukraani kwa babu yao aliyewasafishia njia,naona wajukuu sasa wameshaanza kupanda!but why tunalalama humu kwenye soft landing hii?
 
Naamini hapa kuna makosa ktk teuzi mpya, lazima utasikia atamtoa, jamani, Mh. Rais ni binadamu kama sisi, hivyo makosa kwa bahati mbaya anaweza kufanya, naamini hili atarekebisha na kumtoa kabisa.
Hilo ni zaidi ya kosa, uteuzi huwa inafanyika vetting. Pia list kabla haijatoka inapitiwa

Kama kosa hilo wameshindwa kuliona, vipi mengine makubwa?
 
Kuna Kila Dalili hapaa, Huu mkeka una majina ya maDED wote walotumbuliwa na wenye kesi mahakaman, ila majina Yao yamekuja kivingine yaan Kichwa chini miguu juu, Kwa sababu wanajua SSS hajiangaishi Kusoma, na hata akisoma akikuta jina jingine ,hatozingatia.

Hayati JPM alipitia jina Kwa jina ,jina Kwa jina, Mwambaa hakua na janjajanja
SI mnaona chalamila aliwahi kutumbukiwa,baada ya muda wakasahau kama walimtumbua
 
Naamini hapa kuna makosa ktk teuzi mpya, lazima utasikia atamtoa, jamani, Mh. Rais ni binadamu kama sisi, hivyo makosa kwa bahati mbaya anaweza kufanya, naamini hili atarekebisha na kumtoa kabisa.
Hivi ww uko sawa kweli jamaa?!! Yani taasisi kubwa km Raisi ifanye makosa ya kuwasahau watumishi waliotumbuliwa kisha kuwarudisha upya,ndo kusema sio yeye anaowateua ama?! Kwmb alivoona majinga mengi katia saini tu fresh
 
Wazungu wana kila sababu ya Kutubagua kwa dharau na Kejeli Sisi watu weusi na hiyo yote ni kutokana na mambo kam Haya yani ni Aibu tupu.

Ifike mahali watu weusi tubadilike viongozi Wanatuludisha sana nyuma Sasa kuna maan gan ya mtu kutumbuliwa alf akabadilishiwa tena kitengo apewe kingne ?

Mi nasemaga Hii Afrika ingefaa ipate dikteta mmoja mfano kam Hitler au Kim jong Un, ndo Akili zitatukaa sawa afrika haitokuwa huru mpka Mfumo wa Demokrasia utoke,

Mimi naamini nchi yyte ya kiafrika itakayohitaj maendeleo bas Itumie mfumo wa Udikteta Tu ndo Suluhisho tuachane na hizi siasa za Kulambana miguu na kubembelezana bembelezana.
Hakika, sisi ngozi nyeusi ni wajinga sana
 
Kuna barua inakuja kabla ya kuapishwa watu. Ndiyo maana wanatangazwa majina yao kabla ya kuapishwa. Tuendelee kumsaidia Rais kuyachambua, wala rushwa wanachomeka watu wao. Na mie nimembaini mwizi fulani naandaa ushahidi, nitarudi.
Wacha tuone
 
Anayepaswa kuwajibika sasa ni Katibu Mkuu kiongozi.

Mh Rais kwa hao DED na DAS hana uwezo wa kuwafahamu. Ni watu wadogo Rais kuwafahamu na kuwakumbuka.

Sawa, inavyosomeka ni kuteuliwa na Rais ila wanaoratibu ni ofisi ya Katibu Mkuu kiongozi.

Kama naye kaingizwa Mkenge basi awawajibishe idara ya Utumishi.
Wacha tuone
 
Back
Top Bottom