Rais Samia amefanikisha kwa mara ya kwanza wanafunzi zaidi ya milioni moja kwenda shule kwa pamoja

Rais Samia amefanikisha kwa mara ya kwanza wanafunzi zaidi ya milioni moja kwenda shule kwa pamoja

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Leo Jumatatu ya tarehe 09/01/2023 wanafunzi wamefungua shule ikiwemo wanafunzi 1,073,941 walioanza kidato cha kwanza ambao wote walipangiwa shule hakuna mwanafunzi ambaye yuko nyumbani kusubiri chaguo la pili "Second Selections"

Ikumbuke tangu kuanza kwa utoaji wa elimu bila malipo nchini kumekua na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaojiunga na shule za msingi na sekondari. Mkakati wa serikali ya Rais Samia Suluhu ulikua ni kuboresha mazingira ya elimu na kufuta chaguo la pili hivyo kuanzia mwaka 2021 ujenzi wa madarasa nchi nzima ulianza.

Mwaka 2021 serikali ya Rais Samia ilijenga madarasa 15,000 na Septemba mwaka 2022 ujenzi wa madarasa 8,000 ulianza na kufikia mwezi Desemba tayari yalikua yamekamilika kwa ajili ya kupokea wanafunzi Januari mwaka huu. Mpango huu ni endelevu kwani kupitia TAMISEMI wamefanya tathmini kubaini maeneo ambayo bado yana uhitaji wa Madarasa, walimu, vyoo, mabweni na maabara ili viweze kujengwa.

Serikali ya Rais Samia mbali na kuimarisha miundombinu bado imehakikisha elimu inatolewa bila malipo, mikopo inatolewa kwa wanafunzi wa vyuo pamoja na kuanza kuanzishwa kwa "Samia Scholarship".
FmB1hYvXwAAD6J7
FmB1hYxXoAE8o7g
FmB1hYuXgAIMuh8
FmB1hYvXwAAD6J7
 
hii ni habari njema sana kwa wazalendo wa kweli,
lakini ni habari mbaya kwa wazandiki na wanafiki!!! ambao kwao habari nzuri wanapenda wasikie kuwa wanafunzi wanasomea chini ya mti au wanafunzi wanakaa chini/sakafuni.

pongezi kwa Rais Dr. Samia na wasaidizi wake kwa kutatua changamoto sugu ya upungufu wa madarasa, madawati na matundu ya vyoo.
 
Leo Jumatatu ya tarehe 09/01/2023 wanafunzi wamefungua shule ikiwemo wanafunzi 1,073,941 walioanza kidato cha kwanza ambao wote walipangiwa shule hakuna mwanafunzi ambaye yuko nyumbani kusubiri chaguo la pili "Second Selections"

Ikumbuke tangu kuanza kwa utoaji wa elimu bila malipo nchini kumekua na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaojiunga na shule za msingi na sekondari. Mkakati wa serikali ya Rais Samia Suluhu ulikua ni kuboresha mazingira ya elimu na kufuta chaguo la pili hivyo kuanzia mwaka 2021 ujenzi wa madarasa nchi nzima ulianza.

Mwaka 2021 serikali ya Rais Samia ilijenga madarasa 15,000 na Septemba mwaka 2022 ujenzi wa madarasa 8,000 ulianza na kufikia mwezi Desemba tayari yalikua yamekamilika kwa ajili ya kupokea wanafunzi Januari mwaka huu. Mpango huu ni endelevu kwani kupitia TAMISEMI wamefanya tathmini kubaini maeneo ambayo bado yana uhitaji wa Madarasa, walimu, vyoo, mabweni na maabara ili viweze kujengwa.

Serikali ya Rais Samia mbali na kuimarisha miundombinu bado imehakikisha elimu inatolewa bila malipo, mikopo inatolewa kwa wanafunzi wa vyuo pamoja na kuanza kuanzishwa kwa "Samia Scholarship".
FmB1hYvXwAAD6J7
FmB1hYxXoAE8o7g
FmB1hYuXgAIMuh8
FmB1hYvXwAAD6J7
Aongeze na maticha
 
Da kinacho nifadhaisha tu,mtoto anafika kidato cha kwanza hajui kusoma wala kuandika. Naumia sana maana hakuna anayejali siyo wazazi,wala waalimu wala mpango kazi wa serikali. Najiuliza baada ya miaka 10 tutakuwa na wasomi wa aina gani. Gunapowwkeza kwenye miundo mbinu pia tuwekeze sana kwenye uwajibikaji wa serikali,waalimu na wazazi kwa ujumla kwa mtoto kupata maana halisi ya kwenda shule,kwamaana ya kujua kusoma na kuandika pia kuongeza maarifa. Asanteni
 
Da kinacho nifadhaisha tu,mtoto anafika kidato cha kwanza hajui kusoma wala kuandika. Naumia sana maana hakuna anayejali siyo wazazi,wala waalimu wala mpango kazi wa serikali. Najiuliza baada ya miaka 10 tutakuwa na wasomi wa aina gani. Gunapowwkeza kwenye miundo mbinu pia tuwekeze sana kwenye uwajibikaji wa serikali,waalimu na wazazi kwa ujumla kwa mtoto kupata maana halisi ya kwenda shule,kwamaana ya kujua kusoma na kuandika pia kuongeza maarifa. Asanteni
Mtoto wa form two unamuliza 9x6 anakwambia yeye amechagua Masomo ya arts...🤣
 
Hii nchi Ina ushamba wa kutisha.

Katoa hizo pesa kwenye mshahara wake?

Kuna alichofanya ambacho sio jukumu lake?


Ushamba wa kutisha!
 
Mtoto wa form two unamuliza 9x6 anakwambia yeye amechagua Masomo ya arts...🤣
Inauma sana yaani inamaana kuna shule watoto wanaosoma hawatakuja kuwa na uwezo wowote kiushindani ktk ajira
 
Da kinacho nifadhaisha tu,mtoto anafika kidato cha kwanza hajui kusoma wala kuandika. Naumia sana maana hakuna anayejali siyo wazazi,wala waalimu wala mpango kazi wa serikali. Najiuliza baada ya miaka 10 tutakuwa na wasomi wa aina gani. Gunapowwkeza kwenye miundo mbinu pia tuwekeze sana kwenye uwajibikaji wa serikali,waalimu na wazazi kwa ujumla kwa mtoto kupata maana halisi ya kwenda shule,kwamaana ya kujua kusoma na kuandika pia kuongeza maarifa. Asanteni
Wate hawajui kusoma na kuandika au baadhi?
 
Leo Jumatatu ya tarehe 09/01/2023 wanafunzi wamefungua shule ikiwemo wanafunzi 1,073,941 walioanza kidato cha kwanza ambao wote walipangiwa shule hakuna mwanafunzi ambaye yuko nyumbani kusubiri chaguo la pili "Second Selections"

Ikumbuke tangu kuanza kwa utoaji wa elimu bila malipo nchini kumekua na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaojiunga na shule za msingi na sekondari. Mkakati wa serikali ya Rais Samia Suluhu ulikua ni kuboresha mazingira ya elimu na kufuta chaguo la pili hivyo kuanzia mwaka 2021 ujenzi wa madarasa nchi nzima ulianza.

Mwaka 2021 serikali ya Rais Samia ilijenga madarasa 15,000 na Septemba mwaka 2022 ujenzi wa madarasa 8,000 ulianza na kufikia mwezi Desemba tayari yalikua yamekamilika kwa ajili ya kupokea wanafunzi Januari mwaka huu. Mpango huu ni endelevu kwani kupitia TAMISEMI wamefanya tathmini kubaini maeneo ambayo bado yana uhitaji wa Madarasa, walimu, vyoo, mabweni na maabara ili viweze kujengwa.

Serikali ya Rais Samia mbali na kuimarisha miundombinu bado imehakikisha elimu inatolewa bila malipo, mikopo inatolewa kwa wanafunzi wa vyuo pamoja na kuanza kuanzishwa kwa "Samia Scholarship".
FmB1hYvXwAAD6J7
FmB1hYxXoAE8o7g
FmB1hYuXgAIMuh8
FmB1hYvXwAAD6J7
Baada ya kukopa serikali imejenga madarasa hahahahaha nchi ya misukule inakishwa unga inashangilia
 
Hayo ni mabomu ya kisiasa.

Serikali iachana na wingi iwekeze kwenye ubora wa elimu
 
Leo Jumatatu ya tarehe 09/01/2023 wanafunzi wamefungua shule ikiwemo wanafunzi 1,073,941 walioanza kidato cha kwanza ambao wote walipangiwa shule hakuna mwanafunzi ambaye yuko nyumbani kusubiri chaguo la pili "Second Selections"

Ikumbuke tangu kuanza kwa utoaji wa elimu bila malipo nchini kumekua na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaojiunga na shule za msingi na sekondari. Mkakati wa serikali ya Rais Samia Suluhu ulikua ni kuboresha mazingira ya elimu na kufuta chaguo la pili hivyo kuanzia mwaka 2021 ujenzi wa madarasa nchi nzima ulianza.

Mwaka 2021 serikali ya Rais Samia ilijenga madarasa 15,000 na Septemba mwaka 2022 ujenzi wa madarasa 8,000 ulianza na kufikia mwezi Desemba tayari yalikua yamekamilika kwa ajili ya kupokea wanafunzi Januari mwaka huu. Mpango huu ni endelevu kwani kupitia TAMISEMI wamefanya tathmini kubaini maeneo ambayo bado yana uhitaji wa Madarasa, walimu, vyoo, mabweni na maabara ili viweze kujengwa.

Serikali ya Rais Samia mbali na kuimarisha miundombinu bado imehakikisha elimu inatolewa bila malipo, mikopo inatolewa kwa wanafunzi wa vyuo pamoja na kuanza kuanzishwa kwa "Samia Scholarship".
FmB1hYvXwAAD6J7
FmB1hYxXoAE8o7g
FmB1hYuXgAIMuh8
FmB1hYvXwAAD6J7
Rais Samia Suluhu ameandika historia ndani ya siku chache za utawala wake amejenga madarasa ya kutosha na kupelekea kufutwa kwa second selection elimu ya Tanzania imeboreshwa kweli kweli
 
Kwahiyo Miaka Mingine Walikuwa Hawaendi Shule?
Shule Zilikuwepo Hata Wakati Wa Mkoloni
 
Back
Top Bottom