Rais Samia amefanikiwa kupanda mbegu ya uzalendo kwenye mioyo ya watanzania katika kuijenga nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe

Kwa uungwaji mkono alionao mh Rais na namna anavyokubalika nakuhakikishia kuwa mh Rais anakwenda kuzoa kura Zote uchaguzi ujao, maana amebeba na anatekeleza Sera na ajenda zinazogusa maisha ya mtanzania mnyonge
Sema sera za CCM....chama tawala...sera zinagusa maisha ya mnyonge kweli...unakumbuka JPM alivyokuwa akitambua wanyonge..mama Samia Rais wetu anaendeleza kutokea pale alipoacha mtangulizi wake..anajitahidi sana..aungwe mkono tujenge nchi yetu
 
Hizo ndo propaganda mnaelekezwa kupostii mitandaoni ili mkusanye vigezo vya kupewa teuzi!!??
Watanzania hawa si wajinga tena!
 
Mkuu maelezo haya next time weka takwimu ili kuthibitisha maelezo mazuri uliyotoa..
 
Hapo kwenye NENO MBEGU UZALENDO umekosea ulitakiwa kuandika MBEGU YA ASALI
 
Mada za kumpamba mama "yao" zimekuwa nyingi sana ..... Knacho nakisi hapa ni UOGA WA HALI YA JUU WA SERIKALI ILIYOPO MADARAKANI ...Ina tumia Hawa machawa/kupe kupima upepo.
Kazi iliyofanywa na mh Rais wetu imempa nafasi ya kuwa katika mioyo ya watanzania muda wote
 
Mambo unayoandika mkuu,

Kama vile hauna kichwa kabisa.

Ila naamini kuna wakati ukisoma mada zako huwa unacheka mwenyewe.

Akili zikikurudia lakini.
 
Mambo unayoandika mkuu,

Kama vile hauna kichwa kabisa.

Ila naamini kuna wakati ukisoma mada zako huwa unacheka mwenyewe.

Akili zikikurudia lakini.
Naandika Yale niliyona uhakika nayo na ninayoyaona yakitendeka huku mtaani kwangu kwa namna mh Rais alivyo panda mbegu ya Uzalendo kwa watanzania na juhudi zake katika kugusa maisha ya watanzania kwa kutatua na kushughulikia kero mbalimbali
 
Ningejua ulipo mkuu ningekupiga risasi nipunguze kura moja
Usiwe na mawazo ya namna hiyo ndugu yangu maana tunaweza tukatofautiana kimtizamo lakini tukakubaliana katika hoja ya kwamba nchi yetu itajengwa na sisi wenyewe

Lakini pia usipande mbegu katika moyo wako ya kutaka kumwaga damu ya mtu yoyote Yule unayetofautiana kimtizamo, mpende hata unayetofautiana Naye, unafikiri ukiwa na mawazo ya namna hiyo unazani utaua wangapi? Je ukiwamaliza kuwaua utaongoza wa akina Nani? Unazani hata watakao kupa kura Hakuna siku watakupinga na kukukosoa? Jee nao utawaua Tena

Mimi Nakusamehe bure tu bila shida maana Mimi moyo wangu Ni waupendo kwa watu wote hata ninao tofautiana nao na huwa natamanii Kama ningekuwa na uwezo ningeweza kusaidia wengi wenye kuhitaji msaada , macho yangu na moyo wangu unaguswa na shida za watu na kutamani kusaidia, jifunze kupenda hata unaotofautiana nao, upendo haupimwi kwa wale uwapendao Bali kwa wale unaotofautiana nao
 
Ifike mahali kabla ya watu kuingia Jf wapimwe akili aisee nimechoka Kwa hizi mada.
 
Kiukweli tunaomkubali Samia ni wengi ila 2025 Hawa watukanaji humu mitandaoni hawataamini wamebaki na wimbo wa tozo tu hawana jipya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…