Rais Samia ameonesha udhaifu mkubwa; sasa itaonekana kesi dhidi wapinzani zina mkono wa Serikali

Rais Samia ameonesha udhaifu mkubwa; sasa itaonekana kesi dhidi wapinzani zina mkono wa Serikali

Nimeishia kusoma ulipoandika Magufulist.
Point sio upinzani kuona kesi zao zote ni za kuchonga. Point yako ni kuwa ww mfuasi wa Magufuri na unaamini Magufuri ndiye aliyemfunga Mbowe na haujafurahishwa kuachiwa kwa Mbowe Ila ulifurahia kuachiwa kwa babu Seya.
 
Kwa kukubali viongozi wa dini kumvaa na kwa uhakika ni kwa ushawishi wa askofu shoo rais samia ameonyesha udhaifu mkubwa.

Gharama kiasi gani zimepotea kuendesha kesi dhidi ya Mbowe? Kwanini asisubiri ahukumiwe.

Magufulists hakika tumeudhika sana kuona huyo gaidi aliyekua ameanza kampeni mbaya kumdemonise Magufuli serikali ya Samia imemuachia.

Na ngoja samia ndio atawajua Chadema. Watasema wameshinda kesi ya uonezi na huyohuyo Mbowe ndio ataanza mashambulizi dhidi ya serikali ya CCM akikejeli na kutukana.

Uhakika Mbowe angekutwa na makosa na kuhukumiwa aende jela lakini askofu wa Chadema shoo bila shaka ameweza kuwashawi viongozi wa dini kumuomba rais kesi ifutwe kwenye hatua ya kujitetea mtuhumiwa.

Ili kuleta furaha kwa wote basi Mama Samia atoe msamaha na kufuta kesi zinazomkabili Sabaya. Tunajua Chadema kwa akili yao wanafikiri Mbowe hawezi kua gaidi na kwamba sabaya ni jambazi.

Sisi Magufulists tunaamini Mbowe angekutwa na hatia ya ugaidi na Sabaya amekua framed na wafuasi wa Mbowe. Kwahivyo Sabaya naye aachiwe vinginevyo hakuna kuelewana.
The demons have no friends, when they feel hungry and thirsty for blood the spirits of evils can enter the dirt of spiritually possessed individuals for abomination sacrifice.
 
Back
Top Bottom