Rais Samia amerejea kuomboleza msiba wa Hanang au amekuja kutuhamishia Burundi?

Rais Samia amerejea kuomboleza msiba wa Hanang au amekuja kutuhamishia Burundi?

Mkuu ukichukua 2,000 ya masikini inauma zaidi kuliko kuchukua 2,000,000 ya tajiri. Ukirudia kusoma uzi kwa makini utaelwa hoja yangu.
Kwa hio hao masikin watibiwe bure ? Wasitoe chochote? Wao kazi yao kwenye hili taifa ni ipi? Hao wenye pesa walipewa bure? Watu wafanya biashara wataokatwa pesa za electronic transfer wao walipewa bure?

Acheni ku glorify umaskini, mtu upo kwenye taifa unataka upewe kila kitu bure, wew mchango wako ni upi kama hata kukatwa 2000/- kwa mwezi kwenye electronic money transfer ili ugharamie matibabu yako huwezi?

Watu kama hao bora wahamie Burundi, ila ukweli kila mtu abebe mzigo wake, Binafs naona serikali kuhusu bima kwa wote inazingua, inachotakiwa kufanya ni kuweka mazingira rafiki ya ulipaji kwa kila mtu na bei ambayo ni rafiki kwa watanzania wengi,
Hivyo napendekeza

#1. Malipo yawe kwa mwezi, isiwe lazima mtu kulipa hela yote kwa mkupuo

#2. Watu wakijiunga kupitia vikundi wapunguziwe kadri kundi linavyozidi kuwa kubwa


Kulipiana bima ni kuzalisha kizazi cha wavivu wanaopenda kifanyiwa kila kitu
 
Binafs naona serikali kuhusu bima kwa wote inazingua, inachotakiwa kufanya ni kuweka mazingira rafiki ya ulipaji kwa kila mtu na bei ambayo ni rafiki kwa watanzania wengi,
Hivyo napendekeza

#1. Malipo yawe kwa mwezi, isiwe lazima mtu kulipa hela yote kwa mkupuo

#2. Watu wakijiunga kupitia vikundi wapunguziwe kadri kundi linavyozidi kuwa kubwa


Kulipiana bima ni kuzalisha kizazi cha wavivu wanaopenda kifanyiwa kila kitu
Mkuu umeongea vema. Serikali imekosea big time. Nchi inapuyanga tu kama kipepeo. Hii ndio hasara ya kuongozwa na mijitu isiyokwenda shule.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja sitaki kuwachosha. Mnakumbuka vizuri madhila yaliyotupata watanzania mwaka jana wakati serikali ilipoongezeka tozo za miamala maradufu hivyo kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu maradufu. Kana kwamba hiyo haitoshi waziri wa fedha msomi, Mwigulu Nchemba aliwakejeli watanzania kwa kusema kuwa kodi lazima zikatwe haijalishi watanzania wanaumia kiasi gani na kwamba asiyetaka kukamuliwa tozo ahamie Burundi.

Suala hili liliwauma sana watanzania lakini kwa kuwa hawana pa kukimbilia wameendelea kubakia hapa nchini na wanakamuliwa ‘kodi ya kizalendo’ kweli kweli. Kinachoudhi zaidi ni kwamba wabunge wa CCM wanaofanya haya maamuzi, hawalipi kodi, hivyo hawahusiki na kodi hizi za kizalendo kwa kuwa wao sio wazalendo bali wananchi masikini ndio wazalendo kindakindaki.

Wakati vumbi la kodi ya uzalendo halijatua, Rais Samia amerejea nchini kwa dharula kuja kusaini muswada wa bima ya afya. Baadhi ya watanzania mbumbumbu wasiojua kitu na wasiokuwa na chembe ya ufahamu wa mambo, hasa chawa wa mama, wamesikika wakishangilia kitendo hiki alichofanya Rais kama mazuzu. Wasichokifahamu ni kwamba fedha zitakazotumika kugharamia matibabu ya bima ya afya kwa wote zitatokana na ongezeko la tozo litakaloingizwa tena kwenye miamala ya kieletroniki.

Wakati muswada ulipopitishwa bungeni kwa 100% na wabunge wa CCM, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema moja ya vya mapato ya kugharamia matibabu haya kwa watanzania masikini ni ongezeko jipya la tozo za miamala. Sote tunafahamu kuwa miamala haibagui. Haimjui tajiri wala masikini. Inakata kotekote. Haohao masikini ambao serikali ya CCM inajidai kuwahurumia ndio hao hao watakaobebeshwa mzigo wa tozo ili kugharamia matibabu yao wenyewe. Sasa hapa unafuu upo wapi? Ikiwa wanajinasibu kuwa wanawajali masikini mbona wanawakamua tena masikini kupata fedha za kuwahudumia masikini ‘bila malipo’?

Ni mwendawzimu pekee atakayefurahia ujio wa sheria ya bima ya afya kwa wote. Tukumbuke bima ya afya ya sasa haikamui watu wasiohusika. Naomba tuelewane vizuri hapa. Mfuko wa NHIF unatunishwa kutokana na michango ya wanachama tu. Hauwagusi wasiokuwa wanachama. Lakini bima ya afya kwa wote itawagusa wote……waliomo na wasiokuwamo. Huu ni zaidi uzezeta.

Na tukumbuke kwamba sio watanzania wote wanaotegemea bima ya NHIF. Wengine wamo kwenye bima nyingine kama vile AAR, Strategies, Momentum, nk. Sasa kitakachotokea ni kwamba hata kama mtu unatibiwa kwa bima ya AAR ambako michango yako inaingia, utalazimika tena kukatwa pesa zaidi ili ziende kuhudumia wanachama wa NHIF. Maana yake ni kwamba utalazimika kujilipia bima yako ya AAR huku ukijiandaa kukamuliwa fedha zaidi ziende zikawalipie watu wengine kwenye bima nyingine ya afya isiyokuhusu ndewe wala sikio.

View attachment 2834133
Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha.
Njia mbdala?
 
Mkuu umeongea vema. Serikali imekosea big time. Nchi inapuyanga tu kama kipepeo. Hii ndio hasara ya kuongozwa na mijitu isiyokwenda shule.
Kwa kiasi imekosea, sema tusimalize maneno, tusubiri sheria na sera zinazokuja sasa,
Ila am sure hao wataopewa bima za bure zitakuwa ni za ovyo, zitakuwa za kumuona Dr. Na hazina vipimo vingi na dawa nyingi, ukitaka ya uhakika ni kulipia
 
Iv kwa mfano ww ni mkuu wa kaya wanakutegemea kwa kila kitu lakini haufanyi kazi, kazi yako kuzurura na kuuza kilichopo home kisha kukitokea mmoja wa wanafamilia kupata shida au kufariki,ndo unarudi home na unajifanya umesktishwa na kifo na kutoa msaada,na wanafamilia wakakushangilia kuwa ndo mkuu wa kaya mwema. hii imekaaje, ngoja tu niixhie apa
 
Iv kwa mfano ww ni mkuu wa kaya wanakutegemea kwa kila kitu lakini haufanyi kazi, kazi yako kuzurura na kuuza kilichopo home kisha kukitokea mmoja wa wanafamilia kupata shida au kufariki,ndo unarudi home na unajifanya umesktishwa na kifo na kutoa msaada,na wanafamilia wakakushangilia kuwa ndo mkuu wa kaya mwema. hii imekaaje, ngoja tu niixhie apa
Umeona eeh? Hii ni shida sana mkuu. Nashangaa muathirika mmoja wa mafuriko amepewa msaada kule Hanang amemshukuru Rais kuleta tope limesababisha amepata msaada. Nchi hii ina watu wa ajabu sana aisee!
 
Umeona eeh? Hii ni shida sana mkuu. Nashangaa muathirika mmoja wa mafuriko amepewa msaada kule Hanang amemshukuru Rais kuleta tope limesababisha amepata msaada. Nchi hii ina watu wa ajabu sana aisee!
mungu anisaidie nikue nizae niwe mkuu wa kaya mbona mashamba yote alokodisha bibi nawakabidhi wanakaya iwe mali yao kama wataamua kuyalima watalima kama hawalimi yatabak hvo hvo si ni mali yao kwan lazima kukodisha?
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja sitaki kuwachosha. Mnakumbuka vizuri madhila yaliyotupata watanzania mwaka jana wakati serikali ilipoongezeka tozo za miamala maradufu hivyo kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu maradufu. Kana kwamba hiyo haitoshi waziri wa fedha msomi, Mwigulu Nchemba aliwakejeli watanzania kwa kusema kuwa kodi lazima zikatwe haijalishi watanzania wanaumia kiasi gani na kwamba asiyetaka kukamuliwa tozo ahamie Burundi.

Suala hili liliwauma sana watanzania lakini kwa kuwa hawana pa kukimbilia wameendelea kubakia hapa nchini na wanakamuliwa ‘kodi ya kizalendo’ kweli kweli. Kinachoudhi zaidi ni kwamba wabunge wa CCM wanaofanya haya maamuzi, hawalipi kodi, hivyo hawahusiki na kodi hizi za kizalendo kwa kuwa wao sio wazalendo bali wananchi masikini ndio wazalendo kindakindaki.

Wakati vumbi la kodi ya uzalendo halijatua, Rais Samia amerejea nchini kwa dharula kuja kusaini muswada wa bima ya afya. Baadhi ya watanzania mbumbumbu wasiojua kitu na wasiokuwa na chembe ya ufahamu wa mambo, hasa chawa wa mama, wamesikika wakishangilia kitendo hiki alichofanya Rais kama mazuzu. Wasichokifahamu ni kwamba fedha zitakazotumika kugharamia matibabu ya bima ya afya kwa wote zitatokana na ongezeko la tozo litakaloingizwa tena kwenye miamala ya kieletroniki.

Wakati muswada ulipopitishwa bungeni kwa 100% na wabunge wa CCM, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema moja ya vya mapato ya kugharamia matibabu haya kwa watanzania masikini ni ongezeko jipya la tozo za miamala. Sote tunafahamu kuwa miamala haibagui. Haimjui tajiri wala masikini. Inakata kotekote. Haohao masikini ambao serikali ya CCM inajidai kuwahurumia ndio hao hao watakaobebeshwa mzigo wa tozo ili kugharamia matibabu yao wenyewe. Sasa hapa unafuu upo wapi? Ikiwa wanajinasibu kuwa wanawajali masikini mbona wanawakamua tena masikini kupata fedha za kuwahudumia masikini ‘bila malipo’?

Ni mwendawzimu pekee atakayefurahia ujio wa sheria ya bima ya afya kwa wote. Tukumbuke bima ya afya ya sasa haikamui watu wasiohusika. Naomba tuelewane vizuri hapa. Mfuko wa NHIF unatunishwa kutokana na michango ya wanachama tu. Hauwagusi wasiokuwa wanachama. Lakini bima ya afya kwa wote itawagusa wote……waliomo na wasiokuwamo. Huu ni zaidi uzezeta.

Na tukumbuke kwamba sio watanzania wote wanaotegemea bima ya NHIF. Wengine wamo kwenye bima nyingine kama vile AAR, Strategies, Momentum, nk. Sasa kitakachotokea ni kwamba hata kama mtu unatibiwa kwa bima ya AAR ambako michango yako inaingia, utalazimika tena kukatwa pesa zaidi ili ziende kuhudumia wanachama wa NHIF. Maana yake ni kwamba utalazimika kujilipia bima yako ya AAR huku ukijiandaa kukamuliwa fedha zaidi ziende zikawalipie watu wengine kwenye bima nyingine ya afya isiyokuhusu ndewe wala sikio.

View attachment 2834133
Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha.
"" Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha."" [emoji3596]
NMEKUELEWA VYEMA
 
Wapunguze seminar na washa zimezidi.Viongozi wapunguze safari na misururu ya watu wanaoambatana nao nchiza nje. mabalozi watumike.Mashangingi yasitumike
 
Kama nani? Pendekeza nitawaomba wasi mkolimbe.
Acha utani. Nchi hii inahitaji uongozi thabiti siyo maigizo. Nitakupa majina tutakapoambiwa Watanzania wenye nia wajitokeze. Kumbuka wale wenye IQ na uwezo wa kuongoza huwa hawataki kupewa madaraka. Hao ndiyo itabidi tuwaombe wajitolee ingawa wao hawapendi kuingia kwenye usanii (siasa)!
 
Mkuu
1. Serikali siku zote wanajinasibu kuwa wanawasaidia kupata matibabu BURE lakini pesa inayotumika kugharamia matibabu inakamuliwa kutoka kwa wanyonge hao hao. Kwa hiyo wanakuwa hawajawapa unafuu wowote. Hii ndio pointi yangu.

2. Idadi ya watu wazima (hasa waliohitimu vyuoni) kutokuwa na kazi hili ni tatizo la serikali. Ndiyo inayopaswa kuboresha mitaala itakayowawezesha wahitimu kujiajiri na pia serikali ndio inapaswa kutengeneza nafasi za ajira ili wananchi wapate kuajiriwa.

Kuhusu mapendekezo yako umemsahau Mwigulu Nchemba aliyechota zaidi ya trilionii 3 za ufisadi kupitia mkataba wa ujenzi wa SGR. Hili utekelezaji wake ni mgumu. Kinachoweza kumaliza kansa hii kabisa ni kuwaondoa CCM madarakani kwani CCM ni kama ukoo wa panya......kila panya akizaliwa anakuwa mwizi.
Mkuu, labda tuelezane kidogo;
1. Ulitaka wapewe unafuu gani kwa mfano? Wa kutibiwa bure kabisa sio? Na kama jibu lako ni ndio je hizo dawa zitanunuliwa kwa pesa ya kina nani?
Kwa maoni yangu bure inayoongelewa hapa ni bure ya insurance baada ya mimi, wewe na Yule kukatwa kodi na may be hata mwaka mzima ukaisha na hatujafika hospital.
Pia kuna wale watakaohitaji matibabu say ya million 20 wakat yeye kwenye tozo zake za simu labda amechangia 1,500 tu. Huoni hapo huyo ametibiwa bure?

2. Nafasi za ajira hazitengenezwi bila kuwa na uchumi imara ambao hutengenezwa na mambo mengi kama vile sera bora za uwekezaji, workforce (ambayo Tunayo) pia mazingira safi ya kiuchumi yatakayovutia wawekezaji. Tunatakiwa sisi tudai mazingira bora yatakayofungua fursa na sio kudai serikali iajiri….hebu jiulize iajiri ili kuzalisha nini? Kumbuka ajira ni fixed cost kwenye mambo ya uchumi.

3. Mwigulu anaangukia katika hoja yangu ile ya mafisadi wote wakamatwe, mali zao zitaifishwe na jela iwahusu.

Bottom line, watanzania tuache kulia lia, serikali sio mama yako au baba yako ikupatie vya bure tuuu! Sera nyingi kama siasa ni kilimo, kazi ni kipimo cha utu nk nk zilikuwa ni katika lengo la kuwaamsha wananchi wajenge nchi yao but cha ajabu mpaka sasa wapo wanaotaka vya bure a.k.a DEZOOOO
 
Mkuu ukichukua 2,000 ya masikini inauma zaidi kuliko kuchukua 2,000,000 ya tajiri. Ukirudia kusoma uzi kwa makini utaelwa hoja yangu.
Nani alikuambia hivo mkuu? Kwani yeye huyo tajiri ameokota hiyo pesa?
 
Kwa hio hao masikin watibiwe bure ? Wasitoe chochote? Wao kazi yao kwenye hili taifa ni ipi? Hao wenye pesa walipewa bure? Watu wafanya biashara wataokatwa pesa za electronic transfer wao walipewa bure?

Acheni ku glorify umaskini, mtu upo kwenye taifa unataka upewe kila kitu bure, wew mchango wako ni upi kama hata kukatwa 2000/- kwa mwezi kwenye electronic money transfer ili ugharamie matibabu yako huwezi?

Watu kama hao bora wahamie Burundi, ila ukweli kila mtu abebe mzigo wake, Binafs naona serikali kuhusu bima kwa wote inazingua, inachotakiwa kufanya ni kuweka mazingira rafiki ya ulipaji kwa kila mtu na bei ambayo ni rafiki kwa watanzania wengi,
Hivyo napendekeza

#1. Malipo yawe kwa mwezi, isiwe lazima mtu kulipa hela yote kwa mkupuo

#2. Watu wakijiunga kupitia vikundi wapunguziwe kadri kundi linavyozidi kuwa kubwa


Kulipiana bima ni kuzalisha kizazi cha wavivu wanaopenda kifanyiwa kila kitu
Kwani Kasharudi, lini.
 
Nani alikuambia hivo mkuu? Kwani yeye huyo tajiri ameokota hiyo pesa?
Matajiri wanapata pesa kwa masikini kwa kuwafanyisha kazi za cheap labour na kuwapandishia bei ya bidhaa kiholela. Kwa mfano unakuta serikali inaongeza kodi ya Tsh 100 kwa lita lakini tajiri anatumia kigezo hicho kupandisha nauli kwa Tsh 500 kwa kichwa. Wee huoni kuwa hapo masikini amekamuliwa mno?
 
Tatizo mkuu cjui watz tulilishwa Nini eti!.
Kuna wanavijiji wanatia kichefuchefu Haki ya nani.
Mfano,matatizo yaliyopo ya kimkakati bado wanapiga magoti kwa viongozi WA CCM eti wawasaidie miaka nenda Rudi.Hata ile kujiuliza Serikali inayoo gozwa na chama tangu uhuru ndo ile ile.
Kujiongeza hakuna,Kama mazumbukuku.Kina Tundu lisu Hadi wanachoka mkuu.
Mijitu inatetewa,lakini yapoe CCM miaka dahari na maisha no change.balabala,maji,hakuna.
Inqfikirisha.
Angalau mjini wanamwamko,ila vijijini ndo watu wengi wako kule.
Mungu alituepushia siasa zile zilizokuwa zinachipua kwa Kasi ya ajabu ya kuzimwa sauti mbadala eti zinakwamisha maendeleo😠😠😠.
Ukijiuliza Toka lini wapinzani walio gozwa Serikali ni lini hupati jibu.
Na bado mijitu inashangilia kwa shwangwe kulekule.Me nimpenzi WA Democrasia,kwa maana huamsha mengi.
 
Mkuu

Mkuu, labda tuelezane kidogo;
1. Ulitaka wapewe unafuu gani kwa mfano? Wa kutibiwa bure kabisa sio? Na kama jibu lako ni ndio je hizo dawa zitanunuliwa kwa pesa ya kina nani?
Kwa maoni yangu bure inayoongelewa hapa ni bure ya insurance baada ya mimi, wewe na Yule kukatwa kodi na may be hata mwaka mzima ukaisha na hatujafika hospital.
Pia kuna wale watakaohitaji matibabu say ya million 20 wakat yeye kwenye tozo zake za simu labda amechangia 1,500 tu. Huoni hapo huyo ametibiwa bure?

2. Nafasi za ajira hazitengenezwi bila kuwa na uchumi imara ambao hutengenezwa na mambo mengi kama vile sera bora za uwekezaji, workforce (ambayo Tunayo) pia mazingira safi ya kiuchumi yatakayovutia wawekezaji. Tunatakiwa sisi tudai mazingira bora yatakayofungua fursa na sio kudai serikali iajiri….hebu jiulize iajiri ili kuzalisha nini? Kumbuka ajira ni fixed cost kwenye mambo ya uchumi.

3. Mwigulu anaangukia katika hoja yangu ile ya mafisadi wote wakamatwe, mali zao zitaifishwe na jela iwahusu.

Bottom line, watanzania tuache kulia lia, serikali sio mama yako au baba yako ikupatie vya bure tuuu! Sera nyingi kama siasa ni kilimo, kazi ni kipimo cha utu nk nk zilikuwa ni katika lengo la kuwaamsha wananchi wajenge nchi yao but cha ajabu mpaka sasa wapo wanaotaka vya bure a.k.a DEZOOOO
Hii nchi watu wanadhani wanaidai nchi/serikali vitu vya bure, et mnalalamikia kugharamia bima ya Afya hahah
 
Hii nchi watu wanadhani wanaidai nchi/serikali vitu vya bure, et mnalalamikia kugharamia bima ya Afya hahah
Ni ajabu sana mkuu! Yaan watu wanataka vya bure tu…. Malalamiko yao ni serikali iwasaidie tu bila wao kuchangia maendeleo
 
Ni ajabu sana mkuu! Yaan watu wanataka vya bure tu…. Malalamiko yao ni serikali iwasaidie tu bila wao kuchangia maendeleo
Kwani hizo fedha ambazo wananchi wanaomba serikali "iwasidie" huwa serikali inaziokota wapi wakati hizo ni KODI zao wananchi?

Serikali inakusanya kodi kutoka kwa wananchi, hivyo ni lazima izirejeshe kodi hizo kwa wananchi kwa kuwaboreshea huduma za jamii. Hii sio hisani kwani fedha zote za serikali zinatoka ama kwa wananchi au kwa kuuza rasilimali za watanzania.
 
Back
Top Bottom