Rais Samia amkumbuka Juma Nature, hii ni heshima kubwa kwa mkongwe huyu wa Bongo Fleva

Rais Samia amkumbuka Juma Nature, hii ni heshima kubwa kwa mkongwe huyu wa Bongo Fleva

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Nukuu ya Rais Samia Suluhu Hassan alipokuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa jingo la benki, Machi 5, 2022 amemtaja staa mkongwe wa Bongo Fleva kwa kunukuu moja ya mstari wake aliowahi kuuimba kwenye kazi zake za muziki.

Hii hapa nukuu ya mama Samia:

"Mwanangu Juma Nature alisema, kwani wao waweze wana nini hata sisi tushindwe tuna nini?" amesema Rais Samia wakati akihimiza benki za Tanzania kwenda kuwekeza nje ya nchi kama ambavyo benki za nje zinavyokuja kuwekeza Tanzania.

Juma Kassim 'Nature' au Juma Nature ni msanii ambaye miaka 10 hadi 15 nyuma alikuwa ndiye 'Diamond' wa kipindi hicho, alifanya kazi nyingi zilizotikisa nchi, alikuwa mmoja wa wasanii wa kwanzakwanza wa muziki huo wa kizazi kipya kupata tuzo kutoka nje ya Tanzania.

Makazi yake yakiwa Temeke huku kazi nyingi akifanya na Prodyuza P Funk alijulikana kwa misemo yake hasa ya mtaani, alikuwa na uwezo wa kurap na kuimba pia.

Kwa miaka ya hivi karibuni amepoteza nguvu ya umaarufu wake katika muziki japokuwa amekuwa akiendelea kufanya kwa kutoa nyimbo kadhaa lakini hazijapata 'airtime' kama ilivyokuwa zamani.

FNFm8pUXMAQq8st.jpg


FNFm8tSWUAUx0jP.jpg
 
Jaman heshima na kukumbukwa vinahusiana na fedha, huyu ajakumbukwa Maemo wake umetumika
 
Nature hatari sana miaka yote namfahamu nilikuwa sijawahi muona nywele zake Hadi alipotoa video ya hakuna kulala (kwA mimi ) ndio niliona nywele zake

Jamaa huacha kichwa wazi kwa nadra sana (anapenda kofia balaa)
 
Kwa miaka ya hivi karibuni amepoteza nguvu ya umaarufu wake katika muziki japokuwa amekuwa akiendelea kufanya kwa kutoa nyimbo kadhaa lakini hazijapata 'airtime' kama ilivyokuwa zamani.
Ilitakiwa vyombo vinavyohusika na sanaa vimtembelee na kujua changamoto zake na kumsaidia ili kipaji chake kiendelee kuwa chachu kwenye fani ya sanaa nchini
 
Kuwekeza nje?

Hata ndani tu sio kila kona wanapatikana..., ondoeni Tozo muone jinsi mitandao ya simu hata in the middle of nowhere wanafikika

In short Banking system is soo yesteryear
 
Back
Top Bottom