Rais Samia amtembelea Mzee Warioba. Je, Katiba Mpya kupata kiki?

Rais Samia amtembelea Mzee Warioba. Je, Katiba Mpya kupata kiki?

Salaam Wakuu,

Leo rais Samia amemtembea Waziri Mstaafu Jaji Warioba na Mawaziri Wastaafu wengine.

Kwasababu Jaji Warioba anapigania Katiba Mpya, Je, rais kasikia kilio cha Watanzania? Jaji Warioba ataua ndege Wawili kwa Jiwe moja?

Mawaziri Wakuu wasitaafu wamekuwa Msitari wa Mbele kupambania Katiba Mpya.

Mwaka Ujao unaweza kuwa wa neema kwa Wapigania Katiba Mpya.

Aji Joseph Warioba alikuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Hivi karibuni, August 09 2021 Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba aliwataka viongozi wa Serikali kutegua kitendawili cha lini mchakato wa mabadiliko ya Katiba utahitimishwa ili Taifa liwe na utulivu.

Pia soma alichokisema Waziri Mkuu Msitaafu Msuya: Mzee Cleopa Msuya: Suala la Katiba Mpya haliepukiki kwani Katiba siyo Jiwe au Amri ya Mungu
View attachment 2030589
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumjulia hali leo tarehe 2 Desemba, 2021.
View attachment 2030593
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa David Msuya mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumjulia hali leo tarehe 2 Desemba, 2021.
Mama kaenda kumpiga Mkwara kiutu uzima
 
Kaenda kuweka handbrake wazee wasipige kelele kuhusu katiba mpya.

Kwenye swala la katiba mpya mh nadhani alikuwapo bungeni na alishiriki mijadala mbali mbali na anafahamu nini warioba ali address toka kwa wananchi
 
Hao wazee wasipokuwa wanafiki wakamwambia ukweli, wazo la katiba mpya litamsaidia aonekane shujaa kwataifa. Hilo litamfanya atengwe na inzi wa kijani. Akikataliwa ccm aende upinzani akagombee huko, na atapokelewa japo kwa masharti.
Nawajua wote hao wako straight kama rula na wanazeeka na misimamo yao. Muongeze hapo na Mzee Msekwa.
 
Katiba mpya hawezi kubali sababu itakuwa mwisho wake maana wananchi huku hawataki hata kumsikia kabisa
😁😁😁😁 jf bwana!

kila mmoja akijishibia kande na kujisikia tu kuongea basi huyo anafika na kubwabwaja
 
Anaenda kuwajulia hali si kupata maoni yao. Huwezi kumtembelea mtu lisaa limoja ukapata mawazo yake. Angekuwa serious kupata maoni angewaita ikulu na kufanya nao mikutano siku nzima.
Kwa mtu aliyejipanga maoni ya msingi unayapata ndani ya nusu saa. Ikizidi hapo ni kujirudirudia tu.
 
Hao wazee wasipokuwa wanafiki wakamwambia ukweli, wazo la katiba mpya litamsaidia aonekane shujaa kwataifa. Hilo litamfanya atengwe na inzi wa kijani. Akikataliwa ccm aende upinzani akagombee huko, na atapokelewa japo kwa masharti.
Atuachie kwanza nchi yetu halafu la katiba mpya lifuate. Hana huruma na wananchi. Bidhaa muhimu zote zimepanda bei!!

1 sukari
2. Mafuta ya kula
3. Vifurushi
4. Nondo
5. Cement
6. Mabati
7. Misumali
8. Rangi za nyumba
9. Chakula
10. Ugolo/ Tumbaku

Halafu wala hazumgumzii tatizo hili la mfumuko wa bei.
 
Atuachie kwanza nchi yetu halafu la katiba mpya lifuate. Hana huruma na wananchi. Bidhaa muhimu zote zimepanda bei!!

1 sukari
2. Mafuta ya kula
3. Vifurushi
4. Nondo
5. Cement
6. Mabati
7. Misumali
8. Rangi za nyumba
9. Chakula
10. Ugolo/ Tumbaku

Halafu wala hazumgumzii tatizo hili la mfumuko wa bei.
Lini sasa aichie nchi wakati kwanza ndio miezi 9 tu tangu aichukue. Labda muujiza utokee tena. Usiniulize muujiza gani nitakunasa kofi.
 
Back
Top Bottom