Rais Samia amvua hadhi ya Ubalozi Dkt. Slaa

Rais Samia amvua hadhi ya Ubalozi Dkt. Slaa

Acha kunajisi kanisa katoliki wewe. Slaa kaishi na mushumbusi mpaka na watoto wamezaa ni wapi kanisa linabariki mapadre wazae na wanawake?
Wewe ndio hujui sasa. One's umekuwa pandre ndio kimoja Chief hakuna kurud nyuma
 
DKt Wilbroad Slaa amevuliwa hadhi ya ubalozi kuanzia leo Septemba 1, 2023. Taarifa imetolewa hivi punde na Ikulu katika mtandao wa kijamii wa X ama Twitter.

Hayati Rais John Pombe Magufuli alimteua Dkt. Willibroad Slaa ambaya ni Katibu Mkuu wa zamani wa chama cha Upinzani, CHADEMA kuwa Balozi mnamo Novemba 23, 2017

Julai 22, Dkt. Slaa alizungumza na Wananchi kupitia vyombo vya habari akisema ni kwa ajili ya kuelimisha wananchi kuhusu kasoro zilizopo kwenye mkataba wa uwekezaji katika bandari ya Dar es Salaam.

Aliweka wazi kuwa hapingi uwekezaji katika bandari hiyo ya Dar es Salaam bali anapinga mkataba wa uwekezaji kwa kueleza kuwa hauna maslahi kwa Taifa.

Aidha, siku hiyo alisema “Najua maneno hayo ni makali… nimepokea vitisho na mimi pia sio tu Mawakili, wengine wakasema ubalozi wako tutachukua, nawaambia chukueni sasa hivi, siishi kwa ajili ya ubalozi. Nimesema sina chama najiamini najau ninachosimamia“

View attachment 2735983

=====
WILLIBROD PETER SLAA NI NANI?
View attachment 2735984
Dk Slaa alizaliwa Oktoba 29, mwaka 1948 wilayani Karatu. Alipata elimu ya msingi katika shule za Karatu na Kwermusi (Mbulu) kati ya mwaka 1958 na 1965.

Alisoma elimu ya sekondari katika Shule za Dung’unyi Seminari na Itega Seminari kati ya mwaka 1966 na 1971.

Ni kiongozi mwenye stashahada tatu pamoja na shahada ya Uzamivu (PhD). Anayo Shahada ya Uzamivu (PhD ) katika Sheria ya kanisa kutoka Chuo Kikuu cha St. Urban, Rome. Pia anastashahada ya Theolojia kutoka Kipalapala Seminari, Stashahada ya falsafa kutoka Kibosho Seminari, Stashahada ya Afya ya Macho kutoka Kituo cha Kimataifa cha Macho.

Amewahi kuwa padri wa Kanisa Katoliki kuanzia mwaka 1977 hadi 1991, akishika nafasi za kiutawala katika kanisa pia. Amepata kuandika vitabu vitatu ambavyo ni Utimilifu wa Msichana (1977), Utimilifu wa Mvulana (1977) na Expediency and exigency Liturgical Legislation (1981).

Ni mzungumzaji wa Lugha nane kwa ufasaha; ambazo ni Kiswahili, Kiingereza, Kilatini, Kiitaliano, Kijerumani, Kihispania, Kireno na Kifaransa.
Siku ya Alhamisi, Novemba 23, 2017 Aliyekuwa Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli alimteua Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kuwa balozi. Alikuwa Balozi wa Sweden, pia ailiidhinishwa kwa Nchi za Denmark, Finland, Norway, Iceland, Estonia, Latvia, Ukraine na Lithuania.

Kipindi Dk Slaa anateuliwa kuwa Balozi, alikuwa anaishi Canada, alitangaza kuachana na siasa kutokana na kutofautiana na chama chake katika kumpokea Edward Lowassa aliyehama kutoka CCM na baadaye kumpitisha kuwa mgombea urais kupitia muungano wa vyama vya siasa wa Ukawa.

Pia, soma: Balozi Dkt. Wilbroad Slaa kuvuliwa ubalozi na kukamatwa!
Anaweza kuwa yuko kazini pia .....! Good Morning
 
Nampongeza Mama Samia kwa haya maamuzi magumu. Haiwezekani kulea ujinga unaoathiri watanzania milioni 60. Dr Slaa amestahili hiyo adhabu.
Adhabu hii haina nguvu yoyote sana sana imemu expose Sa100 kwa watu wenye akili timamu!
Mwanamke hata awe na mamlaka vp hawezi acha kisirani, pia ni mnafki alijinasibu yeye ni mcha Mungu na mpenda maridhiano kumbe sivyo alivyo moyoni.
Angempotezea Slaa kwa watu makini angeonekana ana ngozi ngumu kweli kwa yeye kama mwanasiasa ila kumbe ni mpenda kusifiwa na kwamba hata haya maujinga ya chawa wa mama huwa yanamfurahisha sana moyo.
Jinga kabisa!
 
Kwenda huko wewe uliyekosa adabu na heshima.Alipewa na Mtu mwenye cheo cha Urais na sasa Amevuliwa na Rais . Aendelee na matusi na lugha zake za uchochezi aone kama hajatupwa Ndani kujieleza .
Alipewa cheo hicho na Rais (aliyechaguliwa kwa kura) ila kavuliwa na rais (aliyepewa na katiba).
Hata neno Rais na rais inasadifu tofauti zao!.
 
Mwabukuzi naye alisema wakitaka wachukue uwakili. Hivi wakivua wanapeleka wapi. Kuna siku viongozi wastaafu watavuiwa ustaafu we ngoja.
 
mimi nimeelewa uliposema sasa yeye haishi kupitia huo ubalozi.
na je angeliishi kupitia huo ubalozi nadhani mkataba wa bandari ungefaa.
 
Adhabu hii haina nguvu yoyote sana sana imemu expose Sa100 kwa watu wenye akili timamu!
Mwanamke hata awe na mamlaka vp hawezi acha kisirani, pia ni mnafki alijinasibu yeye ni mcha Mungu na mpenda maridhiano kumbe sivyo alivyo moyoni.
Angempotezea Slaa kwa watu makini angeonekana ana ngozi ngumu kweli kwa yeye kama mwanasiasa ila kumbe ni mpenda kusifiwa na kwamba hata haya maujinga ya chawa wa mama huwa yanamfurahisha sana moyo.
Jinga kabisa!
Mama aliyekuzaa wewe mpuuzi naye ni mnafiki sana na mwenye kisirani
 
Unafiki sio kitu kizuri.
Mzee slaa aliwasaliti CHADEMA mbele ya JPM kwajili ya tumbo lake, leo hii tena wapo pamoja kwenye jukwaa la kisiasa.
Mbowe na Lema wanapaswa kujitafakari sana, sio kwamba wanachadema wamesahau ila ...
 
Unafiki sio kitu kizuri.
Mzee slaa aliwasaliti CHADEMA mbele ya JPM kwajili ya tumbo lake, leo hii tena wapo pamoja kwenye jukwaa la kisiasa.
Mbowe na Lema wanapaswa kujitafakari sana, sio kwamba wanachadema wamesahau ila ...
Tujifunze kuheshimu maamuzi ya watu.
Nafikiri Slaa alifanya maamuzi sahihi kuliko hata Mbowe.

Angewezaje kukaa meza moja na Lowasa ambaye yeye alimtaja kuwa ni fisadi na eti anapewa ridhaa ya kugombea uraisi kupitia Chadema?

Slaa pekee ndiye alisimamia maneno yake aliyoyatamka
 
Back
Top Bottom