Rais Samia amwalika Rais Kenyatta kuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za miaka 60 za Uhuru wa Tanzania

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Rais Samia amesema amemuomba Rais Uhuru Kenyata wa Kenya kuwa mgeni rasmi katika sherehe ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania hapi tarehe 09/12/2021.

Rais Kenyatta amekubali ombi hilo.

===

Rais Samia Suluhu: Mwisho ni kwa taarifa yenu waandishi wa habari, mwaka huu ifikapo mwezi December, Tanzania tunatimiza miaka 60 ya uhuru wetu na hivyo nimetoa mwaliko rasmi kwa Rais Uhuru Kenyatta awe mgeni rasmi katika maadhimisho yale ya miaka 60 ya uhuru wetu.


Kazi Iendelee!
 
Mwanzo mzuri wa kukua kwa diplomasia ya Tanzania iliyokuwa imefikia kwango cha chini kabisa (2015-20) kuliko wakati wowote tangu uhuru! Liberata Mulamula kazini!
 
Hajasema "Mungu akipenda"? Kwa hisani ya KP.

Ha ha ha ha.....
 
Naona tumeanza kufungua milango kwa majirani, asije akajisahau tu hizo pesa zikabadilishiwa matumizi huo muda ukifika.
 
Nani anajua kuwa atafika huko decemba?
 
One thing I know for sure, Kenya ni ndugu zetu na marafiki zetu, lakini sisi na wao kila mmoja anajijali yeye kwanza, hivyo kwenye kila majadiliano tunaviziana nani afaidi kuliko mwingine. but generally, wao wakipata shida tutawasaidia na sisi tukipata shida watatusaidia, but kwenye maslahi, hapo tunaviziana.
 
Yani kamwalika Rais wa Kenya awe mgeni rasmi (the most important guest at an occasion) kwenye Sherehe ya Uhuru wa Tanganyika?? Hii protokali imeanza lini ndugu zangu😳😳😳😳
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…