Rais Samia anaweza kutoa mhadhara Chuo kikuu cha Havard au Yale Marekani na dunia nzima ikasimama

Rais Samia anaweza kutoa mhadhara Chuo kikuu cha Havard au Yale Marekani na dunia nzima ikasimama

Mwanzoni nilidhani watu wanakusingizia kumbe ni kweli..
Nilishakwambia siku nyingi kuwa mada zangu siyo saizi yako maana zilishakuzidi kimo cha akili na upeo wako.kwa hiyo ni bora ukae pembeni uache wenye akili wajadili hoja .
 
Kweli wewe ni mjinga sana.kwa hiyo asingeongoza na kuonyesha uwezo wake kiuongozi angefikaje hapo alipofika leo?
Kwahiyo kuwa kiongozi ndo kuwa na akili??

Aliongoza au alishinda wapi?... Chuma si ndo alimchukua tu?... Katiba ya CCM ndo ikamuweka pale?

Haya njoo utuambie aliongoza wapi tangu anasoma Bidudu hadi kuwa karani
 
Ndugu zangu Watanzania,

Chuo kikuu cha Havard kinachopatikana Nchini Marekani ni Chuo Bora kabisa Ulimwenguni ambacho kimekuwa kikishika nafasi ya kwanza kwa Ubora Duniani,huku Yale University nayo ikiwa katika nafasi za juu vilevile, ndipo katika kumi bora unaweza kuona sasa vyuo kama Oxford na Cambridge kutoka Uingereza vikiwemo,japo asilimia na kwa kiasi kikubwa kumi bora hutawaliwa na vyuo vya Marekani tu.

Ni katika vyuo hivyo viwili yaani Havard pamoja na Yale unakuta hata Ma Rais wengi sana walioongoza Taifa la Marekani wametokea na kupita katika vyuo hivyo. Hii ni kwa kuwa vyuo hivyo hubeba na kuchukua vipanga na vijana wenye akili za juu sana na uwezo wa kipekee sana kiakili.tena siyo zile akili za kukariri maandishi na kwenda kuyatema kwenye karatasi ya mtihani bila kuelewa hata maana yake wala umeandika nini.

Ni vyuo vinavyo beba watu wenye akili zinazowaka moto na upeo wa hali ya juu sana .hii ndio sababu vyuo hivi hutoa Na Rais wa Marekani, majasusi na watu mbalimbali kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hususani idara zake za ujasusi na upelelezi yaani CIA au FBI .au kuongoza mabenki na makampuni yao yenye maslahi kwa Taifa lao.hivi ndio vyuo vinatoa watu wenye akili ya kuifanya Marekani kuwa hapo ilipo leo hii.

Nikimuagalia Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan, kwa umakini wake, utulivu wake,upeo wake, akili kubwa aliyo nayo kichwani mwake, maarifa na uelewa wa masuala mbalimbali na kujiamini kwake naamini akipata nafasi ya kutoa Mhadhara kwenye vyuo hivyo,kwa hakika Dunia nzima inaweza kusimama na kutetemeka kama tetemeko la ardhi.

Hii ni kwa kuwa Rais Samia ana uwezo mkubwa sana wa kutoa hotuba, kuelezea jambo kwa utulivu, umakini, ufasaha na kwa mpangilio na mtiririko mzuri na wenye kuvutia. Anajuwa kupangilia hotuba katika namna inayoteka hisia za watu na kuvuta wasikilizaji kusikiliza bila kuchoka. Tofauti na mwingine anakuwa anatoa hotuba isiyo na muunganiko wala mtiririko wa kueleweka wala kuvutia.

Mfano jaribu kuangalia na kusoma hotuba za watu kama Dr Martin Luther king Jr hasa hotuba zake za I have a dream, I have been to the mountain top, Beyond Vietnam au Time to break silence, Our God is Marching on, The other American, Three evil of society. Unaweza pia soma hotuba ya Franklin Roosevelt hasa ile wakati anaapishwa, soma pia ya John F Kennedy ya mwaka 1963 kama sijakosea anayosema usiulize Marekani itakufanyia nini bali jiulize utaifanyia nini Marekani. Pia waweza soma ile ya Winston Churchill waziri mkuu wa Uingereza anayosema kuwa watapambana ardhini, angani, majini na popote pale.

Soma pia hotuba ya Barack Obama ile ya 2004 wakati anahutubia mkutano mkuu wa Democrat au ile siku ya kuapishwa au ya kukubali uteuzi au ile ya baada ya kupata ushindi. Waweza pia soma hotuba ya Mwalimu Nyerere ile ya 1995 akiwa mkoani Mbeya uwanja wa Sokoine siku ya wafanyakazi Duniani au ile pale Dodoma juu ya kiongozi aliyekuwa anahitajika kuletwa na wana CCM kwa watanzania kama mgombea au ile ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete siku ya Mazishi ya Hayati Nelson Mandela. Au waweza pia soma Hotuba ya Mama yetu mpendwa siku ameapishwa kuwa Rais wetu, ni hotuba yenye hisia kali sana inayoweza kukububujisha Machozi.

Nawasihi Wafuasi wa CHADEMA wawe wanasoma vitu na mambo mbalimbali ili kuongeza maarifa na uelewa, maana huwa nikiwasikiliza wakizungumza huwa naona aibu sana maana wao wakishindwa hoja na kuishiwa hoja unakuta wanaanza kuporomosha matusi kama vichaa au wendawazimu, mambo ambayo huwezi kuyakuta CCM, ndani ya CCM ni hoja kwa hoja na ndio maana chama kinaendelea kuaminika na kukubalika kwa mamilioni ya watanzania wa rika zote na kuendelea kusalia madarakani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Uwezo wake unaishia kuwasimamisha chawa na walamba asali wengine....baaasi
 
Usimfananishe Rais wetu mpendwa na kiongozi yeyote yule Barani Afrika.maana Rais wetu ni level nyingi,ni kiongozi na nusu,ni kiongozi aliyebeba Matumaini ya watanzania,ni kiongozi ambaye kama Bara la Afrika ingekuwa nchi moja basi Rais wetu ndiye angekuwa Rais wa Afrika

🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 . Nani amemtaja Rais wa nchi hapa kama sio wewe?
Halafu waswahili walitufundisha mwenzako akinyolewa......Usidharau sana yanayoendelea leo ulimwengu mzima. Kwa namna fulani pia yanatuhusu.
Tusiwe waongo mpaka tunaanza kujidanganya wenyewe
 
Kwahiyo kuwa kiongozi ndo kuwa na akili??

Aliongoza au alishinda wapi?... Chuma si ndo alimchukua tu?... Katiba ya CCM ndo ikamuweka pale?

Haya njoo utuambie aliongoza wapi tangu anasoma Bidudu hadi kuwa karani
Ungekuwa wewe na akili na uwezo basi ungepewa wewe.
 
Lucas Mwashambwa hapo kwenye kuisimamisha dunia ndiyo unaonekana dhahiri unamdhihaki Mh. Rais.
Kaa pembeni huko kama kifusi .maana wewe hujawahi kuwa na upendo wala uungaji mkono kwa Mheshimiwa Rais.wakati wote umekuwa mtu wa lugha chafu chafu tu kama mlevi wa gongo. Kwa hiyo ni bora ukae kimya tu mnafiki mkubwa wewe.
 
Kaa pembeni huko kama kifusi .maana wewe hujawahi kuwa na upendo wala uungaji mkono kwa Mheshimiwa Rais.wakati wote umekuwa mtu wa lugha chafu chafu tu kama mlevi wa gongo. Kwa hiyo ni bora ukae kimya tu mnafiki mkubwa wewe.
Utakuwa una matatizo ya lugha wewe, wapi nimetoa lugha chafu, au unafikiri Mh. Rais hataelewa kuwa unamkejeli kwa huu uzi wako wa kitoto, Waswahili wanasema akutukanaye hakuchagulii tusi. Shauri yako mwenyewe na kiherehere chako.
 
Utakuwa una matatizo ya lugha wewe, wapi nimetoa lugha chafu, au unafikiri Mh. Rais hataelewa kuwa unamkejeli kwa huu uzi wako wa kitoto, Waswahili wanasema akutukanaye hakuchagulii tusi. Shauri yako mwenyewe na kiherehere chako.
Nimesema wewe kaa pembeni na ujinga wako.maana siku zote umekuwa na lugha chafu kwa Mheshimiwa Rais.toa unafiki wako hapa wewe
 
Nimesema wewe kaa pembeni na ujinga wako.maana siku zote umekuwa na lugha chafu kwa Mheshimiwa Rais.toa unafiki wako hapa wewe
Weka hapa hata post yangu hata moja tu nimetoa lugha chafu kwa Rais, unaona umeyatimba sasa unataka kujipangusia kwangu. Wewe unafikiri ni mjanja utoe kejeli ya kiwango hiki kwa Rais halafu uachwe hivi hivi subiri uminywe korodani utie akili. Umeona teuzi zinakupita hivi hivi sasa unaleta matusi ya reja reja kwa Rais, utakomaje !!!
 
Ndugu zangu Watanzania,

Chuo kikuu cha Havard kinachopatikana Nchini Marekani ni Chuo Bora kabisa Ulimwenguni ambacho kimekuwa kikishika nafasi ya kwanza kwa Ubora Duniani,huku Yale University nayo ikiwa katika nafasi za juu vilevile, ndipo katika kumi bora unaweza kuona sasa vyuo kama Oxford na Cambridge kutoka Uingereza vikiwemo,japo asilimia na kwa kiasi kikubwa kumi bora hutawaliwa na vyuo vya Marekani tu.

Ni katika vyuo hivyo viwili yaani Havard pamoja na Yale unakuta hata Ma Rais wengi sana walioongoza Taifa la Marekani wametokea na kupita katika vyuo hivyo. Hii ni kwa kuwa vyuo hivyo hubeba na kuchukua vipanga na vijana wenye akili za juu sana na uwezo wa kipekee sana kiakili.tena siyo zile akili za kukariri maandishi na kwenda kuyatema kwenye karatasi ya mtihani bila kuelewa hata maana yake wala umeandika nini.

Ni vyuo vinavyo beba watu wenye akili zinazowaka moto na upeo wa hali ya juu sana .hii ndio sababu vyuo hivi hutoa Na Rais wa Marekani, majasusi na watu mbalimbali kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hususani idara zake za ujasusi na upelelezi yaani CIA au FBI .au kuongoza mabenki na makampuni yao yenye maslahi kwa Taifa lao.hivi ndio vyuo vinatoa watu wenye akili ya kuifanya Marekani kuwa hapo ilipo leo hii.

Nikimuagalia Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan, kwa umakini wake, utulivu wake,upeo wake, akili kubwa aliyo nayo kichwani mwake, maarifa na uelewa wa masuala mbalimbali na kujiamini kwake naamini akipata nafasi ya kutoa Mhadhara kwenye vyuo hivyo,kwa hakika Dunia nzima inaweza kusimama na kutetemeka kama tetemeko la ardhi.

Hii ni kwa kuwa Rais Samia ana uwezo mkubwa sana wa kutoa hotuba, kuelezea jambo kwa utulivu, umakini, ufasaha na kwa mpangilio na mtiririko mzuri na wenye kuvutia. Anajuwa kupangilia hotuba katika namna inayoteka hisia za watu na kuvuta wasikilizaji kusikiliza bila kuchoka. Tofauti na mwingine anakuwa anatoa hotuba isiyo na muunganiko wala mtiririko wa kueleweka wala kuvutia.

Mfano jaribu kuangalia na kusoma hotuba za watu kama Dr Martin Luther king Jr hasa hotuba zake za I have a dream, I have been to the mountain top, Beyond Vietnam au Time to break silence, Our God is Marching on, The other American, Three evil of society. Unaweza pia soma hotuba ya Franklin Roosevelt hasa ile wakati anaapishwa, soma pia ya John F Kennedy ya mwaka 1963 kama sijakosea anayosema usiulize Marekani itakufanyia nini bali jiulize utaifanyia nini Marekani. Pia waweza soma ile ya Winston Churchill waziri mkuu wa Uingereza anayosema kuwa watapambana ardhini, angani, majini na popote pale.

Soma pia hotuba ya Barack Obama ile ya 2004 wakati anahutubia mkutano mkuu wa Democrat au ile siku ya kuapishwa au ya kukubali uteuzi au ile ya baada ya kupata ushindi. Waweza pia soma hotuba ya Mwalimu Nyerere ile ya 1995 akiwa mkoani Mbeya uwanja wa Sokoine siku ya wafanyakazi Duniani au ile pale Dodoma juu ya kiongozi aliyekuwa anahitajika kuletwa na wana CCM kwa watanzania kama mgombea au ile ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete siku ya Mazishi ya Hayati Nelson Mandela. Au waweza pia soma Hotuba ya Mama yetu mpendwa siku ameapishwa kuwa Rais wetu, ni hotuba yenye hisia kali sana inayoweza kukububujisha Machozi.

Nawasihi Wafuasi wa CHADEMA wawe wanasoma vitu na mambo mbalimbali ili kuongeza maarifa na uelewa, maana huwa nikiwasikiliza wakizungumza huwa naona aibu sana maana wao wakishindwa hoja na kuishiwa hoja unakuta wanaanza kuporomosha matusi kama vichaa au wendawazimu, mambo ambayo huwezi kuyakuta CCM, ndani ya CCM ni hoja kwa hoja na ndio maana chama kinaendelea kuaminika na kukubalika kwa mamilioni ya watanzania wa rika zote na kuendelea kusalia madarakani.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mmmmh, aende akahojiwe na citizen ya Kenya, kwa, kizungu tuone kama anauwezo,
Rais wako anachoweza ni kuteua,kusafiri,na, kuzindua, na, kuuza, sura tu
 
Weka hapa hata post yangu hata moja tu nimetoa lugha chafu kwa Rais, unaona umeyatimba sasa unataka kujipangusia kwangu. Wewe unafikiri ni mjanja utoe kejeli ya kiwango hiki kwa Rais halafu uachwe hivi hivi subiri uminywe korodani utie akili. Umeona teuzi zinakupita hivi hivi sasa unaleta matusi ya reja reja kwa Rais, utakomaje !!!
Sina sababu ya kujibizana wala kubishana na wewe wakati najuwa huna akili .nikupoteza muda na nguvu zangu tu.wewe niwakupuuzwa tu.
 
Back
Top Bottom