Rais Samia, angalia viwanda hivi vilivyofungwa hapa Morogoro

Rais Samia, angalia viwanda hivi vilivyofungwa hapa Morogoro

mbikagani

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2014
Posts
3,107
Reaction score
1,782
RAIS Samia. Morogoro tunashida hizi;

KIWANDA CHA MAZAVA KUFUNGWA
1625661270284.png

Kiwanda hiki kilikuwa kinatengeneza nguo(jezi), kiliajiri zaidi ya watu elfu kumi(10000)

Kwa sasa kimefungwa kwa kile kinachoelezwa kuwa kutokuelewana na serikali ya awamu ya tano katika suala la ulipaji kodi.

Kimsingi hakuna anayependa mtu au taasisi isiyolipa kodi, lakini inasemekana mashariti ya ulipaji kodi yalikuwa kandamizi sana na ndiyo sababu ya hiki kiwanda kufunga uzalishaji.

Rais tupia jicho hapa ili kama kuna haja ya kuzungumza na wawekezaji hawa uwaruhusu wafungue kiwanda hiki maana wananchi wengi wamepoteza ajira zao.

2. KIWANDA CHA SUKARI CHA MBIGIRI CHASABABISHA UMASIKINI KWA WAKULIMA

1625661499174.png

Kiwanda hiki kimeleta umasikini mkubwa kwa wakulima wadogo wadogo wa miwa wilaya ya kilosa.

Mpaka sasa miwa yao imefikia kuvunwa na kiwanda bado hakijakamilika mpaka wanaamua kwenda kuuza kiwanda cha Mtibwa.
Mbaya zaidi benki ya AZANIA imewaongezea riba kwa kuchelewa kurudisha mikopo yao.

Kama haitoshi wakandarasi wamewashitaki wakulima kwa sababu benki ya AZANIA wamekataa kuwapa mkopo ambao kimsingi benki ilisaini mkataba wa kuwapa mkopo.

3. KIWANDA CHA TUMBAKU KUFUNGWA
1625661609830.png

Kiwanda hiki kiliajiri wananchi zaidi ya elfu kumi(10000), kwa sasa kimefungwa kwa kile kinachoelezwa ni kutoelewana na serikali ya awamu ya tano kwenye ulipaji kodi.

Si vema kutolipa kodi lakini inasemakana mpaka wameamua kufunga kiwanda, kodi ilikuwa kandamizi sana.

Angalia na hapa Mama kama mtaelewana waruhusu warejee ili wananchi wapate ajira maana kwa sasa wapo mitaani tu wanaangaika.
 
Mimi nadhani asiangalie Morogoro tu bali aangalie nchi nzima. Kama tukiweza kufufua hata nusu tu ya haya yaliyofungwa amini ukusanyaji wa kodi utakuwa mara dufu maana ajira zitakazo zalishwa sio tu za viwandani bali hata sekta ya kilimo na usafirishaji itakuwa kwa kasi kubwa.

Kizuri ni kwamba hadi sasa Serikali inaungwa mkono asilimia nzuri na wafanya biashara. Ni vema ikitumika nafasi hii kufufua hivi viwanda na hakika Tanzania itapiga hatua kubwa sana. Ni ushauri mzuri sana.
 
Mimi nadhani asiangalie Morogoro tu bali aangalie nchi nzima. Kama tukiweza kufufua hata nusu tu ya haya yaliyofungwa amini ukusanyaji wa kodi utakuwa mara dufu maana ajira zitakazo zalishwa sio tu za viwandani bali hata sekta ya kilimo na usafirishaji itakuwa kwa kasi kubwa. Kizuri ni kwamba hadi sasa Serikali inaungwa mkono asilimia nzuri na wafanya biashara. Ni vema ikitumika nafasi hii kufufua hivi viwanda na hakika Tanzania itapiga hatua kubwa sana. Ni ushauri mzuri sana.
Where you are.
Sehemu nyingi kuna mambo yakifanyiwa kazi kwa maelewano mazuri nchi itapiga hatua kubwa sana.
 
Viwanda amevizungumzia amesema wanashida ya masuala ya kodi

kwa ninavyojua Mazava kilifungwa kutokana na Corona
Mazava kilisimamishwa kwa ajili ya corona, lakini baadaye kilifungwa kwa ajili ya kutoelewa na serikali katika mambo ya ulipaji kodi
 
Mimi nadhani asiangalie Morogoro tu bali aangalie nchi nzima. Kama tukiweza kufufua hata nusu tu ya haya yaliyofungwa amini ukusanyaji wa kodi utakuwa mara dufu maana ajira zitakazo zalishwa sio tu za viwandani bali hata sekta ya kilimo na usafirishaji itakuwa kwa kasi kubwa.

Kizuri ni kwamba hadi sasa Serikali inaungwa mkono asilimia nzuri na wafanya biashara. Ni vema ikitumika nafasi hii kufufua hivi viwanda na hakika Tanzania itapiga hatua kubwa sana. Ni ushauri mzuri sana.
Dikteta aliharibu sn
 
Kiwanda Cha Tumbaku Philip Morris
Kingolwira Hapo Alliance One Nacho Kidogo
 
Kiwanda Cha Tumbaku Philip Morris
Kingolwira Hapo Alliance One Nacho Kidogo
Alliance one ni kidogo sana. Kile cha mjini (TTPL) ndio kilikuwa bonge la kiwanda tena kilikuwa na nyota tano kwa ufanisi na ubora. Msimu wa Tumbaku ukianza, mitambo haizimwi kwa miezi mitatu. Wanapisha wafanyakazi tu kwa shift tatu (kuna wanaoingia asubuhi, kuna wa mchana na wengine usiku). Na kila shift ina wafanyakazi zaidi ya 6,000.

Mbali ya Serekali kupoteza mapato, pia Vijana wengi wamekosa kazi na kusababisha wizi uanze kurudi huku mtaani. Kuna haja ya kufanya kitu ili hivi viwanda viendelee kuwepo.
 
Alliance one ni kidogo sana. Kile cha mjini (TTPL) ndio kilikuwa bonge la kiwanda tena kilikuwa na nyota tano kwa ufanisi na ubora. Msimu wa Tumbaku ukianza, mitambo haizimwi kwa miezi mitatu. Wanapisha wafanyakazi tu kwa shift tatu (kuna wanaoingia asubuhi, kuna wa mchana na wengine usiku). Na kila shift ina wafanyakazi zaidi ya 6,000.

Mbali ya Serekali kupoteza mapato, pia Vijana wengi wamekosa kazi na kusababisha wizi uanze kurudi huku mtaani. Kuna haja ya kufanya kitu ili hivi viwanda viendelee kuwepo.
Aisee ila Tz kuna mazingira magumu sana ya kibiashara mikodi ya kutosha na ukifungua tu kuanzia Mwenyekiti wa CCM mpaka RPC itabid wawe kwenye mfuko wako wa posho la sivyo utapata tabu sana
 
Hili neno Mama,Mama,Mama. Litakuja kuletwa matatizo tuendako. Mwiteni Rais.
 
Wacha tu aitwe mwendazake alikuwa hafai kwa taifa hili, tunamshukuru Mwenyezi kwa maamuzi matakatifu.
 
Wacha tu aitwe mwendazake alikuwa hafai kwa taifa hili, tunamshukuru Mwenyezi kwa maamuzi matakatifu.
Suala la kifo ni juu ya aliyetuumba.
Lakini hisia na kile mtu alichofanyiwa na aliyekufa siyo vibaya kukielezea.
 
Back
Top Bottom