Rais Samia aonya vikao vya Polisi kudhaminiwa

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amelionya jeshi la Polisi nchini kutotumia wadhamini kufanya vikao kazi na badala yake Jeshi hilo lijitegemee na vikao vyake vifanyika kwa gharama za Jeshi.

Amesema kuwatumia wadhamini katika kuwezesha kuendesha vikao hivyo, kutawafanya washindwe kuwaadhibu pale wanapofanya makosa.

Rais Samia ametoa maelekezo hayo leo Jumanne Agost 30, 2022, wakati akifungua kikao cha maofisa wa polisi makao makuu, makamanda wa mikoa na vikosi, kinachofanyika katika Shule ya Polisi Tanzania, mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Amesema kikao kinachofanyika leo kimedhaminiwa na taasisi mbalimbali za kiserikali na zisizo za serikali ambazo nazo zina binadamu na wanaweza kufanya makosa na wakashindwa kuwashughulikia.

"Leo tumekuja tuna wadhamini kama watano sita wametudhamini, lakini kama jeshi la polisi kikao kama hiki tunatakiwa tukifanye wenyewe, tujipange wenyewe,” amesema Rais Samia na kuongeza; "Waliodhamini leo ni taasisi mbalimbali za serikali na ambazo si za kiserikali, zina wanadamu wanaweza wakafanya makosa mkashindwa kuwashughulikia, kwa sababu wamewadhamini, mkutano kama huu mfanye kwa uwezo wenu wa Jeshi la Polisi, mjipekue mifukoni mfanye kikao."
 
Kweli Rais Samia Suluhu ameamua kusimamia haki kwa vitendo watanzania wote tunajivunia wewe mama
 
Ni sawa kabisa kwa utekelezaji wa kazi.
 
Ni kweli kabisa, huwezi kukata tawi ulilokalia hata siku moja au kunyea kambi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Si wanadhaminiwa na matajiri wa ccm?
 
Hii ni sawa na kumkandia Mwajuma mbele ya wana halafu wakiwa hawapo unampigia simu Mwajuma mkabanjuke.
Ndio nchi yetu tunavyo ishi hakuna namna. Hata wanao lia tuzo, itokee uso kwa uso na mama la mama alafu amuulize anazungumzia vipi kuhusu tuzo, lazima aipambe. So acha kila mtu aishi pale kamba yake inapofikia
 
Safi sana,ameongea vizuri.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…