Rais Samia apokea Ripoti za CAG na TAKUKURU za Mwaka 2021/2022
Hata Chadema wameanza kuona maridhiano yao na ccm nchi inaelekea kusiko
 

Attachments

  • FD9DB2FC-19BC-4553-A599-19111BFCA04B.jpeg
    FD9DB2FC-19BC-4553-A599-19111BFCA04B.jpeg
    77.2 KB · Views: 5
Kauli zilitolewa wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM uliopita. Nukuu zilitolewa kuhusu viongozi wazuri kutokufa, huku wake wa wale waliotangulia mbele za haki wakiwemo mkutanoni na kuzishuhudia.

Kauli iliwekwa sawa kuwa Mzee karopoka kwa kuwa alikuwa na mhemuko. Kauli nyingine ilitolewa na Mzee mwingine tena, Mama tunaye mwaka 2025, labda litokee jambo kubwa sana!?

Another one term president!? Jambo kubwa!? Linapaswa kutokea ili kiongozi Mkuu aonekane dhaifu,?

Kweli ukitaka kumuua kobe ni lazima ufanyie "timing" naona wana mtandao wakizidi kusukuma kete zao vyema.
 
Kuna usemi kwamba "Ya kale ni dhahabu. Model ya Magufuli itakumbukwa daima" Mama alipochukuwa nchi alisema hataki watu kuonewa akawaachia huru mafisadi waliowekwa ndani na serikali ya Magufuli (japo ela za Plea Bargaining zilizokuwa kwenye subira ya mchakato wa kisheria kuliwa nyuma ya Magufuli kufariki).

CAG Assad alipumzishwa kwa ripoti kama hizi hizi za CAG Kichere. Sijajuwa kama Kichere ataendelea kuvumiliwa hadi lini.

Mama hata kama hapendi mafisadi walio kwenye ripoti ya Kichere kushughulikiwa (kuonewa) lakini tayari CCM kimeshindwa kuvumilia na kuagiza serikali kuwachukulia hatua wahusika wote.

Pasina kujali udhaifu wa Mhimili wa Mahakama yetu lijapo suala la rushwa katika kufanya maamuzi ya mashauri, ni dhahiri kwamba mama sasa ana kigugumizi cha ni kwa vipi nilitoa mafisadi jela alafu leo tena niwarudishe jela ama wale wale au hata kama ni mafisadi wapya!

Huu ni mfupa mgumu kwa mama na huenda hata kwa CCM kilichompa maagizo kuwachukulia hatua za kisheria.

Dondoo chache kwenye ripoti ya CAG 2022 - 2023:

1. TTCL imekopesha watu wasiojulikana 21 bl.

2. Mkurugenzi Mkuu na maafisa wengine waandamizi wa TPA ambao wote waliondolewa kazini kwa utendaji mbovu bado wanaendelea kuidhinisha malipo kwenye mfumo wa TPA.

3. Takriban V8 mpya 40 za serikali zilizoagizwa zimeyeyuka bandarini.

4. CAG hakusaini (alirukwa) baadhi ya mikataba ya manunuzi makubwa ya kimkakati ughaibuni kama sheria inavyotaka.

Kwa ripoti hii ya CAG Kichere nchi inaenda wapi wakati wapigakura wanakula mlo mmoja? Mchele mbovu (chenga 3,100/)

Tujadili kwa ustaarabu kwa kujifunza kitu siyo kwa kushindana maana nchi ni yetu sote.View attachment 2579909
Hivi ripoti iliyopita ilifanyiwa kazi au ipo kabatini kama zilizopita?

Tunajadili nini kama haziwaumi watawwla wenye kuweza kuchukua hatua?

Tusubiri Mungu aimalize CCM kabisa ndo tutakuwa na mwanzo mpya.
 
Angalia walivyopiga pesa.ila kwakuwa watanzania hamjali hata Mimi nikipata nafasi nitapiga pesa[emoji23][emoji23]
JamiiForums-967246791.jpg
 
Angalia walivyopiga pesa.ila kwakuwa watanzania hamjali hata Mimi nikipata nafasi nitapiga pesa[emoji23][emoji23]View attachment 2582662
Ripoti ya mwisho ya CAG ni ya ubadhirifu ambao viongozi (Menejimenti na Bodi; Wakurugenzi wa Halmashauri, Mawaziri na Makatibu Wakuu) walishindwa kutoa majibu. Halafu Rais anawapa nafasi ya ati kuchunguza wahusika? Wafutwe kazi na TAKUKURU/Polisi wafanye kazi yao ili wasitafute watu wa kuwatwisha uchafu huo au kuficha ukweli.
 
Umeshaambiwa mtu anadai halafu hajui anayemdai mzee...!

IMEISHA HIYO.
 
Back
Top Bottom