Rais Samia asema itungwe Sheria itakayotoa muongozo kuwashughulia viongozi wanaofanya majukumu ambayo sio yao

Nimefarijika na kufurahia sana wasilisho la leo la Tume ya Haki Jinai lilifanywa na Jaji Mkuu mstaafu Mh.Othman Chande.

Juu ya yote nimependezwa na mapendekezo yaliyotolewa na approach aliyotumia Mh.Rais kuyatafutia ufumbuzi.

Tendo zima na dhamira ya Mh.Rais ni ya kiutu na kibinadamu,maana walioko jela ni binadamu kama sisi,wanahitaji kuwajali,kuwapenda na kuwaheshimu pia...japo miaka mingi tumewasahau mno.

Wahusika tumeaswa,tubadili mitazamo/mindset,tabia na tamaduni zetu za kuenenda kama tume ilivyoshauri.

Wazo lililotolewa la kutumia tume ndogo kuandaa mpango wa utelekelezaji/Action Plan,kwa mapendekezo yote na kuanisha wahusika ni nani,time frame, budgetary requirements nk ni zuri zaidi.

Lakini nishauri pia hiyo hoja ya kuandika Concept Note ipewe kipaumbele zaidi,yaweza kusaidia kifedha na tukiinadi kwa wabia wetu wa haki za binadamu, demokrasia na utawala bora,ikiandikwa kwa weledi na viwango Bora na vya ushawishi murua,tunaweza kupata support kubwa zaidi toka kwa wenzetu maana kwao haya ni maeneo ya kimkakati na kiungwana kutuwezesha na huwa wanaguswa vyepesi na maeneo kama haya.
Tutangaze kandarasi kama wafanyavyo UNDP nk tupate wataalam wazuri watuandalie andiko zuri ili tulitembeze panapohusika.

I wish I would be given an opportunity to draft such a concept note...I would do it to my best talent to achieve the desired targets!
 
Hiki kiburi ni another level
Itungwe sheria ya wananchi kuwakamata watawala wabovu tuwaweke magereza mpaka further notice
 
Bonge la article
 
Nimekuwa mvivu wa kusoma ripoti kubwakubwa nategemea uchambuzi wa wadau wa forum hii ya jamii lakini kinyume na matarajio naona ukimya umetawala au DPW bado imeshika hatamu.?
 
Mama anazunguka mbuyu huyu,Itungwe sheria ya kuwaadhibu viongozi wanaofanya makosa period.Yaaan blah blah nyingiii.This county bwana,Aaaah
 
Kuna uzi nilitoa swala la jeshi la polisi swala la ukachero na upelelezi kuwa idara tofauti ila niliishia kushambuliwa na watu ambao itakuwa wapo idara hiyo.

Tumeona tume haki jinai imeeleza kila kitu kuhusu ili jambo na mapungufu yake.

Mda mwengine mtusikilize wananchi kasoro tunazoziona tena undani kabisa
 
Kwa hili, Kongole sana Mh Rais, ila isiwe maneno matupu fuatilia uone utekelezaji wake.
 
Mrejesho wa kamati unadhihirisha namna kulivyo na pengo kubwa la haki kwenye mtirirko wa utoaji na usimamizi wa haki nchini.

Jeshi la polisi livunjwe au sheria ya uundwaji wake iboreshwe mpaka jina lake
 
Nina uhakika hujasikiliza kilichosemwa
 
Samia ni kama ceremonial president, amepwaya sana kwenye mambo ya msingi, yeye anachoweza ni teua, tengua, apisha, na ufunguzi..
Haisaidii. She still The President of URT hata umchukie vp
 
Mtaje kwanza na bei iliyouziwa
Kama ambavyo Loliondo iliuzwa hatukuambiwa tulishangaa watu wanahamishwa anakabidhiwa mnunuzi ndivyo bandari ilivyouzwa sirini tukashangaa kuona kataba la kimangungo. Siku ukiona unafukuzwa kwenye shamba lako na unaambiwa ni mali ya mtu mwingine jua limeshapigwa bei bila wewe kujua hata ukiuliza bei hutaambiwa sasa usishangae bandari imeuzwa kwa mabadilishano na kioo cha kujitazama.
 
hakuna Raia ana haki yoyote Polisi

sana sana Polisi akikukamata ni kama kakamata paka tu.

Jeshi la polisi lichunguzwe sana Raia tunapitia madhira mengi kupitia Polisi.

Polisi akija kukukamataka kitu atakachochukua uhesabu maumivu maana hutakipata tena …
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…