Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki hafla utiaji saini Mkataba wa Usimamiaji wa Shughuli za Lishe leo tarehe 30 Septemba, katika Jengo la Kitega Uchumi jijini Dodoma
Ummy Mwalimu - Waziri wa Afya
Lishe bora ni msingi wa afya na uchumi wa mtu mmoja, familia na taifa kwa ujumla.
Utapiamlo unaleta madhara kiafya na kiuchumi, lishe bora ni muhimu.
Madaraja na miundombinu mingine inaweza kukarabatiwa baada ya kuharibika, ubongo wa mtoto hauwezi kukarabatika baada ya kuharibika.
Watoto milioni 3 Tanzania wamedumaa, hawafundishiki. Ubongo wao umedumaa, hawawezi kuwa wabunifu, hawawezi kujifunza mambo mapya.
Tunaanza kutoa kozi ya afisa lishe ngazi ya Astashahada kuanzia mwaka 2022/23 ili tupate wataalamu wengi wa kusimamia ajenda za lishe hadi sehemu ya chini kabisa.
Tuna tishio la ugonjwa wa Ebola ulio anzia Uganda. Tumetoa maelezo kwa wakuu wa mikoa, tuendelee kujipanga ili usiingie, na hata ukitokea umeingia tuweze kuudhibiti.
Innocent Bashungwa - Waziri TAMISEMI
Tumepokea pesa ya ujenzi wa madarasa 8000 nchi nzima. Zoezi hili tutalisimamia na kulitekeleza kwa ufanisi mkubwa.
Samia Suluhu Hassan - Rais
Nimezungumza na Waziri wa afya tusitishe kwanza ujenzi wa vituo vya afya, kwa sasa tuimarishe huduma kwanza pamoja na kuwekeza vifaa tiba ikiwemo pia kujenga nyumba za wahudumu.
Kasimamieni matunzo ya vifaa hivi vilivyo tolewa. Sitavumilia kusikia kifaa miezi 6 au mwaka mmoja kimeharibika. Aliyehusika atanieleza, na mtumiaji atanieleza.
Simamieni vizuri mkataba huu wa lishe ili matokeo tunayopanga yaweze kutimia.
Wajawazito wapewe lishe bora ili wazae watoto wenye afya bora, watoto hao nao wakizaliwa watunzwe vizuri ili baadae wawe watu wazima wenye afya bora.
Uchunguzi ufanyike kwanini vijana wetu wakifikia umri wa kuongeza jamii wanahangaika, ni mitindo ya maisha (kuwa slim lady) au utasikia supu ya pwenza….. tatizo kubwa hili, lipo kwenye lishe. Watafiti kachunguzeni.
Tukiacha mambo yaende hivi tutakuwa na taifa la watu goigoi, itafika mahali hatutajua mke ni nani na mme ni nani.
Tuna vitambi, udumavu na wengine wana uzito mdogo, vyotr hivi ni matokeo ya lishe mbaya.
Tuna changamoto ya uelewa mdogo kuanzia ngazi ya juu hadi kwa jamii ya chini kabisa, tujikague kwanza sisi watu wa juu, tunaelewa kweli haya mambo?
Hata huku juu tuna matatizo, unamuelekeza mtu jambo lilelile mara tano, bado haelewi. Unawaza, ni dharau, hataki au shida nini? Kumbe hujui historia yake (ya ukuaji)
Sekta ya kilimo iangaliwe upya, watu walime na wapate lishe ya kutosha. Ndiyo maana mwaka huu bajeti tumeiongeza zaidi.
Hatuna sababu yoyote ya kusingizia kwa nini tuna shida ya utapiamlo, tuna mito, ardhi nzuri, mvua n.k Twendeni kushughulikia haya mambo.
Fortification ya mazao na vyakula ifanyike kuanzia ngazi ya chini.
Swala la lishe linamgusa kila mtu, nataka nipate ripoti za lishe kila robo mwaka. Vijana wanakula sana chips, lakini mwisho wa siku vumbi la mkongo linahusika.
Wakuu wa wilaya hamfanyi kazi, mnasubiri mkeka. Sikusema nitawabadilisha leo au kesho, kwahiyo kama hamfanyi kazi hao ndiyo wangu.
Kutoa mkeka ni kazi yangu na nitautoa wakati muafaka, wakuu wa mkoa nataka ripoti za wakuu wenu wa wilaya.
Ummy Mwalimu - Waziri wa Afya
Lishe bora ni msingi wa afya na uchumi wa mtu mmoja, familia na taifa kwa ujumla.
Utapiamlo unaleta madhara kiafya na kiuchumi, lishe bora ni muhimu.
Madaraja na miundombinu mingine inaweza kukarabatiwa baada ya kuharibika, ubongo wa mtoto hauwezi kukarabatika baada ya kuharibika.
Watoto milioni 3 Tanzania wamedumaa, hawafundishiki. Ubongo wao umedumaa, hawawezi kuwa wabunifu, hawawezi kujifunza mambo mapya.
Tunaanza kutoa kozi ya afisa lishe ngazi ya Astashahada kuanzia mwaka 2022/23 ili tupate wataalamu wengi wa kusimamia ajenda za lishe hadi sehemu ya chini kabisa.
Tuna tishio la ugonjwa wa Ebola ulio anzia Uganda. Tumetoa maelezo kwa wakuu wa mikoa, tuendelee kujipanga ili usiingie, na hata ukitokea umeingia tuweze kuudhibiti.
Innocent Bashungwa - Waziri TAMISEMI
Tumepokea pesa ya ujenzi wa madarasa 8000 nchi nzima. Zoezi hili tutalisimamia na kulitekeleza kwa ufanisi mkubwa.
Samia Suluhu Hassan - Rais
Nimezungumza na Waziri wa afya tusitishe kwanza ujenzi wa vituo vya afya, kwa sasa tuimarishe huduma kwanza pamoja na kuwekeza vifaa tiba ikiwemo pia kujenga nyumba za wahudumu.
Kasimamieni matunzo ya vifaa hivi vilivyo tolewa. Sitavumilia kusikia kifaa miezi 6 au mwaka mmoja kimeharibika. Aliyehusika atanieleza, na mtumiaji atanieleza.
Simamieni vizuri mkataba huu wa lishe ili matokeo tunayopanga yaweze kutimia.
Wajawazito wapewe lishe bora ili wazae watoto wenye afya bora, watoto hao nao wakizaliwa watunzwe vizuri ili baadae wawe watu wazima wenye afya bora.
Uchunguzi ufanyike kwanini vijana wetu wakifikia umri wa kuongeza jamii wanahangaika, ni mitindo ya maisha (kuwa slim lady) au utasikia supu ya pwenza….. tatizo kubwa hili, lipo kwenye lishe. Watafiti kachunguzeni.
Tukiacha mambo yaende hivi tutakuwa na taifa la watu goigoi, itafika mahali hatutajua mke ni nani na mme ni nani.
Tuna vitambi, udumavu na wengine wana uzito mdogo, vyotr hivi ni matokeo ya lishe mbaya.
Tuna changamoto ya uelewa mdogo kuanzia ngazi ya juu hadi kwa jamii ya chini kabisa, tujikague kwanza sisi watu wa juu, tunaelewa kweli haya mambo?
Hata huku juu tuna matatizo, unamuelekeza mtu jambo lilelile mara tano, bado haelewi. Unawaza, ni dharau, hataki au shida nini? Kumbe hujui historia yake (ya ukuaji)
Sekta ya kilimo iangaliwe upya, watu walime na wapate lishe ya kutosha. Ndiyo maana mwaka huu bajeti tumeiongeza zaidi.
Hatuna sababu yoyote ya kusingizia kwa nini tuna shida ya utapiamlo, tuna mito, ardhi nzuri, mvua n.k Twendeni kushughulikia haya mambo.
Fortification ya mazao na vyakula ifanyike kuanzia ngazi ya chini.
Swala la lishe linamgusa kila mtu, nataka nipate ripoti za lishe kila robo mwaka. Vijana wanakula sana chips, lakini mwisho wa siku vumbi la mkongo linahusika.
Wakuu wa wilaya hamfanyi kazi, mnasubiri mkeka. Sikusema nitawabadilisha leo au kesho, kwahiyo kama hamfanyi kazi hao ndiyo wangu.
Kutoa mkeka ni kazi yangu na nitautoa wakati muafaka, wakuu wa mkoa nataka ripoti za wakuu wenu wa wilaya.