Rais Samia ashiriki Misa Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Oktoba 14, 2023

Rais Samia ashiriki Misa Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Oktoba 14, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akishiriki Misa Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere leo tarehe 14 Oktoba, 2023 Babati, Mkoani Manyara.


View: https://www.youtube.com/live/KmuRAUC9pSQ?si=GqCzOhpasVu7Yf4w

HOMILIA YA ANTHONY LAGWEN, ASKOFU JIMBO KATOLIKI MBULU

Hayati Baba wa Taifa alivipiga vita vizuri hadi mwendo alipoumaliza, vita vizuri dhidi ya ujinga, maradhi, umasikinj, rushwa na ufisadi. Alikuwa kiongozi mpatanishi ndani na nje ya mipaka yetu.
Alikuwa kiongozi mzalendo kwelikweli. Tulipata bahati ya kuongozwa na mtu aliyemcha mwenyezi Mungu. Alikuwa kiongozi mwenye upendo na mwema.

Bado ni hazina kwa wanasiasa na wananchi. Alipenda kumsikiliza mwenyezi Mungu hivyo alijariwa hekima na busara. Aling’aa, alijaliwa maono ambayo sisi tunachukulia kama utabiri.

Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha yake, kwa kuonesha mengi ya kufaa tena yenye mkono wa mwenyezi Mungu.

Ili tumuenzi vizuri inafaa tutambue kuwa amani, umoja na mshikamano ni msingi wa maendeleo ya kweli. Tutambue kwamba tuna jukumu la kulinda amani, tuna wajibu wa kuleta maisha ya fadhira na dhamiri njema, tukwepe kupuuza au kushabikia uovu au jambo lolote tunaloona ni aibu kwa mtu au fedheha kwa taifa letu, mambo kama ushoga, usagaji na biashara ya binadamu yanapaswa kupigwa vita.

Baada ya kifo ni hukumu, mengine ni ibada za wafu na ibada za sanamu zifanywazo na wasio amini/wapagani.
Aliye andaaa hiyo misa ametukosea sana wakatoliki sisi hatuamini ibada za wafu.
 
Back
Top Bottom