johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
TunasherehekeaSwali.
Leo tunaomboleza au tunashereheka?
Mwenyeheri Julius Nyerere 😂
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
TunasherehekeaSwali.
Leo tunaomboleza au tunashereheka?
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akishiriki Misa Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere leo tarehe 14 Oktoba, 2023 Babati, Mkoani Manyara.
View: https://www.youtube.com/live/KmuRAUC9pSQ?si=GqCzOhpasVu7Yf4w
HOMILIA YA ANTHONY LAGWEN, ASKOFU JIMBO KATOLIKI MBULU
Hayati Baba wa Taifa alivipiga vita vizuri hadi mwendo alipoumaliza, vita vizuri dhidi ya ujinga, maradhi, umasikinj, rushwa na ufisadi. Alikuwa kiongozi mpatanishi ndani na nje ya mipaka yetu.
Alikuwa kiongozi mzalendo kwelikweli. Tulipata bahati ya kuongozwa na mtu aliyemcha mwenyezi Mungu. Alikuwa kiongozi mwenye upendo na mwema.
Bado ni hazina kwa wanasiasa na wananchi. Alipenda kumsikiliza mwenyezi Mungu hivyo alijariwa hekima na busara. Aling’aa, alijaliwa maono ambayo sisi tunachukulia kama utabiri.
Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha yake, kwa kuonesha mengi ya kufaa tena yenye mkono wa mwenyezi Mungu.
Ili tumuenzi vizuri inafaa tutambue kuwa amani, umoja na mshikamano ni msingi wa maendeleo ya kweli. Tutambue kwamba tuna jukumu la kulinda amani, tuna wajibu wa kuleta maisha ya fadhira na dhamiri njema, tukwepe kupuuza au kushabikia uovu au jambo lolote tunaloona ni aibu kwa mtu au fedheha kwa taifa letu, mambo kama ushoga, usagaji na biashara ya binadamu yanapaswa kupigwa vita.